Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 27

Tũbuĩrĩte Gũkĩra Jehova Nĩkĩ?

Tũbuĩrĩte Gũkĩra Jehova Nĩkĩ?

“Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa.”​—ZAB. 25:14.

RWĨMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Letu

MUHTASARI a

1-2. Kũringana na Zaburi 25:14, no mwanka tũthithie atĩa nĩkenda twĩthĩrwa na ũcoore bwa akuĩ na Jehova?

 UNAFIKIRI ni sifa gani zinazohitajika ikiwa unataka kudumisha urafiki wa karibu na mtu fulani? Huenda ukajibu kwamba marafiki wazuri wanapaswa kupendana na kusaidiana. Huenda hutafikiria kwamba woga ni sifa muhimu ili kuwa na urafiki mzuri. Hata hivyo, kama andiko la msingi la makala hii linavyosema, wale wanaotaka kusitawisha urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni lazima ‘wamwogope.’​—Soma Zaburi 25:14.

2 Hata iwe tumemtumikia Yehova kwa muda mrefu kadiri gani, sisi sote tunahitaji kusitawisha woga unaofaa kumwelekea. Lakini kumwogopa Mungu kunamaanisha nini? Tunawezaje kujifunza kumwogopa Yehova? Na tunaweza kujifunza nini kuhusu kumwogopa Mungu kutoka kwa msimamizi Obadia, Kuhani Mkuu Yehoyada, na Mfalme Yehoashi?

GŨKĨRA MŨRUNGU NĨ KUUGA ATĨA?

3. Tarĩĩria nĩ mantũ ta jarĩkũ jomba gũtũma tũkethĩrwa na ũguaa na ũrĩa ũguaa bũu bũtũkaragia.

3 Huenda tukahisi woga ikiwa tunaamini kwamba tutapatwa na madhara ya aina fulani. Woga wa aina hiyo unafaa na unaweza kutuchochea kutenda kwa hekima. Woga wa kuanguka hutuzuia kutembea karibu na ukingo wa mlima. Woga wa kujeruhiwa unaweza kutufanya tukimbie kutoka kwenye hali hatari. Woga wa kuharibu urafiki pamoja na mtu tunayempenda utatuzuia kusema au kufanya jambo lisilo la fadhili.

4. Shaitani endaga twĩthĩrwa na ũguaa bũrĩkũ kwerekera Jehova?

4 Shetani anataka watu wawe na woga usiofaa kumwelekea Yehova. Shetani anaendeleza maoni yaliyosemwa na Elifazi—kwamba Yehova ni Mungu mwenye kisasi na hasira na haiwezekani kumfurahisha. (Ayu. 4:18, 19) Shetani anataka tumhofu sana Yehova hivi kwamba tuache kumtumikia. Ili kuepuka mtego huo, tunahitaji kusitawisha woga unaofaa kumwelekea Mungu.

5. Gũkĩra Mũrungu nĩ kuuga atĩa?

5 Mtu aliye na woga unaofaa kumwelekea Mungu anampenda na anaepuka kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuharibu uhusiano wake pamoja na Mungu. Yesu ‘alimwogopa Mungu’ kwa njia hiyo. (Ebr. 5:7) Hakumwona Yehova kuwa mwenye kutisha. (Isa. 11:2, 3) Badala yake, alikuwa na upendo mwingi sana kumwelekea na alitaka kumtii. (Yoh. 14:21, 31) Kama Yesu, tunamheshimu na kumstahi sana Yehova kwa sababu Yeye ni mwenye upendo, hekima, haki, na nguvu. Pia, tunajua kwamba Yehova anatupenda sana na anapendezwa kuona jinsi tunavyoitikia mwongozo wake. Yehova anahuzunika tunapokosa kutii, lakini tunapomtii moyo wake unashangilia.​—Zab. 78:41; Met. 27:11.

