Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 1

“Barĩa Bacwaga Jehova Gũtĩ Gĩntũ Gĩkĩega Bakaaga”

“Barĩa Bacwaga Jehova Gũtĩ Gĩntũ Gĩkĩega Bakaaga”

ĨANDĨKO RĨA MWAKA JWA 2022: “Barĩa bacwaga Jehova gũtĩ gĩntũ gĩkĩega bakaaga.”​—ZAB. 34:10, NWT.

RWĨMBO 4 “Yehova Ni Mchungaji Wangu”

MUHTASARI *

Daudi alihisi kwamba ‘hakukosa chochote chema’ hata wakati alipokabili hali ngumu (Tazama fungu la 1 hadi 3) *

1. Daudi aciĩthĩĩre ũntũne bũrĩkũ bũbũũmũ?

 DAUDI alikuwa akikimbia ili kuokoa uhai wake. Sauli, mfalme mwenye nguvu wa Israeli, alikuwa ameazimia kumuua. Daudi alipohitaji chakula, alifika katika jiji la Nobu, ambapo aliomba apatiwe mikate mitano tu. (1 Sam. 21:1, 3) Baadaye, yeye na wanaume wake walijificha kwenye pango. (1 Sam. 22:1) Daudi alijikutaje katika hali hiyo?

2. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ Saũlũ aciĩkĩĩre ũgwatine? (1 Samweli 23:16, 17)

2 Sauli alimwonea wivu sana Daudi kwa sababu ya umaarufu wake na ushindi aliopata vitani. Pia, Sauli alijua kwamba Yehova alikuwa amemkataa yeye kuwa mfalme wa Israeli kwa sababu hakumtii na kwamba Yehova alikuwa amemchagua Daudi awe mfalme wakati ujao. (Soma 1 Samweli 23:16, 17.) Akiwa mfalme wa Israeli, bado Sauli alikuwa na jeshi kubwa na wafuasi wengi, hivyo Daudi alihitaji kukimbia ili kuokoa uhai wake. Je, kweli Sauli alifikiri kwamba angefaulu kumzuia Mungu asimfanye Daudi kuwa mfalme? (Isa. 55:11) Biblia haisemi, lakini tunaweza kuwa na uhakika na jambo hili: Sauli alikuwa akijihatarisha mwenyewe. Sikuzote wale wanaompinga Mungu hushindwa!

3. Nĩatĩa Daudi aigĩrue kinya kwethĩrwa nacemanagia na mantũ jamoomũ?

3 Daudi hakuwa akijitafutia makuu. Hakujiamulia mwenyewe kwamba atakuwa mfalme wa Israeli. Yehova ndiye aliyempa jukumu hilo. (1 Sam. 16:1, 12, 13) Sauli alimchukia sana Daudi. Lakini Daudi hakumlaumu Yehova kwa sababu ya hatari aliyokabili; wala hakulalamika kwa sababu hakuwa na chakula cha kutosha na kulazimika kuishi kwenye pango. Badala yake, inawezekana kwamba alipokuwa amejificha katika pango hilo, ndipo alipotunga wimbo mzuri wa sifa unaotia ndani maneno ya andiko letu la msingi: “Wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.”​—Zab. 34:10.

4. Nĩ biũria birĩkũ tũgacũnkũũna, na nĩkĩ birĩ bia bata?

4 Leo, watumishi wengi wa Yehova hawana chakula cha kutosha na mahitaji mengine ya muhimu maishani. * Wengi wamepitia hali hiyo hasa katika kipindi cha janga la COVID-19. Na mambo yatazidi kuwa magumu kadiri “dhiki kuu” inavyozidi kukaribia. (Mt. 24:21) Tukiwa na mambo hayo akilini, acheni tujibu maswali haya manne: Ni kwa njia gani Daudi ‘hakukosa chochote chema’? Kwa nini tunapaswa kujifunza kuridhika? Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atatutunza? Na tunaweza kujitayarishaje sasa kwa ajili ya wakati ujao?

