Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 20

Tũũria Mwonere Jũmwega Jwegie Ũtungatĩri Bwaku

Tũũria Mwonere Jũmwega Jwegie Ũtungatĩri Bwaku

“Umaaria mbeu ciaku waande, . . . ugatiiria. . . waandi.”—MU. 11:6..

RWĨMBO 70 Tafuteni Wanaostahili

MUHTASARI *

Baada ya Yesu kwenda mbinguni, wanafunzi wake wanahubiri kwa bidii katika Yerusalemu na maeneo mengine mengi (Tazama fungu la 1)

1. Nĩ ngerekano ĩrĩkũ Jesu ekĩĩre athingati baawe, na baathithĩrie atĩa? (Ona mbica karatasine ka mbere.)

YESU alidumisha mtazamo unaofaa wakati wa huduma yake yote alipokuwa duniani, na anataka wafuasi wake pia wadumishe mtazamo unaofaa katika huduma. (Yoh. 4:35, 36) Yesu alipokuwa pamoja na wanafunzi wake, walikuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri. (Luka 10:1, 5-11, 17) Hata hivyo, Yesu alipokamatwa na kuuawa, kwa muda mfupi wanafunzi walipoteza tamaa yao ya kuhubiri. (Yoh. 16:32) Alipofufuliwa, Yesu aliwahimiza wakazie fikira kazi ya kuhubiri. Na baada ya Yesu kurudi mbinguni, walihubiri kwa bidii sana hivi kwamba maadui wao walilalamika na kusema hivi: “Tazama! mmejaza Yerusalemu fundisho lenu.”—Mdo. 5:28.

2. Nĩatĩa Jehova atharimĩte ngũgĩ ya gũtũmĩĩria?

2 Yesu aliongoza kazi iliyofanywa na Wakristo hao wa karne ya kwanza, na Yehova aliwabariki na wakawa na ongezeko. Kwa mfano, siku ya Pentekoste 33 W.K., watu karibu 3,000 walibatizwa. (Mdo. 2:41) Na idadi ya wanafunzi iliendelea kuongezeka haraka sana. (Mdo. 6:7) Yesu alitabiri kwamba kazi ya kuhubiri ingefanikiwa hata zaidi katika siku za mwisho.—Yoh. 14:12; Mdo. 1:8.

3-4. Nĩkĩ antũ bamwe boonaga ngũgĩ ya gũtũmĩĩria ĩrĩ ĩnjũmũ, na nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

3 Sote tunajitahidi kudumisha mtazamo unaofaa kuhusu huduma. Katika baadhi ya nchi ni rahisi kufanya hivyo. Kwa nini? Kwa sababu watu wengi sana wanapenda kujifunza Biblia hivi kwamba baadhi yao inabidi wasubiri hadi Shahidi wa Yehova atakapopata nafasi ya kujifunza nao! Lakini katika sehemu nyingine za dunia, ni vigumu sana kuhubiri kwa sababu watu hawapatikani nyumbani, na watu wanaopatikana nyumbani hawapendezwi sana na ujumbe wetu wa Biblia.

4 Ikiwa unaishi katika eneo ambalo ni vigumu kuhubiri, inaelekea mapendekezo yatakayotolewa katika makala hii yatakusaidia. Tutachunguza mambo ambayo baadhi ya wahubiri wanafanya ili kuwapata watu wengi zaidi katika huduma yao. Na tutachunguza kwa nini tunaweza kudumisha mtazamo unaofaa, iwe watu wanaitikia vizuri ujumbe wetu au la.

TŨŨRIA MWONERE JŨMWEGA KINYA RĨRĨA ANTŨ BATĨKWONORA

5. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ Akũũjĩ ba Jehova babaingĩ bacemanagia najo?

5 Ni vigumu sana kwa Mashahidi wengi kuwapata watu nyumbani. Baadhi ya wahubiri wanaishi katika maeneo ambayo majengo mengi yana ulinzi mkali au watu hawaruhusiwi kuingia. Huenda majengo hayo yana mlinzi ambaye haruhusu mtu yeyote asiye na mwaliko kutoka kwa mtu hususa kuingia. Wahubiri wengine wanaweza kwenda nyumba kwa nyumba bila kizuizi chochote lakini wanapata watu wachache nyumbani. Wahubiri wengine wanahubiri maeneo ya vijijini au maeneo ya mbali ambako kuna watu wachache. Huenda wahubiri wakatembea umbali mrefu ili kumtafuta mwenye nyumba mmoja tu, ambaye huenda hata wasimpate nyumbani! Ikiwa tunakabili changamoto hizo hatupaswi kukata tamaa. Tunaweza kufanya nini ili kushinda changamoto hizo na kupata matokeo mazuri katika huduma?

6. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ atũmĩĩria nĩ ta agwatia ba makũyũ?

6 Yesu alilinganisha kazi ya kuhubiri na kazi ya uvuvi. (Marko 1:17) Baadhi ya wavuvi wanaweza kwenda kuvua kwa siku kadhaa bila kupata samaki yeyote. Lakini hawakati tamaa; wanabadilikana kulingana na hali. Wanabadili muda wanaokwenda kuvua, eneo, au mbinu wanazotumia kuvua. Tunaweza kufanya mabadiliko kama hayo katika huduma yetu. Fikiria mapendekezo yafuatayo.

Unapohubiri katika maeneo ambayo si rahisi kuwapata watu nyumbani, jaribu kuwatafuta wakati mwingine, kwenye eneo tofauti, au kwa kutumia mbinu nyingine (Tazama fungu la 7 hadi 10) *

7. Maumĩĩra joomba kwĩthĩrwa jarĩ jarĩkũ twatũmĩĩria magita mwanya mwanya?

7 Jitahidi kuwatafuta watu wakati tofauti. Tutawapata watu wengi zaidi ikiwa tutahubiri wakati ambao kuna uwezekano mkubwa wako nyumbani. Isitoshe, kila mtu hurudi nyumbani wakati fulani! Ndugu na dada wengi wanaona inafaa zaidi kuhubiri wakati wa mchana au jioni kwa sababu wanawapata watu wengi zaidi nyumbani. Pia, huenda wenye nyumba wakawa huru na tayari zaidi kuzungumza nasi wakati huo. Au huenda ukaona inafaa kutumia pendekezo kutoka kwa mzee wa kutaniko anayeitwa David. Anasema kwamba baada ya yeye na mwandamani wake kuhubiri kwa muda fulani katika eneo, wanarudi siku hiyohiyo tena kwenye nyumba ambazo hawakuwapata watu mara ya kwanza. Anasema hivi: “Ninashangazwa na idadi kubwa ya watu tunaowakuta nyumbani tunaporudi mara ya pili.” *

Unapohubiri katika maeneo ambayo si rahisi kuwapata watu nyumbani, jaribu kuwatafuta wakati mwingine (Tazama fungu la 7 na 8)

8. Nĩatĩa tũũmba gũtumĩra Mutumiiria 11:6 ũtungatĩrine bwetũ?

8 Hatupaswi kukata tamaa. Andiko letu la msingi linatukumbusha mtazamo tunaopaswa kuwa nao. (Soma Mhubiri 11:6.) David aliyetajwa awali, hakukata tamaa. Hatimaye, katika nyumba moja alimpata mwenye nyumba baada ya kurudi mara kadhaa bila mafanikio. Mwanamume huyo alivutiwa na mazungumzo ya Biblia, naye alisema, “Nimeishi hapa kwa karibu miaka nane, na sijawahi kamwe kutembelewa na Mashahidi wa Yehova nyumbani.” David anasema hivi: “Nimegundua kwamba unapofaulu kuwapata watu nyumbani, mara nyingi wanasikiliza vizuri ujumbe tunaohubiri.”

Unapohubiri katika maeneo ambayo si rahisi kuwapata watu nyumbani, jaribu kuwatafuta kwenye eneo tofauti (Tazama fungu la 9)

9. Nĩatĩa atũmĩĩria bamwe bombanĩte gũcemania na antũ barĩa batĩonekaga nja?

9 Jaribu eneo tofauti. Ili kuwapata watu ambao ni vigumu kupatikana nyumbani, baadhi ya wahubiri wamebadili eneo wanalohubiri. Kwa mfano, mahubiri ya barabarani na ya kutumia vigari vya machapisho yameonekana kuwa njia yenye matokeo ya kuwafikia watu ambao wanaishi kwenye majengo makubwa ambako mahubiri ya nyumba kwa nyumba hayaruhusiwi. Njia hiyo inawawezesha Mashahidi kuzungumza moja kwa moja na watu ambao wanaishi kwenye majengo hayo. Pia, wahubiri wengi wamegundua kwamba ni rahisi zaidi kwa watu kukubali kuzungumza au kupokea machapisho wanapokuwa kwenye bustani za umma, sokoni, na kwenye maeneo ya biashara. Floiran, mwangalizi wa mzunguko nchini Bolivia, anasema hivi: “Tunaenda sokoni na maeneo ya biashara kati ya saa saba mchana na saa tisa alasiri wakati wateja wamepungua. Mara nyingi tunakuwa na mazungumzo mazuri na hata kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na wafanyabiashara.”

