Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 28

Ĩta na Mbere Kũgunĩka Kuumania na Gũkĩra Mũrungu

Ĩta na Mbere Kũgunĩka Kuumania na Gũkĩra Mũrungu

“Uria witaga na miitire imiega nakiraga Mwathani.”​—NJU. 14:2.

RWĨMBO 122 Iweni Imara, Thabiti!

MUHTASARI a

1-2. O ta Loti nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ Akristũ bagũcemania najo ntukũne cietũ?

 KUHUSU viwango vya maadili vilivyo katika ulimwengu huu, tunahisi kama Loti mwadilifu. ‘Alitaabishwa sana na mwenendo mpotovu wa waasi sheria,’ kwa sababu alijua kwamba Baba yetu wa mbinguni anachukia mwenendo mbaya. (2 Pet. 2:7, 8) Kumwogopa na kumpenda Mungu kulimchochea Loti akatae mwenendo mpotovu wa watu waliomzunguka. Sisi pia tumezungukwa na watu ambao wanapuuza viwango vya maadili vya Yehova. Ingawa hivyo, tunaweza kuendelea kuwa safi kiadili ikiwa tutaendelea kumpenda Mungu na kusitawisha woga unaofaa kumwelekea.​—Met. 14:2.

2 Ili kutusaidia, Yehova anatutia moyo kwa upendo na kutuchochea kupitia kitabu cha Methali. Wakristo wote wanaume na wanawake, vijana na wazee, wanaweza kunufaika sana kwa kuchunguza ushauri wenye hekima ulio katika kitabu hicho.

GŨKĨRA MŨRUNGU NĨGŨTŨKARAGIA

Tunapokuwa kazini, tunapaswa kuepuka marafiki wasiofaa na kuepuka kufanya mambo ambayo hayamfurahishi Yehova (Tazama fungu la 3)

3. Kũringana na Njuno 17:3, nĩ gĩtũmi kĩrĩkũ gĩtũmaga tũkaria nkoro cietũ? (Tega kinya mbica.)

3 Sababu muhimu inayotufanya tuulinde moyo wetu wa mfano ni kwamba Yehova huchunguza moyo wetu. Hilo linamaanisha kwamba haangalii tu jinsi tunavyoonekana kwa wengine, badala yake anachunguza utu wetu wa ndani. (Soma Methali 17:3.) Atatupenda ikiwa tutajaza katika akili zetu hekima yake ambayo inatusaidia kuishi milele. (Yoh. 4:14) Tukifanya hivyo, hatutapatwa na madhara yanayosababishwa na upotovu wa maadili na uwongo unaotoka kwa Shetani na ulimwengu wake. (1 Yoh. 5:18, 19) Kadiri tunavyozidi kumkaribia Yehova, ndivyo tutakavyozidi kumpenda na kumheshimu hata zaidi. Kwa kuwa hatutaki kumhuzunisha Baba yetu, tutaepuka hata kuwazia kutenda dhambi. Tunaposhawishiwa kutenda mabaya, tutajiuliza, ‘Ninawezaje kumuumiza kimakusudi Mtu ambaye amenionyesha upendo mwingi sana?’​—1 Yoh. 4:9, 10.

4. Nĩatĩa gũkĩra Jehova gwatetherie mwarĩ wa baaba ũmwe atĩgatonye magerione?

4 Marta, dada anayeishi nchini Kroatia, ambaye alishawishiwa kujihusisha na ukosefu wa maadili, aliandika hivi: “Ilikuwa vigumu kwangu kufikiria kwa njia nzuri na kushinda tamaa ya kufurahia dhambi kwa muda mfupi. Lakini kumwogopa Mungu kulinilinda.” b Kumwogopa Mungu kulimlindaje? Marta anasema kwamba alitafakari kuhusu matokeo ambayo uamuzi wake mbaya ungemletea. Sisi pia tunaweza kufanya hivyo. Matokeo mabaya zaidi ni kwamba tutamhuzunisha Yehova na kukosa fursa ya kumwabudu milele.​—Mwa. 6:5, 6.

5. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya Leo?

5 Ikiwa tunamwogopa Yehova, tutakuwa waangalifu na kuepuka kushirikiana na watu wanaotenda mabaya. Ndugu Leo, anayeishi nchini Kongo, alijifunza jambo hilo. Miaka minne baada ya kubatizwa, alianza kushirikiana na marafiki wabaya. Alifikiri kwamba maadamu yeye mwenyewe hakufanya matendo mabaya, basi hakuwa akimtendea Yehova dhambi. Ingawa hivyo, baada ya muda mfupi, marafiki hao wabaya walimshawishi, akaanza kunywa pombe kupita kiasi na kujihusisha na ukosefu wa maadili. Kisha akaanza kukumbuka mambo ambayo wazazi wake Wakristo walimfundisha na jinsi alivyopoteza furaha yake. Matokeo yalikuwaje? Alirudiwa na fahamu. Kwa msaada wa wazee wa kutaniko, alimrudia Yehova. Sasa anatumikia kwa furaha akiwa mzee wa kutaniko na painia wa pekee.

