Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 37

“Nkainainia Mĩgongo Yonthe”

“Nkainainia Mĩgongo Yonthe”

“Ningĩ nkainainia mĩgongo yonthe mwanka mĩthithũ yaao ĩreetwe gũkũ.”​—HAG. 2:7 KIMERU BIBLE 2010.

RWĨMBO 24 Njooni Kwenye Mlima wa Yehova

MUHTASARI *

1-2. Nĩ kwinainua kũrĩkũ kwa ngerekano kweranĩri kwa ĩgiita rĩetũ?

“NDANI ya dakika chache, maduka na majengo ya zamani yalianza kuporomoka.” “Kila mahali watu walikuwa wamechanganyikiwa . . . Watu wengi walisema kwamba mtikisiko ulikuwa wa dakika mbili hivi. Lakini kwangu, ulionekana kana kwamba ni milele.” Hayo ni maelezo ya baadhi ya watu waliookoka tetemeko la ardhi lililopiga nchi ya Nepal mwaka wa 2015. Ikiwa ungejionea tukio kama hilo lenye kutisha, usingelisahau kwa urahisi.

2 Hata hivyo, katika kipindi hiki cha wakati, kuna mtikisiko wa aina nyingine ambao hauhusishi tu jiji au nchi moja. Badala yake, unahusisha mataifa yote, na umekuwa ukiendelea kwa miaka mingi. Kutikiswa huko kulitabiriwa na nabii Hagai. Aliandika hivi: “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Kwa mara nyingine tena—baada ya muda mfupi—nitatikisa mbingu na dunia na bahari na nchi kavu.’”​—Hag. 2:6.

3. Nĩatĩa kwinainua kũũ kwa ngerekano tĩ ta kwinainua kwa nthĩgũrũ kungwa?

3 Mtikisiko ambao Hagai anauelezea si kama tetemeko halisi, ambalo husababisha tu uharibifu. Badala yake, mtikisiko huo unaleta matokeo mazuri. Yehova mwenyewe anatuambia hivi: “Nitayatikisa mataifa yote, na vitu vyenye thamani vya mataifa yote vitaingia katika nyumba hii; nami nitaijaza nyumba hii utukufu.” (Hag. 2:7) Unabii huu ulimaanisha nini kwa wale walioishi wakati wa Hagai? Na unatuhusuje sisi leo? Tutazungumzia majibu ya maswali hayo na pia tutajifunza jinsi tunavyoweza kushiriki katika kazi ya kuyatikisa mataifa leo.

NTŨMWA YA GWĨKĨRA INYA YA NTUKŨNE CIA HAGAI

4. Nĩkĩ Jehova aatũmĩre kĩroria Hagai kĩrĩ antũ baawe?

4 Yehova alimpa nabii Hagai kazi muhimu ya kufanya. Fikiria mambo yaliyotokea kabla ya hapo. Inaelekea Hagai alikuwa miongoni mwa wale waliorudi Yerusalemu kutoka uhamishoni Babiloni, mwaka wa 537 K.W.K. Mara tu walipowasili Yerusalemu, waabudu hao waaminifu walijenga msingi wa nyumba ya Yehova, au hekalu. (Ezra 3:8, 10) Lakini baada ya muda mfupi, hali yenye kuhuzunisha ilijitokeza. Walivunjika moyo na kuacha kazi ya ujenzi kwa sababu ya upinzani. (Ezra 4:4; Hag. 1:1, 2) Hivyo, mwaka wa 520 K.W.K., Yehova alimwagiza Hagai awasaidie Wayahudi hao warudie bidii yao na kuwachochea wakamilishe ujenzi wa hekalu. *​—Ezra 6:14, 15.

5. Nĩkĩ ntũmwa ya Hagai no mwanka nĩ yaere antũ ba Mũrungu ũrikithia?

5 Ujumbe wa Hagai ulikusudiwa kuimarisha imani ya Wayahudi katika Yehova. Kwa ujasiri, nabii huyo aliwaambia hivi Wayahudi waliokuwa wamevunjika moyo: “‘Nanyi watu wote wa nchi, jipeni moyo,’ asema Yehova, ‘na mfanye kazi. Kwa maana niko pamoja nanyi,’ asema Yehova wa majeshi.” (Hag. 2:4) Bila shaka maneno “Yehova wa majeshi” yaliwapa uhakika. Yehova ana jeshi kubwa la malaika shujaa walio chini ya amri yake, hivyo Wayahudi hao walihitaji kumtegemea yeye ili wafanikiwe.

