Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 2

Iritane Kuuma Kĩrĩ Mũtaana-O-Ngˈina wa Jesũ Ũrĩa Mũniini

Iritane Kuuma Kĩrĩ Mũtaana-O-Ngˈina wa Jesũ Ũrĩa Mũniini

“Jakubu, nthumba ya Murungu na ya Mwathani wetu Jesu Kristu.”​—JAK. 1:1.

RWĨMBO 88 Nijulishe Njia Zako

MUHTASARI *

1. Nĩatĩa ũũmba gũtaarĩĩria famĩrĩ ĩrĩa Jakubu arereerwe?

 YAKOBO, ndugu ya Yesu, alilelewa katika familia iliyokuwa na hali nzuri sana ya kiroho. * Wazazi wake, Yosefu na Maria, walimpenda sana Yehova na walimtumikia kwa moyo wote. Yakobo alikuwa na pendeleo lingine​—baadaye ndugu yake mkubwa angekuwa Masihi aliyeahidiwa. Yakobo alikuwa na pendeleo kubwa sana la kuwa katika familia hiyo!

Alipokuwa akilelewa pamoja na Yesu, Yakobo alimfahamu vizuri sana ndugu yake mkubwa (Tazama fungu la 2)

2. Jakubu arĩ na itũmi birĩkũ bia kwenda na gũtĩa mũtaana-o-ngˈina ũrĩa mũkũrũ?

2 Yakobo alikuwa na sababu nyingi za kumpenda na kumheshimu ndugu yake mkubwa. (Mt. 13:55) Kwa mfano, Yesu aliyafahamu sana Maandiko alipokuwa na umri wa miaka 12, hivi kwamba aliwashangaza wazee wenye elimu huko Yerusalemu. (Luka 2:46, 47) Huenda Yakobo alifanya kazi ya useremala pamoja na Yesu. Ikiwa ndivyo, basi alimfahamu vizuri sana ndugu yake. Nathan H. Knorr alipenda kusema hivi: “Unapofanya kazi pamoja na mtu unajifunza mengi kumhusu.” * Pia, inaelekea Yakobo aliona jinsi ‘Yesu alivyoendelea kukua na kupata hekima zaidi, na alivyozidi kupata kibali cha Mungu na wanadamu.’ (Luka 2:52) Hivyo, huenda tukadhani kwamba Yakobo alikuwa kati ya wanafunzi wa kwanza wa Yesu. Lakini haikuwa hivyo.

3. Jakubu etĩkĩrĩĩrie atĩa Jesũ akwambĩrĩrĩa ũtungatĩri bwawe?

3 Wakati wa huduma ya Yesu duniani, Yakobo hakuwa mmoja wa wanafunzi wake. (Yoh. 7:3-5) Isitoshe, huenda Yakobo alikuwa miongoni mwa watu wa ukoo wa Yesu waliofikiri kwamba “amerukwa na akili.” (Marko 3:21) Na hakuna jambo linaloonyesha kwamba Yakobo alikuwa pamoja na Maria, mama yao, Yesu alipotundikwa kwenye mti wa mateso.​—Yoh. 19:25-27.

4. Nĩ mantũ jarĩkũ tũgacũnkũũna?

4 Baadaye, Yakobo alimwamini Yesu na akawa mzee aliyeheshimika katika kutaniko la Kikristo. Katika makala hii, tutachunguza mambo mawili tunayoweza kujifunza kutoka kwa Yakobo: (1) kwa nini tunapaswa kuendelea kuwa wanyenyekevu na (2)  tunawezaje kuwa walimu bora?