KWIRITANA GŨKĨRA MŨRUNGU

6. Njĩra ĩmwe ĩrĩa tũũmba kwiritana nayo gũkĩra Mũrungu nĩ ĩrĩkũ? (Zaburi 34:11)

6 Hatuzaliwi tukiwa na woga kumwelekea Yehova; tunapaswa kusitawisha woga huo. (Soma Zaburi 34:11.) Njia moja ya kusitawisha woga huo ni kwa kuchunguza uumbaji. Kadiri tunavyoona hekima, nguvu, na upendo mwingi wa Mungu kutuelekea kupitia “vitu vilivyoumbwa,” ndivyo tunavyomheshimu na kumpenda zaidi. (Rom. 1:20) Dada anayeitwa Adrienne alisema hivi: “Hekima ya Yehova inayoonekana kupitia uumbaji hunishangaza na hunisaidia kutambua kwamba anajua jambo linalonifaa kabisa.” Baada ya kutafakari alifikia mkataa huu, “Kwa nini nifanye jambo lolote ambalo linaweza kuweka kizuizi kati yangu na Yehova, ambaye ni Chanzo cha uhai wangu?” Je, unaweza kutenga muda juma hili ili kufikiria kuhusu jambo fulani katika uumbaji? Kufanya hivyo kutakuchochea kumheshimu na kumpenda zaidi Yehova.​—Zab. 111:2, 3.

7. Nĩatĩa maromba jomba gũtũtethia gũkũria ũgũaa bũrĩa bwagĩrĩte kwerekera Jehova?

7 Njia nyingine ambayo tunaweza kusitawisha woga kumwelekea Mungu ni kwa kusali kwa ukawaida. Kadiri tunavyosali, ndivyo Yehova anavyozidi kuwa halisi kwetu. Kila mara tunapomwomba atuimarishe ili tuvumilie jaribu fulani, tunakumbuka kwamba ana nguvu nyingi sana. Tunapomshukuru kwa ajili ya zawadi ya Mwana wake, tunakumbuka kwamba Yehova anatupenda. Na tunapomsihi Yehova atusaidie kushughulikia tatizo fulani, tunakazia kwenye mioyo yetu kwamba yeye ni mwenye hekima. Sala kama hizo hutusaidia kumheshimu Yehova hata zaidi na zinaimarisha azimio letu la kuepuka kufanya jambo lolote ambalo litaharibu uhusiano wetu pamoja naye.

8. Nĩatĩa tũbuĩrĩte kũthithia nĩkenda twĩta na mbere gũkĩra Mũrungu?

8 Tunaweza kudumisha woga wetu kumwelekea Mungu kwa kujifunza Biblia tukiwa na lengo la kujifunza kutokana na mifano mizuri na mibaya inayotajwa katika Biblia. Acheni tuzungumzie watumishi wawili waaminifu wa Yehova—Obadia, msimamizi wa nyumba ya Mfalme Ahabu na Kuhani Mkuu Yehoyada. Kisha tutaona mambo tunayoweza kujifunza kutokana na Mfalme Yehoashi wa Yuda, ambaye mwanzoni alikuwa mwaminifu lakini baadaye alimwacha Yehova.

ĨTHĨRWA NA ŨCAMBA TA OBADIA

9. Nĩatĩa gũkĩra Jehova gwatetherie Obadia? (1 Anene 18:3, 12)

9 Biblia inamtaja Obadia b kwa mara ya kwanza kwa maneno haya: “Obadia alimwogopa sana Yehova.” (Soma 1 Wafalme 18:3, 12.) Woga huo unaofaa ulimsaidiaje Obadia? Jambo moja ni kwamba ulimsaidia kuwa mnyoofu na mwenye kutegemeka; hivyo, mfalme alimchagua asimamie makao ya mfalme. (Linganisha Nehemia 7:2.) Pia, woga wa Obadia kumwelekea Mungu ulimpatia ujasiri mwingi usio wa kawaida—sifa ambayo aliihitaji sana. Aliishi katika kipindi cha mtawala mwovu Mfalme Ahabu, ambaye “alikuwa mwovu sana machoni pa Yehova kuliko [wafalme] wote waliomtangulia.” (1 Fal. 16:30) Pia, Yezebeli, mke wa Ahabu ambaye alimwabudu Baali, alimchukia sana Yehova hivi kwamba alijaribu kukomesha kabisa ibada safi katika ufalme wa kaskazini. Hata aliwaua manabii wengi wa Mungu. (1 Fal. 18:4) Bila shaka, Obadia alimwabudu Yehova katika kipindi kigumu.