6. Kwinainua kũrĩa kweranĩrwe nĩ Hagai kũrĩngĩĩthĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ?

6 Yehova alimwongoza Hagai awaeleze Wayahudi kwamba kwa njia ya mfano, angeyatikisa mataifa yote. Ufunuo huo uliwahakikishia wajenzi hao waliovunjika moyo kwamba Yehova angeitikisa Uajemi, serikali kuu ya ulimwengu iliyotawala mataifa mengi wakati huo. Kutikiswa huko kungekuwa na matokeo gani? Kwanza, watu wa Mungu wangekamilisha ujenzi wa hekalu. Kisha, hata watu ambao hawakuwa Wayahudi wangejiunga nao kumwabudu Yehova katika hekalu lililojengwa upya. Ni lazima ujumbe huo ulikuwa wenye kutia moyo sana kwa watu wa Mungu!​—Zek. 8:9.

NGŨGĨ ĨRĨA ĨKWINAINIA NTHĨGŨRŨ NAARUA

Je unashiriki kikamili katika kazi ya kutikisa mataifa inayofanywa leo? (Tazama fungu la 7 na 8) *

7. Nĩ ngũgĩ ĩrĩkũ ya kwinainia tũkũgwata mbaru naarua? Taarĩĩria.

7 Unabii wa Hagai unatuhusuje leo? Kwa mara nyingine tena Yehova anayatikisa mataifa yote, na wakati huu sisi tunahusika. Fikiria ukweli huu: Mwaka wa 1914, Yehova alimweka rasmi Yesu Kristo kuwa Mfalme wa Ufalme Wake wa mbinguni. (Zab. 2:6) Kusimamishwa kwa Ufalme huo kulikuwa habari mbaya kwa watawala wa ulimwengu. Kulimaanisha kwamba “nyakati zilizowekwa za mataifa”—kipindi ambacho hakikuwa na mtawala aliyemwakilisha moja kwa moja Yehova—zilikuwa zimetimizwa, au kufikia mwisho wake. (Luka 21:24) Kwa sababu hiyo, hasa kuanzia mwaka wa 1919, watu wa Yehova wamekuwa wakimwambia kila mtu kwamba Ufalme wa Mungu ndio tumaini pekee la wanadamu. Kazi hii ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” imetikisa ulimwengu mzima.​—Mt. 24:14.

8. Kũringana na Zaburi 2:1-3, nĩatĩa mĩgongo ĩmingĩ ĩtĩkĩrĩĩtie ntũmwa yeetũ?

8 Watu wameitikiaje ujumbe huo? Watu wengi wameukataa. (Soma Zaburi 2:1-3.) Mataifa yamekuwa na msukosuko. Yamekataa kumkubali Mtawala ambaye amewekwa rasmi na Yehova. Hawaoni ujumbe wa Ufalme tunaohubiri kuwa “habari njema.” Isitoshe, baadhi ya serikali zimepiga marufuku kazi ya kuhubiri! Hata ingawa watawala wengi wa mataifa hayo wanadai wanamtumikia Mungu, hawataki kuachia mamlaka na nguvu walizo nazo. Hivyo, kama tu watawala katika siku za Yesu, wale wanaotawala leo wanampinga Mtiwa-Mafuta wa Yehova kwa kuwashambulia wafuasi wake washikamanifu.​—Mdo. 4:25-28.

9. Nĩatĩa Jehova athithagia rĩrĩa mĩgongo ĩkũrega ntũmwa ya Ũnene?

9 Yehova anatendaje mataifa yanapokataa ujumbe wa Ufalme? Zaburi 2:10-12 inajibu hivi: “Basi sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu; kubalini kurekebishwa, enyi waamuzi wa dunia. Mtumikieni Yehova kwa woga, na mshangilie mkitetemeka. Mheshimuni mwana, la sivyo Mungu atawaka hasira nanyi mtaangamia kutoka njiani, kwa maana hasira Yake huwaka upesi. Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia Yeye.” Kwa fadhili Yehova anawapa watu hao wanaompinga fursa ya kufanya uamuzi sahihi. Bado wanaweza kubadili maoni yao na kuukubali Ufalme wa Yehova. Hata hivyo, wakati uliobaki umepungua. Tunaishi katika “siku za mwisho” za mfumo huu wa mambo. (2 Tim. 3:1; Isa. 61:2) Sasa kuliko wakati mwingine wowote, ni muhimu watu waijue kweli na kuchagua kumtumikia Yehova.

