Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 10

Bũrĩ ta Kĩũthũrano, Tetheerieni Aritwa ba Bibiria Gũkinyĩra Ũbatithio

Bũrĩ ta Kĩũthũrano, Tetheerieni Aritwa ba Bibiria Gũkinyĩra Ũbatithio

“O kirungo kimwe na ngugi yakio . . . Uu niu mwiri jukuraga.”—AEF. 4:16.

RWĨMBO 85 Karibishaneni

MUHTASARI *

1-2. Nũũ ũũmba gũtetheeria aritwa ba Bibiria gũkinyĩra ũbatithio?

AMY, dada kutoka Fiji, anasema hivi: “Nilipenda mambo niliyokuwa nikijifunza katika funzo langu la Biblia. Nilijua kwamba hiyo ilikuwa kweli. Lakini hadi nilipoanza kushirikiana na ndugu na dada, ndipo nilipofanya mabadiliko yaliyohitajika na kufikia hatua ya ubatizo.” Kisa cha Amy kinakazia ukweli huu muhimu: Mwanafunzi wa Biblia ana uwezekano mkubwa zaidi wa kufanya maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo, anapopata msaada kutoka kwa wengine kutanikoni.

2 Kila mhubiri anaweza kuchangia ukuzi wa kutaniko. (Efe. 4:16) Leilani, painia anayeishi Vanuatu, anasema hivi: “Imesemwa kwamba kijiji chote kinahitajika ili kumlea mtoto vizuri. Ninafikiri hilo ni kweli pia inapohusu kazi ya kufanya wanafunzi; kwa kawaida kutaniko lote linahitajika ili kumsaidia mtu ajiunge na ibada ya kweli.” Watu wa familia, marafiki, na walimu wa shule, wote kwa pamoja wanatimiza jukumu fulani katika kumsaidia mtoto afikie ukomavu. Wanafanya hivyo kwa kumtia moyo na kumfundisha mambo muhimu. Vivyo hivyo, wahubiri wanaweza kuwapa ushauri, kuwatia moyo, na kuwawekea mfano mzuri wanafunzi wa Biblia, ili kuwasaidia wafanye maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo.—Met. 15:22.

3. Nĩmbi tũũmba kwiritana kuumania na biugo bia Ana, Dorin, na Leilani?

3 Kwa nini mhubiri anayeongoza funzo la Biblia anapaswa kukubali msaada ambao wahubiri wengine wanaweza kumpa mwanafunzi wake wa Biblia? Ona jinsi Ana, painia wa pekee kutoka Moldova anavyosema: “Ni vigumu sana kwa mtu mmoja kutosheleza mahitaji yote ya mwanafunzi wa Biblia anayeanza kufanya maendeleo.” Dorin, ndugu anayetumikia akiwa painia wa pekee katika nchi hiyohiyo, anaeleza hivi: “Mara nyingi, wahubiri wengine wanasema jambo ambalo linagusa moyo wa mwanafunzi, jambo ambalo mimi nisingefikiria kusema.” Leilani anataja sababu nyingine: “Upendo na uchangamfu ambao mwanafunzi anaonyeshwa, unaweza kumsaidia kuwatambua watu wa Yehova.”—Yoh. 13:35.

4. Nĩmbi tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

4 Hata hivyo, huenda ukajiuliza, ‘Ninaweza kumsaidiaje mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ilhali si mimi ninayeongoza funzo lake la Biblia?’ Acheni tuchunguze mambo tunayoweza kufanya tunapoalikwa kushiriki kwenye funzo la Biblia, na mambo tunayoweza kufanya mwanafunzi wa Biblia anapoanza kuhudhuria mikutano. Pia, tutaona jinsi wazee wa kutaniko wanavyoweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo.

RĨRĨA WAGWATWA ŨGENI KĨRĨ WIRITANI BWA BIBIRIA

Unapoalikwa kushiriki kwenye funzo la Biblia, tayarisha mapema habari itakayozungumziwa (Tazama fungu la 5 hadi 7)

5. Wĩna kaanya karĩkũ rĩrĩa wagwatwa ũgeni kĩrĩ wiritani bwa Bibiria?

5 Wakati wa funzo la Biblia, mwalimu ndiye aliye na wajibu wa msingi wa kumsaidia mwanafunzi kulielewa Neno la Mungu. Ikiwa mwalimu anakualika uandamane naye kwenye funzo la Biblia, uko hapo ili kumsaidia. Jukumu lako ni kumuunga mkono. (Mhu. 4:9, 10) Unaweza kufanya mambo gani hususa yatakayosaidia kufanya pindi hizo za kujifunza Biblia ziwe na matokeo mazuri?

