Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 40

O ta Petero, Kinya Gwe Womba Kũũmĩĩria

O ta Petero, Kinya Gwe Womba Kũũmĩĩria

“Tigana nani Mwathani; untu ndi muntu wa meeyia.”—LUKA 5:8.

RWĨMBO 38 Atakupa Nguvu

MUHTASARI a

1. Nĩatĩa Petero aathithĩrie arĩkwona kĩama kĩrĩa kĩaringĩrwe kĩa kũgwatia makũyũ jamaingĩ?

 PETRO alikuwa amejaribu kuvua samaki usiku kucha lakini hakupata chochote. Kwa kushangaza, Yesu alimwambia hivi: “Peleka mashua mahali penye kina, kisha mshushe nyavu zenu, mvue samaki.” (Luka 5:4) Petro alitilia shaka kama angevua samaki, lakini alifanya kama alivyoagizwa. Baada ya kushusha nyavu, zilianza kukatika kwa sababu ya uzito wa samaki. Baada ya kutambua kwamba walikuwa wamejionea muujiza, Petro na wale waliokuwa pamoja naye “walishangazwa sana.” Petro akapaza sauti hivi: “Bwana ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi.” (Luka 5:​6-9) Inaonekana Petro alihisi kwamba hakustahili kuwa pamoja na Yesu.

2. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi kĩrĩ tuĩ gũcũnkũũna ngerekano ya Petero?

2 Petro alikuwa sahihi—alikuwa “mtu mwenye dhambi.” Maandiko yanaonyesha kwamba wakati mwingine alisema na kufanya mambo ambayo alijutia baadaye. Je, wakati mwingine unahisi kama Petro? Je, unapambana kushinda udhaifu fulani ulio nao ambao umepambana nao kwa muda mrefu? Ikiwa ndivyo, unaweza kutiwa moyo kwa kujifunza kuhusu mfano wa Petro. Kwa nini? Fikiria jambo hili: Ingekuwa rahisi kwa Yehova kuhakikisha kwamba makosa ya Petro hayaandikwi katika Biblia. Hata hivyo, yaliandikwa kwa mwongozo wa roho takatifu ili tujifunze kutokana nayo. (2 Tim. 3:​16, 17) Mambo tunayojifunza kutokana na mwanamume huyo aliyekuwa na udhaifu na hisia kama zetu yanaweza kutusaidia kuelewa kwamba Yehova hatarajii tuwe wakamilifu. Anataka tuendelee kuwa waaminifu—tuendelee kujitahidi—licha ya udhaifu wetu.

3. Nĩkĩ tũtĩbuĩrĩte gũkua nkoro?

3 Kwa nini ni muhimu kujitahidi kuendelea kuwa waaminifu? Kwa kawaida, ukijitahidi kufanya jambo fulani tena na tena, mwishowe unakuwa na uzoefu. Kwa mfano: Mwanamuziki anaweza kutumia miaka mingi ili kujizoeza kutumia vifaa vyake vya muziki. Katika kipindi hicho, huenda akafanya makosa mengi, lakini akiendelea kufanya mazoezi ataboresha uwezo wake. Hata anapokuwa mwanamuziki mwenye ustadi, huenda nyakati fulani akafanya makosa. Hata hivyo, hakati tamaa. Anaendelea kuboresha uwezo wake. Vivyo hivyo, hata tunapohisi kwamba tumeshinda udhaifu fulani huenda tukafanya makosa tena. Lakini bado tunaendelea kujitahidi kufikia lengo letu. Sisi sote husema au kufanya mambo ambayo baadaye tunajutia; hata hivyo, ikiwa hatutakata tamaa, Yehova atatusaidia tuendelee kusonga mbele. (1 Pet. 5:10) Acheni tuchunguze jinsi Petro alivyojitahidi kuendelea kuwa mwaminifu. Huruma ambayo Yesu alimwonyesha licha ya makosa yake inaweza kutuchochea tuendelee kumtumikia Yehova.

MANTŨ JAMOOMŨ NA ITHARIMO BIRĨA PETERO OONEERE

Ungetendaje ikiwa ungepitia hali kama ya Petro? (Tazama fungu la 4)

4. O ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Luka 5:​5-10, nĩ atĩa Petero ataarĩĩrie bũmwegie, ĩndĩ nĩ ũntũ bũrĩkũ Jesũ aamũrikĩĩthĩrie?