MAUMĨĨRA JAMEEGA JA KWINAINUA

10. Nĩ maumĩĩra jarĩkũ jameega ja ngũgĩ ya kwinainua jagũtaarĩrua kĩrĩ Hagai 2:7-9?

10 Baadhi ya watu wanaitikia vizuri kutikiswa kwa mfano kulikotabiriwa na Hagai. Hagai anatuambia kwamba baada ya kutikiswa kwa mataifa “vitu vyenye thamani [watu wenye mioyo minyoofu] vya mataifa yote vitaingia” ili kumwabudu Yehova. * (Soma Hagai 2:7-9.) Isaya, na pia Mika, walitabiri kwamba hali kama hiyo ingetokea “katika siku za mwisho.”—Isa. 2:2-4, maelezo ya chini; Mika 4:1, 2, maelezo ya chini.

11. Nĩatĩa mũtaana-o-baaba ũmwe aathithĩrie akwigua rĩa mbere ntũmwa ya Ũnene?

11 Fikiria jinsi ujumbe huo wenye kusisimua ulivyomchochea Ken, ndugu anayetumikia kwenye makao yetu makuu ya ulimwenguni pote. Bado anakumbuka vizuri aliposikia kwa mara ya kwanza ujumbe wa Ufalme miaka 40 hivi iliyopita. Ken anasema hivi: “Niliposikia kwa mara ya kwanza kweli kutoka katika Neno la Mungu, nilifurahi kujifunza kwamba tunaishi katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo. Nilitambua kwamba ili nipate kibali cha Mungu na kupata uzima wa milele, nilipaswa kuukimbia ulimwengu huu usiotegemeka na kusimama imara upande wa Yehova. Nilisali na kufanya hivyo mara moja. Niliachana na ulimwengu na kukimbilia usalama katika Ufalme wa Mungu ambao hauwezi kutikiswa.”

12. Nĩatĩa kĩũrũ kĩa Jehova kĩa gĩkĩrundu kĩũjũrĩtue ũkumio ntukũne iji cia mũthia?

12 Ni wazi kwamba Yehova amekuwa akiwabariki watu wake. Katika siku hizi za mwisho, tumeona ongezeko kubwa la idadi ya wale wanaomwabudu. Mwaka wa 1914 tulikuwa elfu chache tu. Sasa kuna zaidi ya watu milioni nane wanaomwabudu Mungu, na mamilioni zaidi wanajiunga nasi kila mwaka kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Kwa njia hiyo, nyua za kidunia za hekalu la kiroho la Yehova, yaani, mpango wake wa ibada safi​—zimejazwa “vitu vyenye thamani vya mataifa yote.” Jina la Yehova pia limetukuzwa kwa sababu ya mabadiliko ambayo watu hao wanafanya wanapovaa utu mpya.​—Efe. 4:22-24.

Watu wa Mungu ulimwenguni pote wameshiriki kwa shangwe katika kazi ya kuwatolea wengine ushahidi kuhusu Ufalme wa Mungu (Tazama fungu la 13))

13. Nĩ mororia jarĩkũ jangĩ jakũũjũrua tontũ bwa kwongereka kwa athathayia ba Jehova? (Tega mbica karatacine ka mbere.)

13 Matukio hayo yenye kusisimua yametimiza unabii mwingine kama ule unaopatikana kwenye Isaya sura ya 60. Mstari wa 22 wa sura hiyo unasema hivi: “Mdogo atakuwa elfu na mnyonge atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaliharakisha jambo hilo kwa wakati wake.” Kwa sababu ya kumiminika kwa watu kwenye ibada ya kweli, jambo fulani la pekee hutukia. ‘Watu hao wenye thamani’ wanakuja na ustadi na uwezo mbalimbali, pamoja na roho ya utayari ili kujiunga katika kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme.” Matokeo yamekuwa kama tu Isaya anavyoeleza kwamba “maziwa ya mataifa” yanatumiwa na watu wa Yehova. (Isa. 60:5, 16) Kwa msaada wa wanaume na wanawake hao wenye thamani, kazi ya kuhubiri inafanywa katika nchi 240 na machapisho yanapatikana katika lugha zaidi ya 1,000.