6. Rĩrĩa wagwatwa ũgeni kĩrĩ wiritani bwa Bibiria, nĩatĩa ũũmba gũtumĩra ũritani bũrĩa bũrĩ kĩrĩ Njuno 20:18?

6 Jitayarishe mapema kwa ajili ya funzo la Biblia. Kwanza, mwombe mwalimu akwambie mambo machache kumhusu mwanafunzi. (Soma Methali 20:18.) Unaweza kuuliza hivi: “Unajua mambo gani kumhusu mwanafunzi wako? Mtakuwa mkijifunza habari gani? Ungependa kukazia mambo gani hususa katika somo hilo? Je, kuna jambo lolote ambalo ninapaswa au sipaswi kusema au kufanya wakati wa funzo? Ni jambo gani ambalo huenda likamtia moyo mwanafunzi afanye maendeleo?” Bila shaka, mwalimu hatafunua habari za siri za mwanafunzi, lakini habari zozote atakazokwambia zinaweza kusaidia. Dada mmishonari anayeitwa Joy huwa na mazungumzo kama hayo na wale anaoshirikiana nao kwenye funzo la Biblia. Anasema hivi: “Mazungumzo hayo humsaidia mwandamani wangu kupendezwa na mwanafunzi wa Biblia na kujua jinsi anavyoweza kuchangia wakati wa funzo.”

7. Rĩrĩa wagwatwa ũgeni kĩrĩ wiritani bwa Bibiria nĩkĩ ũkũbatara kwithuranĩra?

7 Ikiwa utaalikwa kushiriki kwenye funzo la Biblia, itafaa ikiwa utatayarisha mapema habari mtakayozungumzia. (Ezra 7:10) Dorin, ndugu aliyetajwa awali, anasema hivi: “Ninafurahi mwandamani wangu anapojitayarisha mapema kwa ajili ya funzo. Kwa kufanya hivyo, anaweza kutoa maelezo yenye kujenga.” Zaidi ya hayo, inaelekea mwanafunzi wa Biblia atatambua kwamba nyinyi nyote mmejitayarisha vizuri, na jambo hilo litamwekea mfano mzuri. Hata ikiwa hutaweza kupitia habari hiyo kwa kina, jitahidi angalau kujua mambo makuu ya habari mtakayozungumzia.

8. Nĩatĩa ũũmba gũtigĩĩra ũkũgweta mantũ jongwa kĩrĩ ĩromba rĩaku rĩrĩa ũrĩ kĩrĩ wiritani bwa Bibiria?

8 Sala ni sehemu muhimu ya kipindi cha funzo la Biblia, hivyo fikiria mapema kuhusu mambo utakayosema ikiwa utaombwa utoe sala. Ukifanya hivyo, inaelekea utataja mambo hususa katika sala yako. (Zab. 141:2) Hanae, anayeishi nchini Japani, bado anakumbuka sala zilizotolewa na dada fulani aliyeandamana na mwalimu wake wa Biblia. Anasema hivi: “Nilitambua kwamba ana uhusiano wa karibu na Yehova, nami nilitaka kuwa kama yeye. Pia, nilihisi kwamba ninapendwa alipotaja jina langu katika sala zake.”

9. Kũringana na Jakubu 1:19, nĩatĩa ũũmba kũthithia nĩkenda ũrita ũteethio rĩrĩa wagwatwa ũgeni kĩrĩ wiritani bwa Bibiria?

9 Muunge mkono mwalimu wa Biblia wakati wa funzo. Omamuyovbi, dada ambaye ni painia wa pekee nchini Nigeria, anasema hivi: “Mwandamani mzuri anasikiliza kwa makini wakati wa funzo. Anatoa maelezo mazuri wakati wa funzo lakini hazungumzi kupita kiasi, akitambua kwamba ni wajibu wa mwalimu kuongoza funzo la Biblia.” Unaweza kujuaje wakati na jinsi ya kutoa maelezo kwenye funzo? (Met. 25:11) Sikiliza kwa makini mwalimu na mwanafunzi wanapozungumza. (Soma Yakobo 1:19.) Ni kwa kufanya hivyo tu, ndipo utakapokuwa tayari kutoa maelezo wakati unaofaa. Bila shaka, ni lazima uwe na utambuzi. Kwa mfano, hungependa kuzungumza kupita kiasi, kumkatisha mwalimu anapojadiliana na mwanafunzi, au kuanza kuzungumzia habari nyingine. Lakini ukitumia maelezo mafupi, mfano, au swali, unaweza kusaidia kufafanua habari inayozungumziwa. Nyakati fulani, huenda ukahisi kwamba huna mengi ya kuchangia kwenye funzo. Lakini ikiwa utampongeza mwanafunzi na kumwonyesha upendezi wa kibinafsi, utamsaidia sana afanye maendeleo.