4 Maandiko hayasemi kwa nini Petro alijifafanua kuwa “mtu mwenye dhambi” wala hayataji dhambi alizokuwa akizungumzia. (Soma Luka 5:​5-10.) Lakini huenda alifanya baadhi ya makosa mazito. Yesu alitambua kwamba Petro aliogopa, labda ni kwa sababu Petro alihisi kwamba hastahili. Pia, Yesu alijua kwamba Petro angeendelea kuwa mwaminifu. Basi, kwa fadhili Yesu alimwambia Petro ‘aache kuogopa.’ Uhakika ambao Yesu alimwonyesha Petro ulibadili maisha yake. Baadaye, Petro na Andrea, ndugu yake, waliacha biashara yao ya kuvua samaki na wakajiunga na Yesu katika huduma yake, uamuzi ambao uliwaletea baraka nyingi.—Marko 1:​16-18.

5. Nĩ itharimo bĩrĩkũ Petero ooneere arĩgũcinda ũguaa bwawe, na arĩgwĩtĩkĩĩria kũthingata Jesũ?

5 Petro alijionea mambo mengi yenye kusisimua akiwa mfuasi wa Kristo. Alijionea Yesu akiponya wagonjwa, akifukuza roho waovu, na hata kuwafufua wafu. b (Mt. 8:​14-17; Marko 5:​37, 41, 42) Pia, Petro alijionea maono ya utukufu ambao Yesu angekuwa nao katika Ufalme wa Mungu, Petro hakusahau kamwe tukio hilo. (Marko 9:​1-8; 2 Pet. 1:​16-18) Petro aliona mambo ambayo hakutarajia kuona. Kwa kweli alifurahi sana kwamba hakuruhusu hisia zisizofaa kujielekea zimzuie kupata baraka hizo!

6. Rĩ, Petero neka aacindĩre ũguaa bwawe o rĩo? Taarĩĩria.

6 Licha ya mambo aliyokuwa ameona na kusikia, bado Petro alipambana na udhaifu wake mbalimbali. Fikiria mifano michache. Yesu alipoeleza jinsi ambavyo angeteseka na kufa ili kutimiza unabii wa Biblia, Petro alimkemea. (Marko 8:​31-33) Petro na wale mitume wengine walibishana tena na tena kuhusu yule aliyekuwa mkuu zaidi kati yao. (Marko 9:​33, 34) Usiku wa mwisho kabla ya kifo cha Yesu, Petro alimshambulia mwanamume fulani na kumkata sikio. (Yoh. 18:10) Usiku huohuo Petro alilemewa na woga na mara tatu akakana kwamba hamjui Yesu, rafiki yake. (Marko 14:​66-72) Baada ya hapo Petro alilia kwa uchungu.—Mt. 26:75.

7. Nĩ kaanya karĩkũ Petero aaerwe nyuma ya kũrĩũkua kwa Jesũ?

7 Yesu hakumwacha mtume huyo aliyekuwa amevunjika moyo sana. Baada ya Yesu kufufuliwa, alimpa Petro fursa ya kuonyesha kwamba bado anampenda. Yesu alimwalika Petro awe mchungaji mnyenyekevu wa kondoo wake. (Yoh. 21:​15-17) Petro aliitikia kwa njia nzuri. Alikuwa huko Yerusalemu siku ya Pentekoste na alikuwa miongoni mwa Wakristo wa kwanza kutiwa mafuta kwa roho takatifu.  

8. Nĩ ĩatia rĩrĩkũ rĩĩrĩto Petero aathithĩrie narĩa Antiokia?

8 Hata baada ya kuwa Mkristo aliyetiwa mafuta, bado Petro alipambana na udhaifu wake mbalimbali. Mwaka wa 36 W.K., Petro alikuwepo wakati Kornelio, Mtu wa Mataifa asiyetahiriwa, alipotiwa mafuta kwa roho takatifu, jambo lililothibitisha wazi kwamba “Mungu hana ubaguzi” na kwamba watu wa mataifa wangekuwa sehemu ya kutaniko la Kikristo. (Mdo. 10:​34, 44, 45) Baada ya hapo, Petro alijihisi huru kula chakula pamoja na Watu wa Mataifa, jambo ambalo hangeweza kufanya kamwe hapo awali. (Gal. 2:12) Hata hivyo, baadhi ya Wakristo Wayahudi walihisi kwamba Wayahudi na Watu wa Mataifa hawapaswi kula pamoja. Baadhi ya watu waliokuwa na maoni hayo walipokuja huko Antiokia, Petro aliacha kula pamoja na ndugu zake waliokuwa Watu wa Mataifa, inawezekana ni kwa sababu aliogopa kuwakasirisha Wakristo Wayahudi. Mtume Paulo alipoona unafiki huo alimkemea Petro hadharani. (Gal. 2:​13, 14) Licha ya kufanya kosa hilo, Petro aliendelea kuwa mwaminifu. Ni nini kilichomsaidia?