KAGIITA GA KŨTHITHIA ĨTUA

14. Nĩ ĩtua rĩrĩkũ antũ no mwanka barĩtue nandĩ?

14 Katika kipindi hiki cha siku za mwisho, kutikiswa kwa mataifa kunawalazimisha watu wafanye uamuzi. Je, wataunga mkono Ufalme wa Mungu, au wataweka tumaini lao katika serikali za ulimwengu huu? Huo ni uamuzi ambao kila mtu atahitaji kufanya. Ingawa watu wa Yehova wanatii sheria za serikali za nchi wanazoishi, hawaungi mkono kabisa upande wowote inapohusu siasa za ulimwengu huu. (Rom. 13:1-7) Wanajua kwamba Ufalme ndio suluhisho pekee la kweli kwa matatizo ya wanadamu. Ufalme huo si sehemu ya ulimwengu huu.​—Yoh. 18:36, 37.

15. Nĩ kĩgerio kĩrĩkũ gĩkĩnene kĩa wĩtĩkĩkua gĩgũtaarĩĩrua kĩrĩ iuku rĩa Kũgwũrĩrwa?

15 Kitabu cha Ufunuo kinatuambia kwamba ushikamanifu wa watu wa Mungu utajaribiwa katika siku za mwisho. Kipindi hicho cha majaribu kitakuwa na upinzani na mateso makali. Serikali za ulimwengu huu zitataka tuziabudu na zitawatesa wale wanaokataa kuziunga mkono. (Ufu. 13:12, 15) Serikali hizo “[zitawalazimisha] watu wote—wadogo kwa wakubwa, matajiri kwa maskini, walio huru kwa watumwa—ili wote watiwe alama kwenye mkono wao wa kulia au kwenye paji la uso wao.” (Ufu. 13:16) Katika nyakati za kale, watumwa waliwekwa alama ili kuonyesha yule aliyewamiliki. Vivyo hivyo, katika siku zetu wote watatarajiwa kuwa na alama ya mfano kwenye mkono wao au paji la uso wao. Kupitia mawazo na matendo yao wataonyesha kwamba wao ni mali ya serikali hizo na wanaunga mkono mifumo hiyo ya kisiasa.

16. Nĩkĩ kũrikia wĩtĩkĩkua bwetũ kĩrĩ Jehova kũrĩ kwa bata nandĩ?

16 Je, tutakubali kutiwa alama hiyo ya mfano na kuunga mkono serikali hizo? Wale watakaokataa kupokea alama hiyo watakabili hali ngumu na hatari. Kitabu cha Ufunuo kinaendelea kusema hivi: “Yeyote asiweze kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na ile alama.” (Ufu. 13:17) Lakini watu wa Mungu wanajua kile ambacho Mungu atawafanya wale watakaokuwa na alama iliyotajwa kwenye Ufunuo 14:9, 10. Badala ya kukubali kutiwa alama hiyo, wao wataandika kwenye mkono wao, “Mali ya Yehova.” (Isa. 44:5) Sasa ni wakati wa kuhakikisha kwamba ushikamanifu wetu kwa Yehova ni imara. Ikiwa ndivyo, Yehova atafurahi kusema kwamba sisi ni mali yake!

KWINAINUA KWA MŨTHIA

17. Nĩmbi tũkũbatara kũriikana biegie weteeri bwa Jehova?

17 Yehova ameonyesha subira kubwa katika siku hizi za mwisho. Hataki mtu yeyote aangamizwe. (2 Pet. 3:9) Amewapatia watu wote fursa ya kutubu na kufanya uamuzi sahihi. Lakini subira yake ina mipaka. Wale wanaokataa fursa hii, watajikuta katika hali sawa na ile ya Farao katika siku za Musa. Yehova alimwambia hivi Farao: “Kufikia sasa ningekuwa nimeunyoosha mkono wangu kwa nguvu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo kali sana, nawe ungekuwa umefutiliwa mbali kutoka duniani. Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii hasa: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.” (Kut. 9:15, 16) Mwishowe, mataifa yote yatalazimika kujua kwamba Yehova ndiye Mungu pekee wa kweli. (Eze. 38:23) Jambo hili litatukia jinsi gani?