Unapohubiri katika maeneo ambayo si rahisi kuwapata watu nyumbani, jaribu kuwatafuta kwa kutumia mbinu nyingine (Tazama fungu la 10)

10. Nĩ njĩra irĩkũ ũũmba gũtumĩra gũkinyĩra antũ?

10 Jaribu mbinu tofauti. Tuseme umejaribu tena na tena kumtembelea mtu fulani ili uzungumze naye ana kwa ana. Umemtembelea muda tofauti-tofauti lakini bado hujampata nyumbani. Je, kuna njia nyingine za kumfikia mtu huyo? Katarína anasema hivi: “Ninawaandikia barua watu ambao sijawahi kuwapata nyumbani, nikiwaeleza kile nilichotaka kuwaambia ana kwa ana.” Wazo kuu ni nini? Jitahidi kumfikia kila mtu katika eneo lako kwa njia moja au nyingine unaposhiriki katika huduma.

ĨTHĨRWA NA MWEREKERA JŨMWEGA RĨRĨA ANTŨ BATĨGWĨTĨKĨRIA NTŨMĨĨRI

11. Nĩkĩ antũ bamwe batĩĩtĩkagĩĩria ntũmĩĩri yetũ?

11 Baadhi ya watu hawapendezwi na ujumbe wetu. Hawaoni umuhimu wa kumjua Mungu au Biblia. Hawamwamini Mungu kwa sababu wanaona mateso mengi katika ulimwengu. Wanaikataa Biblia kwa sababu wanaona unafiki wa viongozi wa kidini wanaodai kwamba wanaishi kulingana na viwango vya Biblia lakini wanafanya mambo mengi mabaya. Wengine wamelemewa na kazi zao, familia, au matatizo ya kibinafsi, na wanashindwa kuona jinsi ambavyo Biblia inaweza kuwasaidia. Tunaweza kudumishaje shangwe yetu ikiwa watu tunaowahubiria hawaoni umuhimu wa ujumbe wetu?

12. Afilipi 2:4 yũũmba gũtũtethia atĩa rĩrĩa tũrĩ ũtungatĩrine?

12 Waonyeshe upendezi wa kibinafsi. Watu wengi ambao mara ya kwanza walikuwa hawapendezwi na habari njema baadaye walikubali kusikiliza walipoona kwamba mhubiri alikuwa anapendezwa nao kibinafsi. (Soma Wafilipi 2:4.) Kwa mfano, David, aliyenukuliwa awali, anasema hivi: “Ikiwa mtu anasema kwamba hapendezwi, tunaweka kando Biblia au chapisho letu na kumwambia hivi: ‘Ningependa kujua kwa nini unahisi hivyo.’” Watu wanaweza kutambua ikiwa mtu anawajali. Huenda hawatakumbuka jambo tulilosema, lakini watakumbuka jinsi tulivyowafanya wahisi. Hata ikiwa wenye nyumba hawaturuhusu tuzungumze nao, tunaweza kuonyesha kwamba tunawajali kupitia jinsi tunavyotenda na ishara za uso wetu.

13. Nĩatĩa tũũmba kũgarũra ntũmĩĩri yeetũ ĩingia ũbatu bwa muntũ ũrĩa tũgũtũmĩĩrĩria?

13 Tunaonyesha upendezi wa kibinafsi tunapobadili ujumbe wetu ili ufaane na mahitaji na mapendezi ya mwenye nyumba. Kwa mfano, kuna mambo yoyote yanayoonyesha kwamba mwenye nyumba ana watoto? Huenda wazazi wakapendezwa na ushauri wa Biblia kuhusu jinsi ya kulea watoto au mapendekezo kuhusu jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Je, tunaona makufuli kadhaa mlangoni? Tunaweza kuamua kuzungumza kuhusu uhalifu na hofu ambayo imeenea ulimwenguni, huenda baadaye mwenye nyumba akathamini kujifunza kuhusu jinsi uhalifu utakavyoondolewa kabisa. Vyovyote vile, jitahidi kuwasaidia wale wanaosikiliza waone jinsi ushauri wa Biblia unavyoweza kuwasaidia. Katarína, aliyetajwa awali, anasema hivi: “Huwa ninajikumbusha jinsi kweli ilivyofanya maisha yangu yawe bora.” Matokeo ni kwamba Katarína anazungumza kwa usadikisho, na watu anaozungumza nao bila shaka wanaona hilo.

