Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 19

Gũtĩkĩo Kĩũmba Kũgitaria Antũ Babaagĩru

Gũtĩkĩo Kĩũmba Kũgitaria Antũ Babaagĩru

“Baria eendi rwatho rwaku batuuraga kiindaji; na bati untu bwa kubagiitaria.—ZAB. 119:165..

RWĨMBO 122 Iweni Imara, Thabiti!

MUHTASARI *

1-2. Mwandĩki ũmwe augĩre atĩa, na nĩmbi tũkairitana kĩthoomone gĩkĩ?

LEO, mamilioni ya watu wanadai kwamba wanamwamini Yesu, lakini hawakubali mambo aliyofundisha. (2 Tim. 4:3, 4) Isitoshe, mwandishi fulani alisema hivi: “Ikiwa kungekuwa na ‘Yesu’ mwingine miongoni mwetu leo, ambaye angesema mambo kama ambayo Yesu mwenyewe alisema . . . , je, tungemkataa kama Yesu alivyokataliwa miaka 2,000 iliyopita? . . . Matendo na mtazamo wa watu wengi unaonyesha kwamba jibu lao ni: Ndiyo, tungemkataa.”

2 Katika karne ya kwanza, watu wengi walimsikia Yesu akifundisha na kumwona akifanya miujiza, lakini walikataa kumwamini. Kwa nini? Katika makala iliyotangulia, tulichunguza sababu nne kwa nini watu walikwazika na mambo ambayo Yesu alisema na kutenda. Acheni tuchunguze sababu nne zaidi. Tunapofanya hivyo, tutaona kwa nini watu leo wanawakataa wafuasi wa Yesu na jinsi tunavyoweza kuepuka kukwazika.

(1) JESŨ ATA-ATHŨRA

Watu wengi walikwazika kwa sababu ya watu ambao Yesu alichagua kushirikiana nao. Jambo hilo linaweza kuwakwazaje watu leo? (Tazama fungu la 3) *

3. Nĩmbi Jesu athuurĩre kũthithia birĩa biatũmĩre antũ bamwe bagitara?

3 Yesu alipokuwa duniani, alichagua kushirikiana na watu wa aina zote. Alikula pamoja na matajiri na wenye mamlaka, lakini pia alitumia muda wake mwingi pamoja na maskini na watu waliokandamizwa. Pia, aliwahurumia watu ambao walionwa kuwa “watenda dhambi.” Watu waliojiona kuwa waadilifu walikwazika kwa sababu ya mambo ambayo Yesu alifanya. Waliwauliza hivi wanafunzi wake: “Kwa nini mnakula na kunywa pamoja na wakusanya kodi na watenda dhambi?” Ili kuwajibu, Yesu alisema: “Watu wenye afya hawahitaji daktari, lakini wagonjwa wanamhitaji. Sikuja kuwaita waadilifu, bali kuwahimiza watenda dhambi watubu.”—Luka 5:29-32.

4. Kũringana na Kĩroria Isaya, nĩmbi Ayahudi babataraga kwĩrĩgĩĩra kĩegie Mesiya?

4 Maandiko yanasema nini? Muda mrefu kabla ya Masihi kuja, nabii Isaya alimfafanua kuwa mtu ambaye hangekubaliwa na ulimwengu. Unabii huo ulitabiri hivi: “Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu . . . Ilikuwa kana kwamba uso wake ulifichwa kutoka kwetu. Alidharauliwa, nasi tulimwona kuwa asiye na maana.” (Isa. 53:3) Masihi angeepukwa “na wanadamu,” kwa hiyo Wayahudi hao wa karne ya kwanza walipaswa kutarajia kwamba Yesu angekataliwa.

5. Nĩatĩa antũ babaingi boonaga athingati ba Jesũ ntukũne cietũ?

5 Je, tunaona tatizo hilo leo? Ndiyo. Makasisi wengi wanafurahia kuwakubali katika dini zao watu ambao ni mashuhuri, matajiri, na wanaoonwa na ulimwengu kuwa wenye hekima. Makasisi hao wanafanya hivyo hata ingawa maadili na njia ya maisha ya washiriki hao wapya mara nyingi haipatani na viwango vya Mungu. Makasisi haohao wanawadharau watumishi wa Yehova wenye bidii na maadili safi kwa sababu wao si mashuhuri kulingana na viwango vya ulimwengu huu. Ni kama tu mtume Paulo alivyosema, Mungu aliwachagua wale ‘wanaodharauliwa.’ (1 Kor. 1:26-29) Hata hivyo, machoni pa Yehova, watumishi wake wote waaminifu ni wenye thamani.

6. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na mwonere jwa Jesu, o ta ũrĩa gũtarĩrĩĩtue kĩrĩ Mathayo 11:25, 26?

6 Tunaweza kuepukaje kukwazika? (Soma Mathayo 11:25, 26.) Usikubali kuathiriwa na maoni ya ulimwengu kuhusu watu wa Mungu. Tambua kwamba Yehova huwatumia tu watu wanyenyekevu ili wafanye mapenzi yake. (Zab. 138:6) Tafakari kuhusu jinsi ambavyo ametimiza mambo mengi kwa kuwatumia watu ambao ulimwengu unawaona kuwa hawana hekima au si wasomi.

(2) JESŨ NAAGWUŨRĨRE MOORITANI JA ŨRONGO

7. Nĩkĩ Jesũ eetĩre Afarisayo aciayia, nabo bathithĩrie atĩa?

7 Kwa ujasiri Yesu alishutumu matendo ya kinafiki ya viongozi wa kidini wa siku zake. Kwa mfano, alifunua unafiki wa Mafarisayo ambao walihangaikia sana jinsi walivyoosha mikono yao kuliko walivyowatunza wazazi wao. (Mt. 15:1-11) Huenda wanafunzi wa Yesu walishangazwa na maneno yake. Isitoshe, walimuuliza hivi: “Unajua kwamba Mafarisayo walikwazika waliposikia mambo uliyosema?” Yesu aliwajibu hivi: “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hakuupanda utang’olewa. Waacheni. Wao ni viongozi vipofu. Basi, kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili watatumbukia ndani ya shimo.” (Mt. 15:12-14) Yesu hakuruhusu hasira ya viongozi hao wa kidini imzuie kusema ukweli.

8. Jesũ onanĩrie atĩa tĩ mooritani jonthe ja kĩdini jetĩkĩrĩkaga kĩ Mũrungu?

8 Pia, Yesu alifunua mafundisho ya kidini ya uwongo. Hakusema kwamba imani zote za kidini zinakubalika machoni pa Mungu. Badala yake, alizungumza kuhusu watu wengi ambao wangekuwa kwenye barabara yenye nafasi kubwa inayoongoza kwenye uharibifu, lakini alisema ni wachache tu wangekuwa kwenye barabara yenye nafasi ndogo inayoongoza kwenye uzima. (Mt. 7:13, 14) Alisema wazi kwamba baadhi ya watu wangedai wanamtumikia Mungu, lakini kihalisi hawakuwa wanamtumikia. Alionya hivi: “Jihadharini na manabii wa uwongo ambao huja kwenu katika mavazi ya kondoo, lakini ndani wao ni mbwamwitu wakali. Kwa matunda yao mtawatambua.”—Mt. 7:15-20.

Watu wengi walikwazika kwa sababu ya jinsi Yesu alivyoshutumu imani na mazoea ya uwongo. Jambo hilo linaweza kuwakwazaje watu leo? (Tazama fungu la 9) *

9. Nĩ mooritani jarĩkũ ja ũrongo Jesũ agwuũrĩre?

9 Maandiko yanasema nini? Kuhusu Masihi, Biblia ilitabiri kwamba bidii kwa ajili ya nyumba ya Yehova ingemla. (Zab. 69:9; Yoh. 2:14-17) Bidii hiyo ilimchochea Yesu kufunua imani na mazoea ya uwongo ya kidini. Kwa mfano, Mafarisayo walifundisha kwamba nafsi haiwezi kufa; Yesu alifundisha kwamba wafu wamelala usingizi. (Yoh. 11:11) Masadukayo walipinga ufufuo; Yesu alimfufua Lazaro, rafiki yake. (Yoh. 11:43, 44; Mdo. 23:8) Mafarisayo walifundisha kwamba kila kitu kinachotokea ni majaliwa, au kinasababishwa na Mungu; Yesu alifundisha kwamba wanadamu wanaweza kuchagua kumtumikia Mungu au la.—Mt. 11:28.