ĨTA NA MBERE KWĨTHĨRWA WĨNYIĨTIE TA JAKUBU

Yakobo alijinyenyekeza Yesu alipomtokea, na tangu wakati huo akawa mwanafunzi mwaminifu wa Kristo (Tazama fungu la 5 hadi 7)

5. Nĩatĩa Jakubu etĩkĩrĩĩrie Jesũ akũmumĩĩra nyuma ya kũriũkua?

5 Yakobo alianza kuwa mfuasi mshikamanifu wa Yesu lini? Baada ya Yesu kufufuliwa, “alimtokea Yakobo, kisha mitume wote.” (1 Kor. 15:7) Baada ya kukutana na Yesu, Yakobo akawa mwanafunzi wake. Alikuwepo mitume walipokuwa wakisubiri roho takatifu iliyoahidiwa, katika chumba cha juu huko Yerusalemu. (Mdo. 1:13, 14) Baadaye, Yakobo alikuwa na pendeleo la kutumikia akiwa mshiriki wa baraza linaloongoza la karne ya kwanza. (Mdo. 15:6, 13-22; Gal. 2:9) Na muda fulani kabla ya mwaka wa 62 W.K., aliongozwa na roho kuwaandikia barua Wakristo watiwa-mafuta. Barua hiyo inatunufaisha sisi leo, iwe tuna tumaini la kuishi mbinguni au duniani. (Yak. 1:1) Kulingana na mwanahistoria wa karne ya kwanza, Yosefo, Yakobo aliuawa kufuatia agizo la Kuhani Mkuu Myahudi Anania Mdogo. Yakobo aliendelea kuwa mwaminifu kwa Yehova hadi mwisho wa maisha yake hapa duniani.

6. Nĩ na njĩra irĩkũ Jakubu aarĩ mwanya na atongeeria ba dini ba ntukũ ciawe?

6 Yakobo alikuwa mnyenyekevu. Kwa nini tunaweza kusema hivyo? Fikiria tofauti kati ya jinsi ambavyo mwishowe Yakobo alimkubali Yesu, na jinsi viongozi wengi wa kidini walivyotenda. Yakobo alipopata uthibitisho ulio wazi kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, alikubali kwa unyenyekevu. Lakini wakuu wa makuhani huko Yerusalemu hawakufanya hivyo. Kwa mfano, hawangeweza kupinga kwamba Yesu alikuwa amemfufua Lazaro. Badala ya kukubali kwamba Yesu alikuwa ametumwa na Yehova, walijaribu kumuua Yesu na Lazaro. (Yoh. 11:53; 12:9-11) Baadaye, Yesu mwenyewe alipofufuliwa walipanga njama ya kuficha jambo hilo ili watu wasijue. (Mt. 28:11-15) Kwa sababu ya kiburi chao, viongozi hao wa kidini walimkataa Masihi.

7. Nĩkĩ tũbwĩri gũciebania na rwikumio?

7 Somo: Usiwe na kiburi, na uwe tayari kufundishwa. Kama vile ugonjwa unavyoweza kufanya mishipa halisi ya moyo iwe migumu na moyo uache kufanya kazi vizuri, vivyo hivyo kiburi kinaweza kuufanya moyo wetu wa mfano uwe mgumu na kutuzuia kutii mwongozo wa Yehova. Mafarisayo waliruhusu moyo wao uwe mgumu hivi kwamba wakakataa uthibitisho ulio wazi wa roho takatifu ya Mungu. (Yoh. 12:37-40) Uamuzi wao ulikuwa na matokeo mabaya kwa sababu uliwazuia kupata uzima wa milele. (Mt. 23:13, 33) Ni muhimu sana kwetu kuendelea kuruhusu Neno la Mungu na roho yake kuendelea kuongoza fikira na maamuzi yetu! (Yak. 3:17) Kwa kuwa Yakobo alikuwa mnyenyekevu, alikubali kufundishwa na Yehova. Na kama tutakavyoona, unyenyekevu wake ulimsaidia kuwa mwalimu bora.