14. Kuumania na Njuno 27:17, nĩatĩa tũũmba gũteethanĩĩria na ũrĩa tũrĩ nawe ũtungatĩrine?

14 Nufaika na msaada wa wengine. Katika karne ya kwanza, Paulo alishiriki pamoja na Timotheo mbinu zake za kuhubiri na kufundisha, naye alimtia moyo Timotheo atumie mbinu hizo kuwasaidia wengine. (1 Kor. 4:17) Kama Timotheo, tunaweza kujifunza kutoka kwa ndugu na dada wenye uzoefu kutanikoni. (Soma Methali 27:17.) Kwa mfano, mfikirie ndugu anayeitwa Shawn. Kwa kipindi fulani, alifanya upainia katika eneo la kijijini ambalo watu wengi wameridhika na dini zao. Alidumishaje shangwe yake? Anasema hivi: “Kila ilipowezekana, nilihubiri nikiwa na mwandamani. Tulitumia muda tuliokuwa tukitembea kutoka nyumba moja hadi nyingine kusaidiana kuboresha ustadi wetu wa kufundisha. Kwa mfano, tulizungumzia jinsi ambavyo mazungumzo yetu na mwenye nyumba yalivyokuwa. Kisha, tungejadili jinsi tunavyoweza kuzungumzia jambo hilo kwa njia tofauti ikiwa tutakutana na kisa kingine kama hicho.”

15. Nĩkĩ ĩromba rĩrĩ rĩa bata rĩrĩa tũrĩ ũtungatĩrine?

15 Sali kwa Yehova ili akusaidie. Tafuta mwongozo wa Yehova kila wakati unapokuwa katika huduma. Pasipo msaada wa roho yake takatifu yenye nguvu, hakuna anayeweza kutimiza jambo lolote. (Zab. 127:1; Luka 11:13) Unaposali kwa Yehova ili akusaidie, taja jambo hususa. Kwa mfano, mwombe akuelekeze kwa mtu yeyote mwenye mwelekeo unaofaa na aliye tayari kusikiliza. Kisha, tenda kulingana na sala yako kwa kuwahubiria wote unaokutana nao.

16. Nĩkĩ kwiritana muntũ kĩũmbe bũrĩ ũntũ bwa bata nĩkenda tũũmbana ũtungatĩrine?

16 Tenga wakati kwa ajili ya funzo la kibinafsi. Neno la Mungu linasema: “Mjihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.” (Rom. 12:2) Kadiri tunavyozidi kusadiki kwamba tunajua kweli kumhusu Mungu, ndivyo usadikisho wetu utakavyokuwa mkubwa zaidi tunapozungumza na wengine katika huduma. Katarína, aliyetajwa awali anasema hivi: “Wakati fulani uliopita, nilitambua kwamba nilihitaji kuimarisha imani yangu kuhusu baadhi ya mafundisho ya msingi ya Biblia. Hivyo, nilijifunza kwa kina uthibitisho kwamba kuna Muumba, kwamba Biblia ni Neno la Mungu, na kwamba Mungu ana tengenezo linalomwakilisha leo.” Katarína anasema kwamba funzo lake la kibinafsi liliimarisha imani yake na kuongeza shangwe yake katika huduma.

NĨKĨ TWĨTHĨRWE NA MWONERE JŨMWEGA ŨTUNGATĨRINE BWETŨ

17. Nĩkĩ tontũ Jesũ aarĩ na mwonere jũmwega kĩrĩ ũtungatĩri bwawe?

17 Yesu alidumisha mtazamo unaofaa na kuendelea kuhubiri hata ingawa baadhi ya watu hawakupendezwa na ujumbe wake. Kwa nini? Alijua jinsi watu walivyohitaji sana kujifunza kweli, na alitaka kuwapatia watu wengi iwezekanavyo fursa ya kukubali ujumbe wa Ufalme. Pia, alijua kwamba baadhi ya watu ambao mwanzoni hawakupendezwa, mwishowe wangeitikia vizuri. Fikiria kile kilichotokea katika familia yake mwenyewe. Katika kipindi chote cha miaka mitatu na nusu ya huduma yake, hakuna hata ndugu yake mmoja aliyekuwa mwanafunzi wake. (Yoh. 7:5) Lakini baada ya ufufuo wake, walikuja kuwa Wakristo.—Mdo. 1:14.