NĨMBI BIATETHERIE PETERO KŨŨMĨĨRIA?

9. Nĩatĩa Johana 6:​68, 69 ĩkwonania wĩtĩkĩkua bwa Petero?

9 Petro alikuwa mshikamanifu; hakuruhusu jambo lolote limzuie kuendelea kumfuata Yesu. Kwa mfano, pindi fulani alionyesha ushikamanifu wake Yesu aliposema jambo ambalo wanafunzi wake hawakuelewa. (Soma Yohana 6:​68, 69.) Bila kusubiri au kutafuta ufafanuzi, wengi waliacha kumfuata Yesu. Lakini Petro hakuacha. Alitambua kwamba Yesu tu ndiye aliyekuwa na “maneno ya uzima wa milele.”

Kwa nini uhakika ambao Yesu alikuwa nao katika Petro unakutia moyo? (Tazama fungu la 10)

10. Nĩatĩa Jesũ oonanĩrie atĩ ataarĩ na nkaanja na Petero? (Tega kinya mbica.)

10 Yesu hakumwacha Petro. Usiku wa mwisho wa uhai wake duniani, Yesu alijua kwamba Petro na wale mitume wengine wangemwacha. Ingawa hivyo, Yesu alikuwa na uhakika kwamba Petro angerudi na kuendelea kuwa mwaminifu. (Luka 22:​31, 32) Yesu alielewa kwamba “roho inataka, lakini mwili ni dhaifu.” (Marko 14:38) Hivyo, hata baada ya Petro kukana kwamba hamjui Yesu, Yesu hakumwacha mtume huyo. Baada ya kufufuliwa Yesu alimtokea Petro—inaonekana Petro alikuwa peke yake. (Marko 16:7; Luka 24:34; 1 Kor. 15:5) Hilo lilimwimarisha mtume huyo ambaye alikuwa amehuzunika sana!

11. Nĩatĩa Jesũ aarikĩthĩĩrie Petero atĩ Jehova akamwigĩka?

11 Yesu alimhakikishia Petro kwamba Yehova angemtegemeza. Yesu aliyefufuliwa alimsaidia Petro na mitume wenzake kuvua tena samaki kimuujiza. (Yoh. 21:​4-6) Bila shaka, muujiza huo ulimhakikishia Petro kwamba Yehova angemwandalia mahitaji yake ya kimwili. Labda mtume huyo alikumbuka maneno ya Yesu kwamba Yehova angewaandalia wale ambao wanaendelea “kuutafuta kwanza Ufalme.” (Mt. 6:33) Hilo lilimsaidia Petro kutanguliza huduma maishani badala ya kazi ya kuvua samaki. Alitoa ushahidi kwa ujasiri siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K., na kuwasaidia maelfu kukubali habari njema. (Mdo. 2:​14, 37-41) Baadaye, aliwasaidia Wasamaria na Watu wa Mataifa kuwa Wakristo. (Mdo. 8:​14-17; 10:​44-48) Bila shaka, Yehova alimtumia Petro kwa njia kubwa kuwasaidia watu wa kila namna wajiunge na kutaniko.

NĨMBI TŨKWIRITANA?

12. Tũkĩthũgaanagĩria ngerekano ya Petero, nĩmbi tũbuĩrĩte kũriikana kethĩra nĩtwĩthĩrĩtwe tũkĩrwa na gũtaũkĩrwa gwetũ?

12 Yehova anaweza kutusaidia kuendelea kuwa waaminifu. Huenda isiwe rahisi sikuzote hasa ikiwa tunapambana na udhaifu unaoendelea kwa muda mrefu. Nyakati nyingine, huenda udhaifu wetu ukaonekana kuwa mkubwa zaidi kuliko ule ambao Petro alikabili. Lakini Yehova anaweza kutupatia nguvu ili tusife moyo. (Zab. 94:​17-19) Kwa mfano, ndugu fulani alijihusisha na ngono za watu wa jinsia moja kwa miaka mingi kabla ya kujifunza kweli. Aliamua kuacha maisha hayo yaliyopotoka kimaadili. Hata hivyo, wakati mwingine alipambana na tamaa zisizofaa. Ni nini kilichomsaidia kuendelea kuwa mwaminifu? Anaeleza hivi: “Yehova ndiye anayetuimarisha.” Anaongezea hivi: “Kwa msaada wa roho ya Yehova . . . , nimejifunza kwamba ninaweza [kuendelea] kutembea kwenye njia ya kweli . . . Yehova ameendelea kunitumia na licha ya udhaifu wangu mbalimbali anaendelea kuniimarisha.”