10. Nĩkĩ babaingĩ bagitaragua nĩ mooritani jeetũ?

10 Je, tunaona tatizo hilo leo? Ndiyo. Watu wengi wanakwazika kwa sababu mafundisho yetu yanayotegemea Biblia yanafunua mafundisho ya uwongo kidini. Makasisi wanafundisha wafuasi wao kwamba Mungu huwaadhibu waovu kwenye moto wa mateso. Wanatumia mafundisho hayo ya uwongo kuwadhibiti watu. Tukiwa watumishi wa Yehova wanaomwabudu Mungu mwenye upendo, tunafunua fundisho hilo la uwongo. Pia, makasisi wanafundisha kwamba nafsi haiwezi kufa. Sisi tunafunua chanzo cha kipagani cha fundisho hilo, ambalo ikiwa lingekuwa la kweli, ufufuo usingehitajika. Kinyume na fundisho la kwamba Mungu hupanga mambo yote kimbele—ambalo dini nyingi zinafundisha—sisi tunafundisha kwamba wanadamu wana uhuru wa kuchagua na wanaweza kuchagua kumtumikia Mungu. Viongozi wa kidini wanatendaje tunapofunua mafundisho yao ya uwongo? Mara nyingi, wanakasirika sana!

11. Kũringana na biugo bia Jesũ birĩa bikwoneka kĩrĩ Johana 8:45-47, nĩmbi Mũrungu akwĩrĩgĩĩra kuuma kĩrĩ antũ baawe?

11 Tunaweza kuepukaje kukwazika? Ikiwa tunaipenda kweli, ni lazima tuyakubali maneno ya Mungu. (Soma Yohana 8:45-47.) Tofauti na Shetani Ibilisi, sisi tunasimama imara katika kweli. Sikuzote tunashikamana na mambo tunayoamini. (Yoh. 8:44) Mungu anataka watu wake ‘wachukie maovu’ na ‘kushikamana na mema,’ kama tu Yesu alivyofanya.—Rom. 12:9; Ebr. 1:9.

(3) JESŨ NATHAANGĨKĨRUE

Watu wengi walikwazika kwa sababu ya jinsi Yesu alivyokufa kwenye mti wa mateso. Jambo hilo linaweza kuwakwazaje watu leo? (Tazama fungu la 12) *

12. Nĩkĩ ũrĩa Jesũ akuĩre kwagitarĩrie Ayahudi babaingĩ?

12 Ni jambo gani lingine ambalo liliwakwaza Wayahudi katika siku za Yesu? Paulo alisema hivi: “Tunamhubiri Kristo aliyeuawa kwenye mti, kwa Wayahudi ni sababu ya kujikwaa.” (1 Kor. 1:23) Kwa nini Wayahudi wengi walihangaishwa na njia ambayo Yesu alikufa? Kulingana na maoni yao, Yesu kufa kwenye mti wa mateso kulifanya aonekane kuwa mhalifu na mtenda dhambi, na si Masihi.—Kum. 21:22, 23.

13. Nĩmbi barĩa bagitarĩtue nĩ Jesũ batamenyere?

13 Wayahudi ambao walikwazika kwa sababu ya Yesu walishindwa kutambua kwamba hakuwa na hatia, kwamba alishtakiwa kwa uwongo, na kwamba alitendewa isivyo haki. Wale ambao walikuwa wanaendesha kesi yake hawakutenda kwa haki. Washiriki wa mahakama kuu ya Kiyahudi walikusanyika haraka, na waliendesha kesi hiyo bila kufuata utaratibu uliowekwa. (Luka 22:54; Yoh. 18:24) Badala ya kusikiliza bila ubaguzi mashtaka na ushahidi dhidi ya Yesu, watu hao waliomhukumu walitafuta “ushahidi wa uwongo dhidi ya Yesu ili wamuue.” Mbinu yao iliposhindikana, kuhani mkuu alijaribu kumtega Yesu ili aseme jambo ambalo wangeweza kutumia kumshtaki. Hilo lilikuwa kinyume kabisa na sheria zilizowekwa. (Mt. 26:59; Marko 14:55-64) Baada ya Yesu kufufuliwa kutoka kwa wafu, mahakimu hao wasio waadilifu waliwalipa askari wa Roma ambao walikuwa wanalinda kaburi lake, “kiasi kikubwa cha fedha” ili wasambaze hadithi ya uwongo iliyoeleza kwa nini kaburi lilikuwa tupu.—Mt. 28:11-15.