“GUTI GANTU MBAGIKIA”

5-6. Zaburi 23:1-6 nĩatĩa ĩtũtethagia gũtaũkĩrwa ũrĩa Daudi endaga tũciũkĩrwa rĩrĩa augĩre atumĩkĩri ba Mũrungũ “gũtĩ gĩntũ gĩkĩega bakaaga”?

5 Daudi alimaanisha nini aliposema kwamba watumishi wa Yehova “hawatakosa chochote chema”? Tunaweza kupata jibu kwa kuchunguza maneno ambayo yanafanana na hayo kwenye Zaburi ya 23. (Soma Zaburi 23:1-6.) Daudi anaanza zaburi hiyo kwa maneno haya: “Yehova ni Mchungaji wangu. Sitakosa chochote.” Katika sehemu inayobaki ya zaburi hiyo, Daudi anataja mambo ambayo kwa kweli yana thamani inayodumu, yaani, baraka nyingi za kiroho ambazo alifurahia kwa kukubali Yehova awe Mchungaji wake. Yehova alimwongoza “katika njia za uadilifu,” na kumtegemeza Daudi kwa ushikamanifu katika nyakati nzuri na nyakati ngumu. Hata ingawa alikuwa katika “malisho yenye majani mengi” ya Yehova, Daudi alitambua kwamba angekabili matatizo maishani mwake. Nyakati nyingine, huenda angevunjika moyo na kuhisi kwamba alikuwa akitembea “katika bonde lenye kivuli kizito,” na angekuwa na maadui. Lakini kwa sababu Yehova alikuwa Mchungaji wake, Daudi ‘hangeogopa madhara yoyote.’

6 Basi tumepata jibu la swali letu: Ni kwa njia gani Daudi ‘hakukosa chochote chema’? Kwa njia ya kiroho, alikuwa na kila kitu alichohitaji. Furaha yake haikutegemea vitu vya kimwili. Daudi aliridhika na mambo ambayo Yehova alimwandalia. Jambo muhimu zaidi kwake lilikuwa kupata baraka na ulinzi wa Mungu wake.

7. Kũringana na Luka 21:20-24, Akristũ ba karine ya mbere barĩa batũũraga Judea bacemanirie na mantũ jarĩkũ jamoomũ?

7 Kutokana na maneno ya Daudi tunaweza kuona jinsi ilivyo muhimu kwetu kuwa na maoni yanayofaa kuhusu vitu vya kimwili. Bila shaka, tunaweza kufurahia vitu vya kimwili tulivyo navyo, lakini havipaswi kuwa jambo kuu katika maisha yetu. Wakristo wa karne ya kwanza waliokuwa wanaishi Yudea, walikuja kuelewa kweli hiyo muhimu. (Soma Luka 21:20-24.) Yesu alikuwa amewaonya kuhusu wakati ambapo jiji la Yerusalemu ‘lingezingirwa na majeshi yaliyopiga kambi.’ Hilo lilipotukia walipaswa ‘kuanza kukimbilia milimani.’ Ikiwa wangekimbia wangeokoka, lakini wangeacha vitu vingi sana. Miaka kadhaa iliyopita, gazeti la Mnara wa Mlinzi lilisema hivi: “Waliacha mashamba na nyumba, hata hawakukusanya mali zao kutoka katika nyumba zao. Huku wakiwa na uhakika katika ulinzi na utegemezo wa Yehova, walitanguliza ibada yake kuliko kitu kingine chochote ambacho kingeonekana kuwa muhimu.”

8. Tũũmba kwiritana kĩthoomo kĩrĩkũ kĩa bata kuumania na mantũ jarĩa jagwatire Akristũ ba karine ya mbere baria batũũraga Judea?