10. Nĩatĩa Obadia oonanĩrie ũcamba bũtĩ bwa wĩthĩre?

10 Obadia alionyeshaje ujasiri usio wa kawaida? Yezebeli alipoanza kuwatafuta manabii wa Mungu ili awaue, Obadia aliwachukua 100 kati yao na kuwaficha ‘manabii 50 katika kila pango, na kuwapa mikate na maji.’ (1 Fal. 18:13, 14) Ikiwa angegunduliwa, kwa hakika Obadia mwenye ujasiri angeuawa. Bila shaka, Obadia alikuwa na hofu na hakutaka kufa, lakini Obadia alimpenda Yehova na wale waliomtumikia kuliko alivyopenda uhai wake mwenyewe.

Licha ya kazi yetu kupigwa marufuku, ndugu anawasambazia machapisho kwa ujasiri Mashahidi wenzake (Tazama fungu la 11) d

11. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ atumĩkĩri ba Jehova ba ĩgiita rĩrĩ bakari ta Obadia? (Tega kinya mbica.)

11 Leo, watumishi wengi wa Yehova wanaishi katika nchi ambazo kazi yetu imepigwa marufuku. Wanawaonyesha heshima wenye mamlaka, lakini kama Obadia, ndugu na dada hao wapendwa wanampa Yehova kile anachostahili kupokea, yaani, ibada ya pekee. (Mt. 22:21) Wanaonyesha wanamwogopa Mungu kwa kumtii yeye badala ya wanadamu. (Mdo. 5:29) Wanafanya hivyo kwa kuendelea kuhubiri habari njema na kukutana pamoja kisiri. (Mt. 10:16, 28) Wanajitahidi kuhakikisha kwamba ndugu na dada zao wanapata chakula cha kiroho wanachohitaji. Fikiria kisa cha Henri, ambaye anaishi katika nchi moja barani Afrika ambako kazi yetu ilipigwa marufuku kwa muda fulani. Wakati wa marufuku, Henri alijitolea kusambaza machapisho kwa Mashahidi wenzake. Aliandika hivi: “Kwa kawaida, mimi ni mwenye haya. Nimesadiki kwamba ni heshima nyingi niliyo nayo kumwelekea Yehova ambayo ilinipa ujasiri niliohitaji.” Je, wewe unaweza kuwa na ujasiri kama wa Henri? Unaweza ikiwa utasitawisha woga unaofaa kumwelekea Mungu.

ĨTHĨRWA ŨRĨ MWĨTĨKĨKUA TA MŨTHĨNJĨRI MŨRUNGU ŨMŨNENE JEHOIADA

12. Mũthĩnjĩri wa Mũrungu Ũmũnene Jehoiada na mwekũrũ waawe boonanĩrie wĩtĩkĩkua bũbũnene atĩa kwerekera Jehova?

12 Kuhani Mkuu Yehoyada alimwogopa Yehova, na woga huo ulimsaidia kuwa mshikamanifu na kuendeleza ibada safi. Jambo hilo lilikuwa wazi wakati Atalia, binti ya Yezebeli, alipochukua mamlaka kwa nguvu na kuanza kutawala Yuda. Watu walikuwa na sababu nzuri ya kumwogopa Atalia. Alikuwa mkatili na mwenye pupa sana ya kupata mamlaka hivi kwamba alijaribu kuwaua warithi wote, yaani, wajukuu wake mwenyewe! (2 Nya. 22:10, 11) Mmoja wa watoto hao—Yehoashi—aliokoka kwa sababu Yehoshabeathi, mke wa Yehoyada, alimwokoa. Yeye na mume wake walimficha mtoto huyo na kumtunza. Kwa njia hiyo, Yehoyada na Yehoshabeathi walilinda ukoo wa wafalme waliotokana na Daudi. Yehoyada alikuwa mshikamanifu kwa Yehova na hakutetemeka kwa woga kwa sababu ya Atalia.​—Met. 29:25.