14. Nĩatĩa Maandĩko jaugĩte bũkonie gĩkuũ kĩa Mesiya?

14 Maandiko yanasema nini? Ingawa Wayahudi wengi katika siku za Yesu hawakutarajia kwamba Masihi angehitaji kufa, Maandiko yalitabiri hivi: “Aliumwaga uhai wake mpaka kifo naye alihesabiwa miongoni mwa wakosaji; aliibeba dhambi ya watu wengi, naye aliwatetea wakosaji.” (Isa. 53:12) Hivyo, Wayahudi hawakuwa na sababu ya kukwazika Yesu alipouawa kama mtenda dhambi.

15. Nĩ nthitango irĩkũ ikonie akũũjĩ ba Jehova itũmĩte bamwe bagitarua?

15 Je, tunaona tatizo hilo leo? Bila shaka! Yesu alishtakiwa na kuhukumiwa isivyo haki, na Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakitendewa kwa njia hiyohiyo isiyo ya haki. Tuchunguze mifano kadhaa. Nchini Marekani katika miaka ya 1930 na 1940, uhuru wetu wa kumwabudu Mungu ulipingwa mahakamani tena na tena. Baadhi ya mahakimu, walitubagua bila aibu. Katika jimbo la Quebec, Kanada, Kanisa Katoliki lilishirikiana bega kwa bega na serikali ili kupinga kazi yetu. Wahubiri wengi walifungwa gerezani kwa sababu tu waliwaeleza majirani zao kuhusu Ufalme wa Mungu. Nchini Ujerumani, wakati wa serikali ya Wanazi, ndugu wengi vijana waaminifu waliuawa na utawala huo usiomwogopa Mungu. Katika miaka ya karibuni, ndugu zetu wengi nchini Urusi wamehukumiwa na kufungwa gerezani kwa sababu ya kuzungumza na wengine kuhusu Biblia, jambo ambalo wenye mamlaka wanadai kwamba ni utendaji wenye “msimamo mkali.” Hata Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika lugha ya Kirusi imepigwa marufuku na kutangazwa kuwa ni chapisho lenye “msimamo mkali” kwa sababu linatumia jina Yehova.

16. O jaũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ 1 Johana 4:1, nĩkĩ tũtĩbuĩri kwaaĩrua nĩ ngono cia ũrongo ikonie antũ ba Jehova?

16 Tunaweza kuepukaje kukwazika? Tafuta habari kamili. Katika Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu aliwaonya wasikilizaji wake kwamba baadhi ya watu ‘wangewasingizia kila aina ya uovu.’ (Mt. 5:11) Chanzo cha uwongo huo ni Shetani. Yeye huwachochea wapinzani waeneze uchongezi mbaya sana kuhusu wale wanaoipenda kweli. (Ufu. 12:9, 10) Ni lazima tukatae uwongo unaosemwa na wapinzani wetu. Hatupaswi kamwe kuruhusu uwongo kama huo ututetemeshe au kudhoofisha imani yetu.—Soma 1 Yohana 4:1.

(4) JESŨ NAKUNYANĨĨRWE NA ATIGANĨRUA

Watu wengi walikwazika kwa sababu ya jinsi Yesu alivyosalitiwa na Yuda. Jambo hilo linaweza kuwakwazaje watu leo? (Tazama fungu la 17 na 18) *

17. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ mantũ jarĩa jathingatĩre gĩkuũ kĩa Jesũ jarĩngĩgitaria antũ bamwe?

17 Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu alisalitiwa na mmoja wa mitume wake 12. Mtume mwingine alimkana Yesu mara tatu, na mitume wake wote walimwacha usiku uliotangulia kifo chake. (Mt. 26:14-16, 47, 56, 75) Yesu hakushangazwa na jambo hilo. Hata alikuwa ametabiri kwamba mambo hayo yangetokeaa. (Yoh. 6:64; 13:21, 26, 38; 16:32) Walipoona mambo hayo, huenda baadhi ya watu wangeweza kukwazika, wakitoa sababu kwamba ‘Ikiwa hivyo ndivyo mitume wa Yesu wanavyojiendesha, mimi sitaki kuwa mmoja wao!’