10. Nĩatĩa mantũ jarĩa ũcionerete ũtũũrone joomba gũteethia mũritwa wa Bibiria?

10 Msimulie mambo ambayo umepitia maishani. Ikiwa inafaa, kwa ufupi unaweza kumsimulia mwanafunzi jinsi ulivyojifunza kweli, jinsi ulivyoshinda changamoto fulani, au jinsi ambavyo umejionea mkono wa Yehova maishani mwako. (Zab. 78:4, 7) Huenda jambo utakalosimulia ndilo jambo ambalo mwanafunzi alihitaji kusikia. Maelezo yako yanaweza kuimarisha imani yake au kumtia moyo aendelee kufanya maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo. Na huenda yakamwonyesha jinsi anavyoweza kushinda jaribu analokabili. (1 Pet. 5:9) Gabriel, anayeishi nchini Brazili, ambaye sasa anatumikia akiwa painia, anakumbuka jinsi alivyonufaika alipokuwa akijifunza Biblia. Anakumbuka hivi: “Niliposikia masimulizi ya akina ndugu, nilitambua kwamba Yehova anaona changamoto tunazokabili. Na ikiwa waliweza kuzishinda, mimi ningeweza pia.”

RĨRĨA MŨRITWA WA BIBIRIA EEJA MĨCEMANIONE

Sisi sote tunaweza kumtia moyo mwanafunzi aendelee kuhudhuria mikutano (Tazama fungu la 11)

11-12. Nĩkĩ tũkũbatara kũgwata ũgeni aritwa ba Bibiria twĩna nkerũ rĩrĩa beeja mĩcemanione?

11 Ili mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo, ni lazima ahudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na kunufaika kutokana nayo. (Ebr. 10:24, 25) Inaelekea mwalimu wake atamwalika ahudhurie mkutano kwa mara ya kwanza. Anapohudhuria, sisi sote tunaweza kumtia moyo aendelee kuja kwenye Jumba la Ufalme. Tunaweza kufanyaje hivyo kihususa?

12 Mkaribisheni mwanafunzi wa Biblia kwa uchangamfu. (Rom. 15:7) Ikiwa tutamfanya mwanafunzi ahisi amekaribishwa kwenye mikutano, kuna uwezekano mkubwa zaidi kwamba ataendelea kuja kwenye Jumba la Ufalme. Mkaribishe kwa uchangamfu, lakini usipite kiasi na kumlemea, na umtambulishe kwa wengine. Usifikie mkataa kwamba tayari kuna mtu anayemtunza; kwa sababu huenda mwalimu wake amechelewa au anashughulikia majukumu mengine. Msikilize kwa makini mwanafunzi huyo, na umwonyeshe upendezi wa kibinafsi. Kunaweza kuwa na matokeo gani unapomkaribisha mwanafunzi kwa uchangamfu? Fikiria kisa cha Dmitrii, ambaye alibatizwa miaka michache tu iliyopita na sasa anatumikia akiwa mtumishi wa huduma. Anapokumbuka mkutano wake wa kwanza, anasema hivi: “Ndugu fulani aliniona nikisubiri kwa wasiwasi nje ya Jumba la Ufalme na kwa fadhili aliongozana nami kuingia ndani. Watu wengi walikuja kunisalimia. Nilishangaa sana. Nilipendezwa sana na jambo hilo hivi kwamba nilitamani tungekuwa na mikutano kila siku ya juma. Sijawahi kujionea jambo kama hilo mahali pengine popote.”

13. Mwĩtĩre jwaku jũrĩ na nkucanio ĩrĩkũ kĩrĩ mũritwa wa Bibiria?

13 Mwekeeni mfano mzuri. Mwenendo wetu unaweza kumsadikisha mwanafunzi wa Biblia kwamba ameipata kweli. (Mt. 5:16) Vitalii, ambaye sasa anatumikia akiwa painia nchini Moldova, anasema hivi: “Nilijionea jinsi wengine kutanikoni walivyoishi, walivyofikiri, na walivyojiendesha. Hilo lilinisadikisha kwamba kwa kweli Mashahidi wa Yehova wanatembea pamoja na Mungu.”