13. Rĩrĩa Joashi aarĩ na mĩaka mũgwanja, nĩatĩa Jehoiada oonanĩrie wĩtĩkĩkua kaĩrĩ?

13 Yehoashi alipokuwa na umri wa miaka saba, Yehoyada alionyesha ushikamanifu wake tena kwa Yehova. Alifanya mpango fulani. Ikiwa mpango huo ungefaulu, Yehoashi angekuwa mfalme, mrithi wa Daudi aliyestahili. Hata hivyo, ikiwa mpango huo ungekosa kufaulu, Yehoyada angeuawa. Yehova alibariki mpango huo, nao ukafaulu. Yehoyada akiungwa mkono na wakuu na Walawi, walimfanya Yehoashi awe mfalme na kumuua Atalia. (2 Nya. 23:1-5, 11, 12, 15; 24:1) Yehoyada “akafanya agano kati ya Yehova na mfalme na watu, kwamba wataendelea kuwa watu wa Yehova.” (2 Fal. 11:17) Yehoyada aliwaweka “pia walinzi wa malango karibu na malango ya nyumba ya Yehova, ili mtu yeyote asiye safi kwa njia yoyote ile asiingie.”​—2 Nya. 23:19.

14. Nĩ itharimo birĩkũ Jehoiada oonere tontũ bwa gũtĩĩa Jehova?

14 Hapo awali Yehova alikuwa amesema hivi: “Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu.” Kwa kweli, Yehova alimthawabisha Yehoyada. (1 Sam. 2:30) Kwa mfano, alihakikisha kwamba matendo mazuri ya kuhani huyo mkuu yaliandikwa ili kutufundisha. (Rom. 15:4) Na Yehoyada alipokufa, alipewa heshima ya pekee kwa kuzikwa “katika Jiji la Daudi pamoja na wafalme, kwa sababu alikuwa ametenda mema katika Israeli kwa ajili ya Mungu wa kweli na nyumba Yake.”​—2 Nya. 24:15, 16.

Kama Kuhani Mkuu Yehoyada, kumwogopa Mungu kunatuchochea kuwasaidia ndugu zetu kwa ushikamanifu (Tazama fungu la 15) e

15. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na rũgono rwa Jehoiada? (Tega kinya mbica.)

15 Simulizi kuhusu Yehoyada linaweza kutusaidia sisi sote kusitawisha woga kumwelekea Mungu. Wazee Wakristo wanaweza kumwiga Yehoyada kwa kuendelea kuwa chonjo na kulilinda kwa ushikamanifu kundi la Mungu. (Mdo. 20:28) Wale walio na umri mkubwa wanaweza kujifunza kutokana na Yehoyada kwamba ikiwa watamwogopa Yehova na kuendelea kuwa washikamanifu kwake, anaweza kuwatumia ili kutimiza kusudi Lake. Hawapuuzi. Vijana wanaweza kujifunza jinsi Yehova alivyomtendea Yehoyada na wanaweza kumwiga Yehova kwa kuwastahi na kuwaheshimu watumishi washikamanifu wenye umri mkubwa, hasa wale ambao wametumikia kwa uaminifu kwa muda mrefu. (Met. 16:31) Mwishowe, sisi sote tunaweza kujifunza kutokana na wakuu na Walawi ambao walimuunga mkono Yehoyada. Acheni tuwaunge mkono kwa ushikamanifu “wale wanaoongoza” kwa kuwatii.​—Ebr. 13:17.

ŨGAKARA TA MŨNENE JOASHI

16. Nĩmbi bikwonania Mũnene Joashi atathingatagĩra mantũ jarĩa aairitanĩte?

16 Mfalme Yehoashi alinufaika sana kwa kushirikiana na Yehoyada. (2 Fal. 12:2) Matokeo ni kwamba mfalme huyo kijana alitamani kumfurahisha Yehova. Lakini baada ya Yehoyada kufa, Yehoashi aliwasikiliza wakuu walioasi imani. Matokeo yalikuwaje? Yeye na raia wake “[walianza] kuabudu miti mitakatifu na sanamu.” (2 Nya. 24:4, 17, 18) Ingawa Yehova alihuzunika sana, “aliendelea kuwatuma manabii miongoni mwao ili wawarudishe . . . , lakini walikataa kusikiliza.” Hata hawakumsikiliza Zekaria, c mwana wa Yehoyada ambaye alikuwa nabii na kuhani wa Yehova na pia binamu ya Yehoashi. Isitoshe, bila shukrani kwa familia ambayo ilikuwa imemsaidia sana, Mfalme Yehoashi alimuua Zekaria.​—2 Nya. 22:11; 24:19-22.