18. Nĩ moororia jarĩkũ joojũrĩrue kĩrĩ mantũ jarĩa jathiũrũkĩrĩte gĩkuũ kĩa Jesũ?

18 Maandiko yanasema nini? Karne nyingi mapema, Yehova alifunua katika Neno lake kwamba Masihi angesalitiwa kwa vipande thelathini vya fedha. (Zek. 11:12, 13) Msaliti angekuwa mtu wa karibu wa Yesu. (Zab. 41:9) Nabii Zekaria pia aliandika hivi: “Mpige mchungaji, acha kondoo watawanyike.” (Zek. 13:7) Badala ya kukwazwa na matukio hayo, watu wenye mioyo minyoofu walipaswa kuimarishwa kwa kuona unabii huo mbalimbali ukitimizwa kupitia Yesu.

19. Nĩatĩa antũ barĩa baarĩ na mwerekera jũmwega baamenyere?

19 Je, tunaona tatizo hilo leo? Ndiyo. Katika nyakati zetu, Mashahidi wachache wanaojulikana sana wameiacha kweli, wakawa waasi-imani, na kisha wanajaribu kuwapotosha wengine. Wameeneza ripoti mbaya, kweli nusu-nusu, na uwongo wa moja kwa moja kuhusu Mashahidi wa Yehova kupitia vyombo vya habari na Intaneti. Lakini watu wenye mioyo minyoofu hawakwaziki. Badala yake, wanatambua kwamba Biblia ilitabiri kwamba mambo kama hayo yangetokea.—Mt. 24:24; 2 Pet. 2:18-22.

20. Nĩatĩa tũũmba kweba kũgitarua nĩ antũ barĩa batiganĩte na ũmma? (2 Timotheo 4:4, 5)

20 Tunaweza kuepukaje kukwazika? Tunahitaji kuimarisha imani yetu kwa kujifunza kwa ukawaida, kwa kusali bila kuacha, na kuwa na bidii katika kazi ambayo Yehova ametupatia tuifanye. (Soma 2 Timotheo 4:4, 5.) Ikiwa tuna imani, hatutaogopa tunaposikia ripoti mbaya kuhusu Mashahidi wa Yehova. (Isa. 28:16) Upendo wetu kwa Yehova, Neno lake, na ndugu zetu utatusaidia kuepuka kukwazwa na wale walioiacha kweli.

21. Kinya gũkeethĩrwa antũ babaingĩ nĩ bareganaga na ntũmĩĩri yetũ, twĩthĩrwe na ũmma bũrĩkũ?

21 Katika karne ya kwanza, wengi walikwazika, na walimkataa Yesu. Hata hivyo, wengine wengi walimkubali Yesu. Watu hao walitia ndani angalau mshiriki mmoja wa Sanhedrini ya Wayahudi na hata “umati mkubwa wa makuhani.” (Mdo. 6:7; Mt. 27:57-60; Marko 15:43) Vivyo hivyo leo, mamilioni ya watu hawajakwazika. Kwa nini? Kwa sababu wanajua na wanazipenda kweli zinazopatikana katika Maandiko. Neno la Mungu linasema hivi: “Wale wanaoipenda sheria yako wana amani nyingi; hakuna chochote kinachoweza kuwakwaza.”—Zab. 119:165.

RWĨMBO 124 Washikamanifu Sikuzote

^ gic. 5 Katika makala iliyotangulia, tulizungumzia sababu nne zilizofanya watu wamkatae Yesu wakati uliopita, na kwa nini wanawakataa wafuasi wake leo. Katika makala hii, tutachunguza sababu nne zaidi. Pia, tutaona kwa nini watu wenye mioyo minyoofu wanaompenda Yehova hawaruhusu kitu chochote kiwakwaze.

^ gic. 60 MAELEZO YA PICHA: Yesu akishiriki mlo pamoja na Mathayo na wakusanya kodi.

^ gic. 62 MAELEZO YA PICHA: Yesu akiwafukuza hekaluni wafanyabiashara.

^ gic. 64 MAELEZO YA PICHA: Yesu analazimishwa kubeba mti wa mateso.

^ gic. 66 MAELEZO YA PICHA: Yuda anamsaliti Yesu kwa kumbusu.