14. Nĩatĩa ngerekano yaku ĩnjega yũũmba gũteetheeria mũritwa wa Bibiria eeta na mbere?

14 Ili astahili kubatizwa, mwanafunzi wa Biblia anahitaji kutumia mambo anayojifunza. Si rahisi kufanya hivyo sikuzote. Lakini mwanafunzi wa Biblia anapoona jinsi ambavyo kutumia kanuni za Biblia kunavyotunufaisha, anaweza kuchochewa kutuiga. (1 Kor. 11:1) Fikiria kisa cha Hanae aliyetajwa awali. Anaeleza hivi: “Akina ndugu na dada walikuwa wakiishi kulingana na mambo niliyokuwa nikijifunza. Niliona jinsi ninavyoweza kuwa mwenye kutia moyo, kusamehe, na jinsi ninavyoweza kuwaonyesha wengine upendo. Sikuzote walizungumza mambo mazuri kuhusu wengine. Nilitaka kuwaiga.”

15. Njuno 27:17 ĩrĩtũteethia atĩa kwona gĩtũmi gĩa kũthithia ũcoore na mũritwa wa Bibiria rĩrĩa eeta na mbere kwĩja mĩcemanione?

15 Anzisha urafiki na mwanafunzi wa Biblia. Mwanafunzi wa Biblia anapoendelea kuhudhuria mikutano, endelea kumwonyesha upendezi wa kibinafsi. (Flp. 2:4) Kwa nini usijitahidi kumfahamu zaidi? Bila kuingilia mambo yake ya kibinafsi, unaweza kumpongeza kwa mabadiliko yoyote mazuri ambayo amefanya na unaweza kumwuliza kuhusu funzo lake la Biblia, familia yake, na kazi yake. Huenda mazungumzo hayo yakawafanya muwe na uhusiano wa karibu zaidi. Unapoanzisha urafiki na mwanafunzi wa Biblia unamsaidia kufanya maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo. (Soma Methali 27:17.) Sasa, Hanae anatumikia akiwa painia wa kawaida. Anapokumbuka pindi alipohudhuria mikutano kwa mara ya kwanza, anasema hivi: “Nilipopata marafiki kutanikoni, nilianza kutazamia kwa hamu mikutano, na nilihudhuria mikutano hata nilipokuwa nimechoka. Nilifurahia ushirika na marafiki wangu wapya, na hilo lilinisaidia kuvunja urafiki na wale ambao hawakumtumikia Yehova. Nilitaka kuwa na uhusiano wa karibu zaidi na Yehova na ndugu na dada. Hivyo, niliamua kubatizwa.”

16. Nĩmbi ĩngĩ ũũmba kũthithia nĩkenda ũtetheeria mũritwa wa Bibiria aigua angˈanĩri?

16 Mwanafunzi anapoendelea kufanya maendeleo na kufanya mabadiliko, msaidie ahisi kwamba yeye ni sehemu ya kutaniko. Unaweza kufanya hivyo kwa kuwa mkaribishaji wageni. (Ebr. 13:2) Anapofikiria wakati alipokuwa akijifunza Biblia, Denis, ambaye anatumikia nchini Moldova, anakumbuka hivi: “Mara kadhaa, mimi na mke wangu tulialikwa ili tukafurahie ushirika pamoja na akina ndugu. Walitusimulia jinsi ambavyo Yehova aliwasaidia. Jambo hilo lilitutia moyo. Pindi hizo zilisaidia kutusadikisha kwamba tulitaka kumtumikia Yehova na kwamba wakati ujao tungekuwa na maisha mazuri ajabu.” Mwanafunzi wa Biblia anapostahili kuwa mhubiri, unaweza pia kumwalika aandamane nawe katika huduma. Diego, mhubiri kutoka nchini Brazili, anasema hivi: “Akina ndugu wengi walinialika ili niende nao katika huduma. Hiyo ilikuwa njia bora ya kuwafahamu vizuri. Nilipofanya hivyo, nilijifunza mengi, na nilijihisi kuwa karibu zaidi na Yehova na Yesu.”

RĨRĨA ARĨ KĨŨTHŨRANONE NĨATĨA AKŨRŨ BOOMBA KŨMŨTEETHIA?