18. Nĩkĩ twĩtaga na mbere gũtũmĩĩria?

18 Hatujui ni nani ambaye mwishowe atakubali kweli za Biblia tunazofundisha. Baadhi ya watu huchukua muda mrefu kuliko wengine kukubali ujumbe wetu. Hata wale ambao hawataki kutusikiliza wanaona mwenendo na mtazamo wetu mzuri, na huenda hatimaye wakaanza “kumtukuza Mungu.”—1 Pet. 2:12.

19. Kũringana na 1 Akorintho 3:6, 7, nĩmbi tũbwĩrĩte kũmenya?

19 Tunapopanda na kutia maji, ni lazima tutambue kwamba Yehova ndiye hukuza. (Soma 1 Wakorintho 3:6, 7.) Getahun, ndugu anayetumikia nchini Ethiopia, anasema hivi: “Kwa zaidi ya miaka 20, nilikuwa Shahidi wa Yehova pekee katika eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida. Lakini sasa kuna wahubiri 14. Kumi na tatu kati yao wamebatizwa, kutia ndani mke wangu na watoto wangu watatu. Kwa wastani, watu 32 huhudhuria mikutano.” Getahun anafurahi kwamba aliendelea kuhubiri huku akimngojea Yehova kwa subira awavute watu wenye mioyo minyoofu katika tengenezo Lake!—Yoh. 6:44.

20. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ tũkari ta antũ barĩa boonokagia mĩoyo?

20 Yehova anaona uhai wa kila mtu kuwa wenye thamani. Anatupatia pendeleo la kufanya kazi pamoja na Mwana wake ili kuwakusanya watu kutoka katika mataifa yote kabla ya mwisho wa mfumo huu kufika. (Hag. 2:7) Kazi yetu ya kuhubiri inaweza kulinganishwa na kazi ya uokoaji. Na sisi ni kama kikundi cha waokoaji waliotumwa kuokoa watu walionaswa kwenye mgodi. Ingawa huenda ni watu wachache tu watakaopatikana wakiwa hai, kazi inayofanywa na waokoaji hao wote ni ya muhimu. Hivyo ndiyo ilivyo kwa kazi yetu ya kuhubiri. Hatujui ni watu wangapi watakaookolewa kutoka katika mfumo huu wa Shetani. Lakini Yehova anaweza kumtumia yeyote kati yetu awasaidie. Andreas, anayeishi nchini Bolivia, anasema hivi: “Ninaona kila mtu anayejifunza kweli za Biblia na kubatizwa kuwa matokeo ya jitihada za watu wengi.” Acheni sisi pia tudumishe mtazamo kama huo kuelekea huduma yetu. Tukifanya hivyo, Yehova atatubariki na huduma yetu itatupatia shangwe nyingi.

RWĨMBO 66 Tangaza Habari Njema

^ gic. 5 Tunaweza kudumishaje mtazamo unaofaa katika huduma hata ikiwa watu hawapatikani nyumbani au hawataki kusikiliza ujumbe wetu? Makala hii itatoa mapendekezo yanayoweza kutusaidia kudumisha mtazamo unaofaa.

^ gic. 7 Wahubiri wanapofanya aina mbalimbali za utumishi zinazozungumziwa kwenye makala hii, wanapaswa kuzingatia sheria zinazolinda taarifa za kibinafsi zinazotumiwa.

^ gic. 60 MAELEZO YA PICHA Ukurasa wa 16-17 (kutoka juu kwenda chini): Mume na mke wakihubiri katika eneo ambalo si rahisi kuwapata watu nyumbani. Mwenye nyumba wa kwanza yuko kazini, wa pili yuko hospitalini, na wa tatu anafanya ununuzi. Wanakutana na mwenye nyumba wa kwanza kwa kumtembelea baadaye siku hiyo. Wanakutana na wa pili wanaposhiriki katika mahubiri ya hadharani karibu na hospitali. Na mwenye nyumba wa tatu wanampata kwa kumpigia simu.