ĨTHĨRWA ŨRĨ MWARIMŨ ŨMWEGA TA JAKUBU

8. Nĩmbi bĩgatũtethia kwaa arimũ babega?

8 Yakobo hakuwa na elimu nyingi ya ulimwengu. Bila shaka, viongozi wa kidini wa siku zake walimwona Yakobo kama walivyowaona mtume Petro na Yohana, yaani, kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” (Mdo. 4:13) Lakini Yakobo alijifunza kuwa mwalimu bora, kama inavyoonekana kwenye kitabu kinachoitwa kwa jina lake. Kama Yakobo, huenda tukawa na kiwango kidogo cha elimu ya ulimwengu. Hata hivyo, kwa msaada wa roho ya Yehova na mazoezi tunayopata katika tengenezo lake, sisi pia tunaweza kuwa walimu wazuri. Acheni tuchunguze mfano ambao Yakobo alituwekea akiwa mwalimu na tuone mambo tunayoweza kujifunza.

9. Nĩatĩa ũũmba gũtaarĩĩria njĩra ya Jakubu ya kũritana?

9 Yakobo hakutumia maneno magumu au ufafanuzi ulio mgumu kueleweka. Matokeo ni kwamba wasomaji wake walijua mambo waliyohitaji kufanya na jinsi ya kuyafanya. Kwa mfano, fikiria jinsi Yakobo alivyofundisha kwa njia rahisi kwamba Wakristo wanapaswa kuwa tayari kutendewa isivyo haki bila kuwa na kinyongo. Aliandika hivi: “Tunawaona wale ambao wamevumilia kuwa wenye furaha. Mmesikia kuhusu uvumilivu wa Ayubu na mmeona matokeo ambayo Yehova alileta, kwamba Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.” (Yak. 5:11) Ona kwamba mafundisho ya Yakobo yalitegemea Maandiko. Alitumia Neno la Mungu kuwasaidia wasomaji wake waone kwamba sikuzote Yehova huwathawabisha wale ambao kama Ayubu, ni washikamanifu Kwake. Yakobo alifundisha somo hilo kwa kutumia maneno rahisi na yanayopatana na akili. Kwa kufanya hivyo, alimletea Yehova sifa, badala ya kujielekezea fikira.

10. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ ĩmwe tũũmba kwigerekania na Jakubu rĩrĩa tũkũritana?

10 Somo: Fundisha kwa njia rahisi, na utumie Neno la Mungu. Lengo letu si kuwaonyesha watu kwamba tunajua mambo mengi, bali ni kuwaonyesha jinsi Yehova alivyo na ujuzi mwingi na anavyowajali sana. (Rom. 11:33) Tunaweza kufikia lengo hilo ikiwa sikuzote mambo tunayofundisha yanategemea Maandiko. Kwa mfano, badala ya kuwaambia wanafunzi wetu mambo ambayo tungefanya ikiwa tungekuwa katika hali kama yao, tunapaswa kuwasaidia wafikirie mifano iliyo katika Biblia na waelewe jinsi ambavyo Yehova anafikiri na kuhisi. Kisha watachochewa na tamaa yao ya kumfurahisha Yehova, na si sisi.

11. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomu bamwe ba Akristũ ba ntukũ cia Jakubu bacemanagia najo, na nĩ ũtaaro bũrĩkũ abaere? (Jakubu 5:13-15)

11 Yakobo aliona mambo kihalisi. Kutokana na barua yake, ni wazi kwamba Yakobo alitambua changamoto ambazo waabudu wenzake walikuwa wakipambana nazo, naye aliwapa mwongozo ulio wazi wa jinsi ya kuzishinda. Kwa mfano, baadhi ya Wakristo walisita kufuata ushauri wa Maandiko. (Yak. 1:22) Wengine waliwaonyesha upendeleo matajiri. (Yak. 2:1-3) Ilhali wengine walishindwa kudhibiti ulimi wao. (Yak. 3:8-10) Wakristo hao walikuwa na matatizo mazito, lakini Yakobo alikuwa na mtazamo mzuri kuwahusu. Aliwashauri kwa fadhili lakini kwa njia ya moja kwa moja. Na akawatia moyo wale waliokuwa na matatizo ya kiroho watafute msaada zaidi kutoka kwa wazee.​—Soma Yakobo 5:13-15.