18. (a) Nĩ kwinainua kũrĩkũ kũngĩ gũgũtaarĩrua kĩrĩ Hagai 2:6, 20-22? (b) Nĩatĩa tũkũmenya atĩ biugo bia Hagai bikethĩrwa na kũũjũrua kũngĩ igiita rĩĩjĩte?

18 Karne nyingi baada ya siku za Hagai, mtume Paulo aliongozwa na Mungu kuonyesha kwamba maneno yanayopatikana kwenye Hagai 2:6, 20-22 yangekuwa na utimizo mwingine wakati ujao. (Soma.) Paulo aliandika hivi: “Sasa ameahidi: ‘Nitatikisa kwa mara nyingine tena, si dunia tu bali pia mbingu.’ Sasa maneno ‘kwa mara nyingine tena’ yanaonyesha kuondolewa kwa vitu vinavyotikiswa, vitu vilivyotengenezwa, ili vitu ambavyo havitikiswi vibaki.” (Ebr. 12:26, 27) Tofauti na kutikiswa kunakotajwa kwenye Hagai 2:7, kutikiswa kunakotajwa na Paulo kutamaanisha uharibifu wa milele kwa wale ambao kama Farao, wanakataa kutambua haki ya Yehova ya kutawala.

19. Nĩmbi gĩtiinainua, na nĩatĩa tũkũmenya?

19 Ni kitu gani ambacho hakitatikiswa, au kuondolewa? Paulo aliendelea kusema hivi: “Kwa kuwa tutapokea Ufalme usioweza kutikiswa, acheni tuendelee kupokea fadhili zisizostahiliwa, ambazo zitatuwezesha kumtolea Mungu utumishi mtakatifu kwa njia inayokubalika, kwa kumwogopa Mungu na kumheshimu.” (Ebr. 12:28) Naam, baada ya kutikiswa huko kwa mara ya mwisho na vumbi kutulia, ni Ufalme wa Mungu pekee ambao hautatikiswa. Bado Ufalme huo utasimama imara mahali pake!​—Zab. 110:5, 6; Dan. 2:44.

20. No mwanka antũ bathithie ĩtua rĩrĩkũ, na nĩatĩa tũũmba kũbatethia?

20 Hakuna muda wa kupoteza! Ni lazima watu wachague: Je, wataendelea kuunga mkono njia ya maisha inayoendelezwa na ulimwengu huu, ambayo itaongoza kwenye uharibifu, au je, watajitahidi kupatanisha maisha yao na mapenzi ya Mungu, na hivyo kupata uzima wa milele? (Ebr. 12:25) Kupitia kazi yetu ya kuhubiri, tunaweza kuwasaidia watu waamue watachukua msimamo gani inapohusu swala hili muhimu. Acheni tuwasaidie watu wengi zaidi wenye thamani, wachukue msimamo upande wa Ufalme wa Mungu. Na tuendelee kukumbuka maneno haya ya Yesu, Bwana wetu: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mt. 24:14.

RWĨMBO 40 Sisi Ni wa Nani?

^ gic. 5 Makala hii itazungumzia uelewaji uliorekebishwa wa Hagai 2:7. Tutajifunza jinsi tunavyoweza kushiriki katika kazi yenye kusisimua inayotikisa mataifa yote. Kazi hii ya kutikisa mataifa ina matokeo mawili; baadhi ya watu wanaitikia vizuri na wengine hawaitikii vizuri.

^ gic. 4 Tunajua kwamba kazi ya Hagai ilifanikiwa kwa sababu ujenzi wa hekalu ulikamilishwa mwaka wa 515 K.W.K.

^ gic. 10 Huu ni uelewaji uliorekebishwa. Nyakati zilizopita tulisema kwamba kuvutwa kwa watu wenye mioyo minyoofu kwa Yehova hakukusababishwa na kutikiswa kwa mataifa yote. Tazama “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 2006.

^ gic. 63 MAELEZO YA PICHA: Hagai aliwahimiza watu wa Mungu wawe na bidii katika kujenga upya hekalu; watu wa Mungu katika siku zetu wametangaza kwa bidii ujumbe wa Mungu. Wenzi wa ndoa wakihubiri ujumbe kuhusu kutikiswa kwa mara ya mwisho kunakokuja.