Enyi wazee, kupendezwa kwenu na wanafunzi kunaweza kuwasaidia wafanye maendeleo (Tazama fungu la 17)

17. Nĩatĩa akũrũ boomba gũteetheeria aritwa ba Bibiria?

17 Tumieni wakati pamoja na wanafunzi wa Biblia. Enyi wazee, kupendezwa kwenu kibinafsi na wanafunzi kunaweza kuwasaidia wafanye maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo. Je, mnaweza kuzungumza kwa ukawaida na wanafunzi wa Biblia kwenye mikutano? Watahisi kwamba mnawajali ikiwa mnakumbuka majina yao, hasa wanapoanza kutoa maelezo. Je, mnaweza kupanga vizuri ratiba zenu mara kwa mara ili kuandamana na mhubiri anapojifunza Biblia na mwanafunzi fulani? Mnaweza kumsaidia sana mwanafunzi wa Biblia kuliko mnavyowazia. Jackie, painia anayeishi nchini Nigeria, anasema hivi: “Wanafunzi wengi wa Biblia wanashtuka wanapotambua kwamba ndugu aliyeandamana nami kwenye funzo lao ni mzee wa kutaniko. Mwanafunzi fulani wa Biblia alisema hivi: ‘Mchungaji wangu hawezi kufanya hivyo kamwe. Anawatembelea tu matajiri na anafanya hivyo ikiwa tu watamlipa pesa!’” Mwanafunzi huyo sasa anahudhuria mikutano.

18. Nĩatĩa akũrũ boomba kũũjũria kaanya karĩa baei ja ũrĩa gũkwonanua kĩrĩ Mathithio 20:28?

18 Wazoezeni na kuwatia moyo walimu wa Biblia. Enyi wazee wa kutaniko, mna jukumu zito la kuwasaidia wahubiri ili wawe na matokeo katika huduma yao, kutia ndani kazi ya kuongoza mafunzo yao ya Biblia. (Soma Matendo 20:28.) Ikiwa mhubiri anaona haya kuongoza funzo la Biblia ukiwepo, jitolee kuliongoza funzo hilo. Jackie, aliyenukuliwa awali, anasema hivi: “Wazee huniuliza kuhusu wanafunzi wangu wa Biblia kwa ukawaida. Ninapopata changamoto wakati wa kuongoza funzo la Biblia, wao hunipa ushauri unaonisaidia.” Wazee wanaweza kufanya mengi ili kuwatia moyo na kuwachochea walimu wa Biblia wasonge mbele. (1 The. 5:11) Jackie anaongezea hivi: “Ninafurahi wazee wanaponitia moyo na kuniambia kwamba wanathamini kazi ninayofanya kwa bidii. Maneno hayo huniburudisha kama kunywa glasi ya maji baridi katika siku yenye joto kali. Pongezi zao zinanisaidia kujiamini zaidi na kuongeza shangwe ninayopata katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia.”—Met. 25:25.

19. Nĩatĩa twinthe tũũmba kwĩthĩrwa na kũgwĩrua?

19 Hata ikiwa kwa sasa hatuongozi funzo la Biblia, bado tunaweza kumsaidia mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. Bila kutawala mazungumzo, tunaweza kuwaunga mkono walimu wa Biblia kupitia maelezo yetu yaliyotayarishwa vizuri. Tunaweza kusitawisha urafiki na wanafunzi wa Biblia wanapokuja kwenye Jumba la Ufalme, na tunaweza kuwawekea kielelezo kizuri. Na wazee wanaweza kuwatia moyo wanafunzi kwa kutenga wakati wa kuwa pamoja nao na wanaweza kuwatia moyo walimu kwa kuwazoeza na kuwapongeza. Kwa kweli, hakuna shangwe kubwa zaidi kuliko kujua kwamba tunachangia hata kwa sehemu ndogo kumsaidia mtu kumpenda na kumtumikia Baba yetu, Yehova.

RWĨMBO 79 Wafundishe Kusimama Imara

^ gic. 5 Kwa sasa, si kila mmoja wetu aliye na pendeleo la kuongoza funzo la Biblia. Hata hivyo, sote tunaweza kumsaidia mtu fulani afanye maendeleo na kufikia ubatizo. Katika makala hii, tutaona jinsi kila mmoja wetu anavyoweza kumsaidia mwanafunzi wa Biblia afikie lengo hilo.