17. Nĩatĩa gwakarĩkĩre kĩrĩ Joashi?

17 Yehoashi hakudumisha woga unaofaa kumwelekea Yehova, na matokeo yalikuwa mabaya. Yehova alikuwa amesema hivi: “Wale wanaonidharau watadharauliwa.” (1 Sam. 2:30) Baadaye, jeshi dogo la Wasiria lilishinda “jeshi kubwa sana” la Yehoashi na ‘kumjeruhi vibaya.’ Baada ya Wasiria kuondoka, Yehoashi aliuawa na watumishi wake mwenyewe kwa sababu ya kumuua Zekaria. Watu walimwona mfalme huyo kuwa mwovu sana hivi kwamba hakustahili kuzikwa “katika makaburi ya wafalme.”​—2 Nya. 24:23-25.

18. Kũringana na Jeremia 17:7, 8, nĩatĩa tũũmba kũrega kwigerekania na Joashi?

18 Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Yehoashi? Alikuwa kama mti wenye mizizi mifupi ambao ulitegemezwa na nguzo, nguzo hiyo ilipoondolewa, yaani, Yehoyada alipokufa, upepo wa uasi-imani ulivuma na kumwangusha Yehoashi. Hilo ni somo lenye nguvu kwamba hatupaswi kumwogopa Mungu kwa sababu tu ya kuchochewa na Wakristo wenzetu, kutia ndani watu wa familia yetu. Ili tuendelee kuwa wenye nguvu kiroho, ni lazima tuimarishe ujitoaji wetu kimungu na woga wetu kumwelekea Mungu kwa kujifunza kwa ukawaida, kutafakari, na kusali.​—Soma Yeremia 17:7, 8; Kol. 2:6, 7.

19. Nĩ ũntũ bũrĩkũ Jehova erĩgagĩĩra kuuma kĩrĩ batuĩ?

19 Yehova hadai mengi kutoka kwetu. Jambo ambalo anataka tufanye linatajwa kwenye andiko la Mhubiri 12:13, linalosema: “Mwogope Mungu wa kweli na ushike amri zake, kwa maana huu ndio wajibu wote wa mwanadamu.” Ikiwa tutamwogopa Mungu, tutafaulu kukabiliana na majaribu ya wakati ujao na kusimama imara kama Obadia na Yehoyada. Hakuna kitu chochote kitakachoharibu urafiki wetu pamoja na Yehova.

RWĨMBO 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

a Kama linavyotumiwa katika Maandiko, neno “kuogopa” lina maana zaidi ya moja. Ikitegemea muktadha, linaweza kumaanisha heshima, jambo lenye kutisha, au kustaajabisha. Makala hii itatusaidia kusitawisha woga ambao utatuchochea kuwa jasiri na kumtumikia Baba yetu wa mbinguni kwa ushikamanifu.

b Obadia anayetajwa hapa, si nabii Obadia ambaye aliishi karne nyingi baadaye na aliyeandika kitabu cha Biblia kinachoitwa kwa jina lake.

c Andiko la Mathayo 23:35 linasema kwamba ‘Zekaria alikuwa mwana wa Barakia.’ Maoni yametolewa kwamba huenda Yehoyada alikuwa na majina mawili, kama ilivyo kwenye visa vingine katika Biblia (linganisha Mathayo 9:9 na Marko 2:14), au kwamba Barakia alikuwa babu ya Zekaria au mtu wa ukoo aliyeishi muda mrefu kabla yake.

d MAELEZO YA PICHA: Katika igizo hili, ndugu anasambaza machapisho wakati wa marufuku.

e MAELEZO YA PICHA: Dada mwenye umri mdogo anajifunza kutoka kwa dada mwenye umri mkubwa jinsi ya kuhubiri kupitia simu; ndugu mwenye umri mkubwa anaweka mfano wa ujasiri anapohubiri hadharani; ndugu mwenye uzoefu anawazoeza wengine kazi ya udumishaji katika Jumba la Ufalme.