6. Nĩ ekũrũ barĩkũ baĩrĩ ba ngerekano tũkarĩĩria?

6 Acheni tuchunguze Methali sura ya 9, ambayo inalinganisha hekima na upumbavu, na wanawake wawili wa mfano. (Linganisha Waroma 5:14; Wagalatia 4:24.) Tunapofanya hivyo, kumbuka kwamba ulimwengu wa Shetani unakazia sana uasherati na ponografia. (Efe. 4:19) Basi, ni jambo muhimu tuendelee kusitawisha woga kumwelekea Mungu na kujiepusha na uovu. (Met. 16:6) Hivyo, sisi sote iwe ni wanaume au wanawake tunaweza kunufaika kutokana na sura hiyo. Kila mmoja wa wanawake hao wawili anatoa mwaliko kwa wajinga, yaani, wale “wasio na busara.” Ni kana kwamba kila mwanamke anasema hivi, ‘Karibu nyumbani kwangu tule chakula.’ (Met. 9:1, 5, 6, 13, 16, 17) Lakini kila mwaliko una matokeo yaliyo tofauti sana.

ŨGETĨKĨĨRIA GWĨTWA NĨ MWEKŨRŨ ŨMŨRIITU

“Mwanamke mpumbavu” anatoa mwaliko unaoweza kusababisha matokeo mabaya (Tazama fungu la 7)

7. Kũringana na Njuno 9:13-18, gwĩtĩkĩĩria gwĩtwa nĩ mwekũrũ ũmũriitu kũũmba kwĩthĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ? (Tega kinya mbica.)

7 Fikiria mwaliko unaotoka kwa “mwanamke mpumbavu.” (Soma Methali 9:13-18.) Kwa ujasiri na kwa sauti kubwa anawaambia hivi wale wasio na busara, ‘Njooni hapa’ mle chakula. Wanapatwa na matokeo gani? “Wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo.” Huenda ukakumbuka lugha kama hiyo ya mfano inayotumiwa mwanzoni mwa kitabu cha Methali. Tunaonywa kuhusu “mwanamke aliyepotoka” na “mwanamke mwasherati.” Tunaambiwa hivi: “Nyumba yake huzama katika kifo.” (Met. 2:11-19) Methali 5:3-10 inatoa onyo kuhusu ‘mwanamke mwingine aliyepotoka’ ambaye “miguu yake hushuka kwenye kifo.”

8. Tũbuĩrĩte gũtua ĩtua rĩrĩkũ?

8 Wale wanaosikia sauti ya “mwanamke mpumbavu” wanahitaji kufanya uamuzi huu: Je, watakubali mwaliko wake au wataukataa? Huenda sisi pia tukahitaji kufanya uamuzi kama huo. Tutafanya nini ikiwa tutashawishiwa kufanya uasherati au kutazama picha au video za ponografia kwenye Intaneti?

9-10. Nĩ itũmi birĩkũ bimwe bitũmaga tũciebania na ũthũngĩri?

9 Tuna sababu nzuri sana zinazotuchochea tuepuke uasherati. “Mwanamke mpumbavu” anafafanuliwa kuwa anasema hivi: “Maji yaliyoibwa ni matamu.” “Maji yaliyoibwa” ni nini? Biblia inalinganisha uhusiano wa kingono ambao watu waliofunga ndoa hufurahia na maji yenye kuburudisha. (Met. 5:15-18) Mume na mke waliofunga ndoa kisheria wanaweza kufurahia kufanya ngono. Hata hivyo, mambo ni tofauti kuhusu “maji yaliyoibwa.” Maji hayo yanarejelea uasherati. Watu hufanya uasherati kisiri kama mwizi anavyoiba kisiri. ‘Maji hayo yaliyoibwa’ huenda yakaonekana kuwa matamu hasa ikiwa wale wanaohusika wanafikiri kwamba hakuna mtu atakayejua jambo hilo. Kwa kweli wanajidanganya! Yehova anaona mambo yote. Ikiwa tutapoteza kibali cha Yehova, tutapatwa na uchungu mwingi sana na kwa kweli hilo si jambo ‘tamu’ au linalofurahisha. (1 Kor. 6:9, 10) Lakini kuna mengi zaidi.