12. Nĩatĩa tũũmba gwĩta na mbere kwĩthĩrwa na mwonere jũmwega rĩrĩa tũgũtethia aritwa beetũ ba Bibiria?

12 Somo: Ona mambo kihalisi, lakini uwe na mtazamo mzuri kuwahusu wengine. Huenda ikawa vigumu kwa watu wengi tunaojifunza nao kufuata ushauri wa Biblia. (Yak. 4:1-4) Huenda ikawachukua muda kuacha tabia zisizofaa, na kusitawisha sifa za Kikristo. Kwa kumwiga Yakobo, tunapaswa kuwa na ujasiri wa kuwaambia wanafunzi wetu mabadiliko wanayohitaji kufanya. Pia, tunahitaji kuendelea kuwa na mtazamo unaofaa, tukitumaini kwamba Yehova atawavuta kwake watu wanyenyekevu na atawapa nguvu za kufanya mabadiliko maishani mwao.​—Yak. 4:10.

13. O ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Jakubu 3:2 na nteto cia gaiti [NWT], nĩatĩa Jakubu aciũkĩrwe?

13 Yakobo alikuwa na maoni yaliyosawazika kujihusu. Yakobo hakujiona kuwa muhimu kuliko Wakristo wenzake kwa sababu ya familia yake au mapendeleo aliyokuwa nayo. Aliwaita waabudu wenzake “ndugu zangu wapendwa.” (Yak. 1:16, 19; 2:5) Hakutaka kujionyesha kuwa mkamilifu. Badala yake, alijihusisha aliposema: “Sisi sote hufanya makosa mara nyingi.”​—Soma Yakobo 3:2 na maelezo ya chini.

14. Nĩkĩ tũbwĩrĩte gwĩtĩkĩria maatia jeetũ?

14 Somo: Kumbuka kwamba sisi sote ni watenda dhambi. Hatupaswi kufikiri kwamba kwa njia fulani sisi ni bora kuliko wale tunaowafundisha. Kwa nini? Ikiwa tutamfanya mwanafunzi wetu afikiri kuwa sisi hatukosei, tutamfanya ahisi kwamba hawezi kamwe kumtii Mungu kikamili. Lakini ikiwa kwa unyoofu tunakiri kwamba sikuzote haijawa rahisi kwetu kufuata kanuni za Maandiko na kumweleza jinsi ambavyo Yehova ametusaidia kushinda changamoto zetu, tutamsaidia mwanafunzi wetu aone kwamba yeye pia anaweza kumtumikia Yehova.

Yakobo alitumia mifano rahisi, inayoeleweka wazi, na inayofaa (Tazama fungu la 15 na 16) *

15. Nĩatĩa ũũmba kuuga bwegie ngerekano iria Jakubu atũmĩĩre? (Jakubu 3:2-6, 10-12)

15 Yakobo alitumia mifano iliyogusa moyo. Bila shaka, alisaidiwa na roho takatifu, lakini inaelekea pia alijifunza mambo mengi kuhusu kufundisha kwa kuchunguza mifano ambayo Yesu, ndugu yake mkubwa, aliitumia. Mifano ambayo Yakobo alitumia katika barua yake ni rahisi, na masomo yako wazi.​—Soma Yakobo 3:2-6, 10-12.

16. Nĩkĩ tũbwĩrĩte gũtumĩra ngerekano iria ciagĩrĩte?

16 Somo: Tumia mifano inayofaa. Unapotumia mifano kwa ustadi, unamsaidia mwanafunzi awazie mambo anayojifunza. Unamsaidia kupiga picha akilini. Picha hizo huwasaidia wale wanaokusikiliza kukumbuka kweli muhimu za Biblia. Yesu alitumia mifano kwa ustadi sana, na Yakobo, ndugu yake, aliiga mfano wake. Acheni tuchunguze mojawapo kati ya mifano ambayo Yakobo alitumia na tuone kwa nini unafaa sana.