8 Tunaweza kujifunza somo gani muhimu kutokana na mambo yaliyowapata Wakristo wa karne ya kwanza walioishi Yudea? Gazeti la Mnara wa Mlinzi lililotajwa katika fungu lililotangulia, lilisema hivi: “Huenda majaribu yako mbele kuhusiana na jinsi tunavyoziona mali za kimwili; je, hivyo ndivyo vitu muhimu zaidi, au je, ule wokovu utakaowajia wale wote walio upande wa Mungu ni wa muhimu zaidi? Naam, huenda kukimbia kwetu kukahusisha magumu fulani na hasara. Itatubidi tuwe tayari kufanya lolote lihitajiwalo, kama walivyofanya Wakristo wenzetu wa karne ya kwanza, ambao walikimbia kutoka Yudea.” *

9. Nĩatĩa ũtaaro bwa mũtũmwa Paũlũ kĩrĩ Ahibirania bũgũgwĩkĩra inya?

9 Je, unaweza kuwazia jinsi ilivyokuwa vigumu kwa Wakristo hao kuacha karibu kila kitu walichokuwa nacho na kuanza maisha mapya? Walihitaji kuwa na imani ili kumtegemea Yehova kwa ajili ya mahitaji yao ya msingi. Lakini kulikuwa na jambo ambalo lingewasaidia. Miaka mitano kabla ya Waroma kulizingira jiji la Yerusalemu, mtume Paulo aliwapa Waebrania ushauri huu muhimu: “Njia yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mkiridhika na vitu mlivyo navyo. Kwa maana amesema: ‘Sitakuacha wala kukutupa kamwe.’ Ili tuwe hodari na kusema: ‘Yehova ni msaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu atanifanya nini?’” (Ebr. 13:5, 6) Bila shaka, ilikuwa rahisi kwa wale waliochukua kwa uzito ushauri wa mtume Paulo kabla ya shambulizi la Waroma, kuzoea maisha rahisi katika makao yao mapya. Walikuwa na uhakika kwamba Yehova angewaandalia mahitaji yao ya msingi. Maneno ya mtume Paulo yanatusadikishia kwamba sisi pia tunaweza kuwa na uhakika huohuo.

“TWANGˈANWA NI INTO BIU”

10. Nĩ “witho” bũrĩkũ Paũlũ agũtũmenyithia?

10 Paulo alimpatia Timotheo ushauri unaofanana na huo, na ambao pia unatuhusu. Aliandika hivi: “Basi, tukiwa na chakula na mavazi, tutaridhika na vitu hivyo.” (1 Tim. 6:8) Je, hilo linamaanisha kwamba hatuwezi kufurahia mlo mzuri, kuwa na mahali pazuri pa kuishi, au kununua mavazi mapya mara kwa mara? Paulo hakuwa akimaanisha hivyo. Alikuwa akimaanisha kwamba tunapaswa kuridhika na vitu vya kimwili tulivyo navyo. (Flp. 4:12) Hiyo ndiyo iliyokuwa “siri” ya Paulo. Uhusiano wetu pamoja na Yehova ndilo jambo lenye thamani zaidi tulilo nalo, si vitu vya kimwili tulivyo navyo.​—Hab. 3:17, 18.

Waisraeli ‘hawakukosa chochote’ walipokuwa nyikani kwa miaka 40. Je, tunaweza kuridhika na vitu tulivyo navyo sasa? (Tazama fungu la 11) *

11. Nĩmbi tũkwiritana biegie kũngˈanĩrwa kumania na biugo bia Musa kĩrĩ Aisraeli?

11 Huenda kukawa na tofauti kati ya maoni yetu na maoni ya Yehova kuhusu mambo tunayohitaji. Fikiria mambo ambayo Musa aliwaambia Waisraeli baada ya kukaa miaka 40 nyikani: “Yehova Mungu wenu amewabariki katika mambo yote mliyofanya. Anajua vizuri kabisa safari yenu katika nyika hii kubwa. Yehova Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi kwa miaka hii 40, nanyi hamjakosa kitu chochote.” (Kum. 2:7) Wakati wa miaka hiyo 40, Yehova aliwaandalia Waisraeli mana. Nguo zao, yaani, nguo zilezile ambazo walitoka nazo Misri, hazikuchakaa. (Kum. 8:3, 4) Ingawa huenda baadhi walihisi maandalizi hayo hayakutosha, Musa aliwakumbusha Waisraeli kwamba walikuwa na kila kitu walichohitaji. Yehova atafurahi ikiwa tutajifunza kuridhika, yaani, kuthamini hata maandalizi rahisi anayotuandalia na kuyaona kuwa baraka na kumshukuru.