10 Uasherati unaweza kusababisha aibu, kujihisi kwamba hufai, mimba zisizotakikana, na kuvunjika kwa familia. Ni wazi kwamba ni jambo la hekima kuepuka “nyumba” ya mwanamke mpumbavu na chakula chake. Mbali na kupoteza kibali cha Yehova, wengi wanaofanya uasherati hupatwa na magonjwa ambayo yanasababisha kifo cha mapema. (Met. 7:23, 26) Methali 9:18 inamalizia kwa kusema hivi: “Wageni wake wamo katika vina vya kaburi.” Basi, kwa nini watu wengi hukubali mwaliko wa mwanamke huyo unaoongoza kwenye msiba?​—Met. 9:13-18.

11. Nĩkĩ nĩũntũ bũthũũku mono gũtega ponografia?

11 Mtego mmoja wa kawaida ni ponografia. Baadhi ya watu wanafikiri kwamba kutazama ponografia hakuna madhara yoyote. Kinyume chake, ponografia husababisha madhara, hufanya watu wakose kujiheshimu, na kuwa waraibu wa ponografia. Mtu anapotazama ponografia ni vigumu sana kuondoa picha hizo akilini. Isitoshe, ponografia haiwezi kutusaidia kushinda tamaa zisizofaa; badala yake, inachochea tamaa hizo. (Kol. 3:5; Yak. 1:14, 15) Naam, baada ya kutazama ponografia, watu wengi hujihusisha na mwenendo mpotovu.

12. Nĩatĩa tũũmba kũthithia nĩkenda tũciebania na gũtega mbica irĩa ciũmba gũtũma twĩthĩrwa na wirĩrĩria bwa kũmenyana kĩmwĩrĩ?

12 Tukiwa Wakristo, tunapaswa kufanya nini ikiwa picha ya ponografia itatokea bila kutarajia kwenye kifaa chetu cha kielektroni? Tunapaswa kuacha mara moja kutazama picha hiyo. Itakuwa rahisi kufanya hivyo ikiwa tutakumbuka kwamba uhusiano wetu pamoja na Yehova ndilo jambo lenye thamani zaidi kwetu. Hata baadhi ya picha ambazo hazionwi kuwa za ponografia zinaweza kuchochea hamu ya ngono. Kwa nini tunapaswa kuziepuka? Kwa sababu hatungependa hata kuwazia kufanya uasherati katika moyo wetu. (Mt. 5:28, 29) David, mzee wa kutaniko anayeishi nchini Thailand, anasema hivi: “Mimi hujiuliza: ‘Ingawa picha hizo si ponografia, je, nitamfurahisha Yehova ikiwa nitaendelea kuzitazama?’ Kufikiria kwa njia hiyo hunisaidia kutenda kwa hekima.”

13. Nĩmbi biũmba gũtũtethia kũthithia na njĩra ya ũũme?

13 Tutatenda kwa hekima ikiwa tutasitawisha woga unaofaa kwa kuepuka kufanya jambo linalomchukiza Yehova. Kumwogopa Mungu ndio “mwanzo,” au msingi, “wa hekima.” (Met. 9:10) Tunaona jambo hilo mwanzoni mwa Methali sura ya 9, ambapo tunasoma kuhusu mwanamke mwingine wa mfano, anayeitwa “hekima ya kweli.”

ĨTĨKĨĨRIA ŨRITANI BWA ‘ŨŨME BWA MMA’

14. Nĩmbi ĩngĩ ĩgwĩtana na njĩra ya ngerekano kũringana na Njuno 9:1-6?

14 Soma Methali 9:1-6. Hapa tunasoma kuhusu mwaliko unaotoka katika Chanzo na Msingi wa hekima ya kweli, yaani, Muumba wetu mwenye hekima yote. (Met. 2:6; Rom. 16:27) Hapa tunasoma kuhusu nyumba kubwa iliyo na nguzo saba. Hilo linaonyesha kwamba Yehova ni mkarimu na anawakaribisha wote wanaotaka kujifunza jinsi ya kutumia hekima yake maishani.

15. Nĩatĩa Mũrungu endaga tũthithia?

15 Yehova ni mkarimu, naye hutuandalia vitu kwa wingi. Sifa hizo zinaonekana katika “hekima ya kweli,” ambayo kwenye Methali sura ya 9 inalinganishwa na mwanamke. Simulizi hilo linasema kwamba mwanamke huyo wa mfano ametayarisha kabisa nyama yake, amechanganya divai yake, na kupanga meza yake katika nyumba yake. (Met. 9:2, maelezo ya chini) Isitoshe, kulingana na mstari wa 4 na 5, mwanamke huyo anayefananishwa na hekima ya kweli, “humwambia yule asiye na busara: ‘Njoo, ule mkate wangu.’” Kwa nini tunapaswa kukubali mwaliko wa kwenda kwenye nyumba ya hekima ya kweli na kula chakula cha mwanamke huyo? Yehova angependa watoto wake wawe wenye hekima na wawe salama. Hataki tujifunze masomo maishani kwa njia ngumu, yaani, kupitia kufanya makosa ambayo yatatusababishia majuto. Ndiyo sababu yeye “huwahifadhia wanyoofu hekima inayotumika.” (Met. 2:7) Tukisitawisha woga unaofaa kumwelekea Yehova, tutatamani kumfurahisha. Tunasikiliza ushauri wake wenye hekima, na tunafurahi kuufuata.​—Yak. 1:25.