17. Nĩkĩ ngerekano ĩrĩa ĩrĩ kĩrĩ Jakubu 1:22-25 yagĩrĩte?

17 Soma Yakobo 1:22-25. Mfano wa Yakobo kuhusu kioo unafaa kwa sababu mbalimbali. Alikuwa akifundisha jambo hususa, yaani, ili tunufaike na Neno la Mungu, tunapaswa kufanya mengi zaidi ya kulisoma tu; ni lazima tutende kulingana na mambo tunayosoma. Yakobo alichagua mfano ambao wasikilizaji wake wangeuelewa kwa urahisi, yaani, mtu anayejitazama kwenye kioo. Alikuwa akifundisha somo gani? Ni upumbavu ikiwa mtu angejitazama kwenye kioo, kisha aone kasoro, naye asijirekebishe. Vivyo hivyo, ni upumbavu ikiwa tutasoma Neno la Mungu, tuone jambo fulani tunalohitaji kufanyia marekebisho katika utu wetu, kisha tukose kuchukua hatua.

18. Nĩ mantũ jarĩkũ jathatũ tũbwĩrĩte kũthithia rĩrĩa tũgũtumĩra ngerekano?

18 Unapotumia mifano, unaweza kumwiga Yakobo kwa kufanya mambo matatu: (1) Hakikisha kwamba mfano unaotumia unafaa jambo unalozungumzia. (2) Tumia mfano ambao wasikilizaji wako watauelewa kwa urahisi. (3) Onyesha waziwazi jinsi ya kutumia masomo yaliyo katika mfano huo. Ikiwa ni vigumu kwako kupata mifano inayofaa, tafuta kwenye Fahirisi. Chini ya kichwa “Mifano,” utapata mifano mingi ambayo unaweza kuitumia. Hata hivyo, kumbuka kwamba mifano ni kama kipaza sauti​—inaweka wazi jambo unalofundisha. Basi hakikisha kwamba unatumia mfano ili kufundisha tu mambo makuu. Bila shaka, lengo kuu la kuboresha ustadi wetu wa kufundisha si kujiletea sifa, bali kuwasaidia watu wengi iwezekanavyo wajiunge na familia ya Yehova yenye furaha.

19. Nĩatĩa tũũmba kwonania nĩtwendete ataana na aarĩ-ba-baaba beetũ?

19 Tofauti na Yakobo, sisi hatukuwa na pendeleo la kulelewa pamoja na ndugu mkubwa mkamilifu, lakini tuna pendeleo la kumtumikia Yehova katika familia kubwa ya akina ndugu na dada Wakristo. Tunawaonyesha upendo kwa kushirikiana pamoja nao, kujifunza kutoka kwao, na kutumikia kwa ushikamanifu bega kwa bega pamoja nao katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Tukijitahidi kuiga mtazamo, mwenendo, na njia ya kufundisha ya Yakobo, tutamletea utukufu Yehova na kuwasaidia watu wenye mioyo minyoofu wamkaribie Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.

RWĨMBO 114 “Iweni na Subira”

^ Yakobo alilelewa katika familia ileile pamoja na Yesu. Wakati huo, Yakobo alimjua vizuri zaidi Mwana wa Mungu kuliko watu wengi walivyomjua. Katika makala hii, tutachunguza mambo tunayoweza kujifunza kutokana na maisha na mafundisho ya ndugu mdogo wa Yesu ambaye alikuja kuwa nguzo katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza.

^ Katika makala hii, tutamwita Yakobo kuwa ndugu ya Yesu. Kihalisi alikuwa ndugu nusu wa Yesu na inaonekana yeye ndiye aliyeandika barua inayoitwa kwa jina lake.

^ Nathan H. Knorr alikuwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza. Alimaliza mwendo wake duniani mwaka wa 1977.

^ MAELEZO YA PICHA: Yakobo alitumia mfano wa moto mdogo​—jambo ambalo watu wangeweza kuelewa kwa urahisi—​ili kuonyesha hatari ya kutumia vibaya ulimi wetu.