ĨTHĨRWA NA MMA ATĨ JEHOVA AGAKŨMENYEERA

12. Nĩmbi bikwonania Daudi nerĩgĩrĩĩre Jehova, na ataciĩrĩgĩrĩĩre wengwa?

12 Daudi alijua kwamba Yehova ni mshikamanifu na anawajali sana wale wanaompenda. Ingawa uhai wake ulikuwa hatarini alipotunga Zaburi ya 34, kwa macho ya imani Daudi alimwona “malaika wa Yehova” akipiga kambi ‘pande zote kumzunguka.’ (Zab. 34:7) Labda Daudi alikuwa akimlinganisha malaika wa Yehova na mwanajeshi aliyepiga kambi, sikuzote akiwa macho ili kumwona adui. Ingawa Daudi mwenyewe alikuwa mwanamume mwenye nguvu wa vita na Yehova alikuwa amemwahidi ufalme, hakutegemea uwezo wake wa kurusha mawe kwa kombeo au kutumia upanga ili kumshinda adui. (1 Sam. 16:13; 24:12) Daudi alimtumaini Mungu akiwa na uhakika kwamba malaika wa Yehova ‘huwaokoa wale wanaomwogopa Yeye.’ Bila shaka, leo hatutarajii kulindwa kimuujiza. Lakini tunajua kwamba wote wanaomtumaini Yehova hawatapata madhara ya kudumu.

Wakati wa dhiki kuu, huenda majeshi ya Gogu wa Magogu yakajaribu kutushambulia tukiwa nyumbani. Lakini tunafarijika kujua kwamba Yesu na malaika wake wanajua kinachotukia nao watatulinda (Tazama fungu la 13)

13. Nĩkĩ tũkonekana teka tũtĩ na ũkaria rĩrĩa Gogu wa Magogu agatwithũkĩra, na nĩkĩ tũtĩkĩra? (Tega mbica karatacine ka mbere.)

13 Hivi karibuni, uhakika wetu katika uwezo wa Yehova wa kutulinda utajaribiwa. Gogu wa Magogu, yaani, muungano wa mataifa, utakapowashambulia watu wa Mungu, maisha yetu yataonekana kuwa hatarini. Tutahitaji kusadiki kabisa kwamba Yehova anaweza na atatuokoa. Mataifa hayo, yatatuona kama kondoo wasioweza kujitetea ambao hawana mtu wa kuwalinda. (Eze. 38:10-12) Hatutakuwa na silaha, wala mazoezi ya vita. Mataifa yataona kwamba ni rahisi kutushinda. Hawataona kile tutakachoona kwa macho ya imani, yaani, malaika wengi waliopiga kambi kuwazunguka watu wa Mungu, wakiwa tayari kutulinda. Ni wazi kwamba mataifa hayatawaona, kwa kuwa hawana macho ya kiroho. Watashangaa sana jeshi la mbinguni litakapokuja kutusaidia!​—Ufu. 19:11, 14, 15.

ITHURANĨRE NANDĨ TONTŨ BWA ĨGIITA RĨĨJĨTE

14. Tũũmba kũjũkia matagaaria jarĩkũ nandĩ kenda twithuranĩra tontũ bwa ĩgiita rĩĩjĩte?

14 Tunaweza kufanya nini sasa ili kujitayarisha kwa ajili ya wakati ujao? Kwanza kabisa, tunahitaji kuwa na mtazamo unaofaa kuhusu vitu vya kimwili, tukitambua kwamba siku moja tutaviacha. Pia, tunahitaji kuridhika na kupata shangwe kubwa zaidi katika uhusiano wetu na Yehova. Kadiri tunavyomjua vizuri zaidi Mungu wetu, ndivyo tutakavyosadiki zaidi kwamba atatulinda tutakaposhambuliwa na Gogu wa Magogu.