16. Gũkĩra Mũrungu gwatetherie Alain atĩa gũtua ĩtua na njĩra ya ũũme, na maumĩĩra jarĩ jarĩkũ?

16 Fikiria jinsi kumwogopa Mungu kulivyomsaidia Alain kufanya uamuzi wenye hekima. Mzee huyo wa kutaniko ambaye pia ni mwalimu wa shule anasema hivi: “Wengi kati ya wafanyakazi wenzangu walifikiri kwamba video za ponografia ni moja kati ya masomo kuhusu ngono.” Lakini Alain hakudanganyika. Anasema hivi: “Kwa kuwa ninamwogopa Mungu, nilikataa kabisa kutazama sinema hizo. Pia, niliwaeleza wafanyakazi wenzangu sababu iliyonifanya nikatae.” Alikuwa akifuata ushauri kutoka kwa “hekima ya kweli” wa ‘kutembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.’ (Met. 9:6) Msimamo thabiti wa Alain uliwafurahisha baadhi ya walimu wenzake na sasa wanajifunza Biblia na kuhudhuria mikutano ya Kikristo.

Kukubali mwaliko wa “hekima ya kweli” kutatusaidia kuishi milele (Tazama fungu la 17 na 18)

17-18. Barĩa betĩkagĩĩria ũũme bwa mma bagwĩragĩrua itharimo birĩkũ na nĩ birĩkũ bingĩ beterete ĩgiita rĩĩjĩte? (Tega kinya mbica.)

17 Yehova anatumia mifano ya wanawake hao wawili, ili kutuonyesha jinsi tunavyoweza kuwa na wakati ujao wenye furaha. Wale wanaokubali mwaliko unaotolewa kwa sauti kubwa na “mwanamke mpumbavu,” wanakazia fikira kujifurahisha kupitia ukosefu wa maadili kisiri. Lakini hawatambui kwamba mambo wanayofanya yataathiri wakati wao ujao. Matendo yao yatawaongoza katika “vina vya Kaburi.”​—Met. 9:13, 17, 18.

18 Matokeo ni tofauti kabisa kwa wale wanaokubali mwaliko wa “hekima ya kweli”! Leo, wageni wa mwanamke huyo wanafurahia karamu iliyopangwa vizuri na inayojenga afya, mlo wa vyakula vya kiroho vilivyoandaliwa kwa njia nzuri. (Isa. 65:13) Yehova alisema hivi kupitia nabii Isaya: “Nisikilizeni kwa makini, mle kilicho chema, nanyi mtafurahia sana vitu vyenye lishe kwelikweli.” (Isa. 55:1, 2) Tunajifunza kupenda mambo ambayo Yehova anapenda na kuchukia mambo ambayo anachukia. (Zab. 97:10) Na tunafurahi kuwaalika wengine ili waje na kunufaika kutokana na “hekima ya kweli.” Ni kana kwamba tunaita “kwa sauti [hivi] kutoka vileleni juu ya jiji: ‘Yeyote ambaye ni mjinga na aje humu.’” Sisi na wale wanaokubali mwaliko huo hatunufaiki tu sasa. Tutaendelea kunufaika na kuishi milele ‘tunapotembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.’​—Met. 9:3, 4, 6.

19. O ta ũrĩa Mutumiiria 12:13, 14, yonanĩtĩe, tũbuĩrĩte gũtua ĩtua rĩrĩkũ? (Tega kinya kathandũkũ “ Gũkĩra Mũrungu Nĩgũtũgunaga.”)

19 Soma Mhubiri 12:13, 14. Acheni kumwogopa Mungu kuendelee kulinda mioyo yetu na kutusaidie kudumisha hali nzuri ya kimaadili na kiroho katika siku hizi za mwisho zenye uovu. Woga huo unaofaa utatusaidia kuendelea kuwaalika watu wengi iwezekanavyo watafute “hekima ya kweli” na wanufaike nayo.

RWĨMBO 127 Napaswa Kuwa Mtu wa Namna Gani?

a Wakristo wanahitaji kusitawisha woga unaofaa kumwelekea Mungu. Woga kama huo unaweza kulinda mioyo yetu na kutusaidia kuepuka uasherati na ponografia. Katika makala hii, tutazungumzia Methali sura ya 9, ambayo inaonyesha tofauti kati ya hekima na upumbavu kwa kutumia wanawake wawili wa mfano. Sura hii inaweza kutunufaisha sasa na wakati ujao.

b Baadhi ya majina yamebadilishwa.