15. Nĩ mantũ jarĩkũ Daũdi acioneere jarĩa jamũritanĩre atĩ Jehova atĩũmba kũmũtiganĩria?

15 Fikiria jambo lingine lililomsaidia Daudi na linaloweza kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya majaribu. Daudi alisema hivi: “Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema; mwenye furaha ni mtu anayemkimbilia.” (Zab. 34:8) Maneno hayo yanaonyesha kwa nini Daudi alijua kwamba angeweza kumtegemea Yehova. Mara nyingi Daudi alimtegemea Yehova, na sikuzote Mungu alimsaidia. Alipokuwa kijana, Daudi alikabiliana na Goliathi, jitu la Wafilisti, na akamwambia hivi mpiganaji huyo mwenye nguvu: “Siku hii ya leo Yehova atakutia wewe mikononi mwangu.” (1 Sam. 17:46) Baadaye, Daudi alikuwa mtumishi wa Mfalme Sauli, ambaye alijaribu mara kadhaa kumuua. Lakini “Yehova alikuwa pamoja” na Daudi. (1 Sam. 18:12) Kwa sababu Daudi alikuwa amejionea jinsi Yehova alivyomsaidia wakati uliopita, alijua kwamba angeweza kumtegemea Mungu nyakati hizo.

16. Nĩ gũkũrũkĩĩra njĩra ĩrĩkũ yongwa tũũmba “gũcema” wega bwa Jehova?

16 Kadiri tunavyomtegemea Yehova ili atupatie mwongozo sasa, ndivyo tutakavyokuwa na uhakika zaidi katika uwezo wake wa kutuokoa wakati ujao. Tunahitaji kuwa na imani na kuwa tayari kumtegemea Yehova tunapomwomba mwajiri wetu ruhusa ili tuhudhurie makusanyiko, au tunapoomba kubadili ratiba yetu ya kazi ili tuweze kuhudhuria mikutano yetu yote na kupata muda zaidi kwa ajili ya utumishi. Tuseme mwajiri wetu anakataa ombi letu na tunapoteza kazi. Je, tuna imani kwamba Yehova hatatuacha, wala kutusahau kamwe na kwamba sikuzote atatuandalia mahitaji yetu ya msingi? (Ebr. 13:5) Watumishi wengi wa wakati wote wamejionea mara nyingi jinsi Yehova alivyowategemeza walipohitaji sana msaada wake. Yehova ni mwaminifu.

17. Ĩandĩko rĩa mwaka jwa 2022 nĩ rĩrĩkũ, na nĩkĩ rĩkwagĩra?

17 Yehova akiwa upande wetu, hatuna sababu ya kuogopa mambo yatakayotokea wakati ujao. Mungu wetu hatatuacha kamwe maadamu tunatanguliza mapenzi yake maishani. Ili kutukumbusha umuhimu wa kujitayarisha sasa kwa ajili ya hali ngumu tutakazokabili wakati ujao na kuwa na uhakika kwamba Yehova hatatuacha kamwe, Baraza Linaloongoza limechagua Zaburi 34:10 kuwa andiko letu la mwaka wa 2022: “Wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.”

RWĨMBO 38 Atakupa Nguvu

^ Andiko la mwaka wa 2022 limetolewa kwenye Zaburi 34:10: “Wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.” Watumishi wengi waaminifu wa Yehova hawana pesa au mali nyingi. Basi kwa nini tunaweza kusema kwamba ‘hawakosi chochote chema’? Na kuelewa maana ya mstari huo kunaweza kutusaidiaje kujiandaa kwa ajili ya hali ngumu za wakati ujao?

^ Tazama “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 2014.

^ MAELEZO YA PICHA: Hata alipokuwa amejificha pangoni ili kumkimbia Mfalme Sauli, Daudi alithamini maandalizi ya Yehova.

^ MAELEZO YA PICHA: Baada ya Waisraeli kuondoka Misri, Yehova aliwaandalia mana na kutunza nguo zao ili zisichakae.