Horst Henschel alianza utumishi wa wakati wote Januari 1, 1950. Je, unafikiri kwamba alijuta kutumia maisha yake kumtumikia Yehova? (Tazama fungu la 13 na 15) d

13. O ta ũrĩa Mathithio 4:​13, 29, 31 yonanĩĩtie, nĩatĩa tũũmba kũthingata ngerekano ya Petero? (Tega kinya mbica.)

13 Kama tulivyoona, Petro alifanya makosa mazito mara kadhaa kwa sababu aliwaogopa wanadamu. Lakini Petro alisali ili apate ujasiri, na akafaulu kuonyesha ujasiri. (Soma Matendo 4:​13, 29, 31.) Sisi pia tunaweza kushinda woga wetu. Fikiria jambo lililompata Horst, ndugu kijana aliyeishi katika Ujerumani ya Wanazi. Zaidi ya mara moja, alilemewa na mkazo shuleni na kusema “Heil Hitler!” (Hitler atukuzwe!) Badala ya kumkemea, wazazi wa Horst walisali pamoja naye na kumwomba Yehova ampe ujasiri. Kwa msaada wa wazazi wake na kumtegemea Yehova, mwishowe Horst alipata nguvu za kusimama imara. Baadaye alisema hivi: “Yehova hakuniacha kamwe.” c

14. Nĩatĩa akũrũ ba kĩũthũrano bomba gwĩkĩra inya barĩa baunĩki nkoro?

14 Yehova na Yesu hawatatuacha. Baada ya Petro kumkana Yesu alihitaji kufanya uamuzi muhimu. Je, angekata tamaa, au angejitahidi kuendelea kuwa mwanafunzi mwaminifu wa Kristo? Yesu alikuwa ametoa dua kwa Yehova kwamba imani ya Petro isidhoofike. Yesu alimwambia Petro kuhusu sala hiyo na akamhakikishia Petro kwamba baadaye angewaimarisha ndugu zake. (Luka 22:​31, 32) Bila shaka, Petro alitiwa moyo sana alipokumbuka maneno ya Yesu! Tunapohitaji kufanya uamuzi muhimu maishani, huenda Yehova akawatumia wachungaji wanaotujali kututia moyo ili tuendelee kuwa waaminifu. (Efe. 4:​8, 11) Paul ambaye ametumikia kwa muda mrefu akiwa mzee wa kutaniko hujitahidi kuwafariji wengine. Yeye huwaambia wale ambao wanakaribia kukata tamaa wakumbuke jinsi Yehova alivyowavuta kwenye kweli mwanzoni. Kisha anawahakikishia kwamba Yehova ni mwenye upendo mshikamanifu na hivyo hawezi kuwaacha. Anamalizia hivi: “Nimewaona watu wengi waliokuwa wamevunjika moyo wakiendelea kuwa waaminifu kwa msaada wa Yehova.”

15. Ngerekano ya Petero na ya Horst ĩrĩonania atĩa ũmma bwa Mathayo 6:33?

15 Kama vile Yehova alivyowaandalia mahitaji ya kimwili Petro na mitume wengine, atatuandalia mahitaji yetu ya kimwili ikiwa tutatanguliza huduma maishani. (Mt. 6:33) Baada ya Vita vya Pili vya Ulimwengu, Horst aliyetajwa awali, alifikiria kuhusu kufanya upainia. Hata hivyo, alikuwa maskini sana, na alitilia shaka ikiwa angeweza kujitegemeza na kuendelea na utumishi wa wakati wote. Angefanya nini? Aliamua kumjaribu Yehova, na hivyo akatumia juma zima katika huduma wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Mwishoni mwa juma hilo, alishangaa mwangalizi wa mzunguko alipompa bahasha iliyokuwa na kiasi fulani cha pesa lakini hakutaja yule aliyetoa zawadi hiyo. Ilikuwa na kiasi cha kutosha cha kumtegemeza katika utumishi wa upainia kwa miezi kadhaa. Horst aliona zawadi hiyo kuwa uhakikisho wa kwamba Yehova angemwandalia mahitaji yake. Alitanguliza kazi ya Ufalme katika maisha yake yote.—Mal. 3:10.

16. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi gũcũnkũũna ngerekano ya Petero na mantũ jarĩa aandĩkĩre?

16 Petro alifurahi kwamba Yesu hakuondoka na kumwacha, kama Petro alivyokuwa amemwambia afanye! Kristo aliendelea kumzoeza Petro ili awe mtume mwaminifu na mfano bora kwa Wakristo. Rekodi ya mazoezi hayo ina masomo mengi yenye thamani ambayo yanaweza kutunufaisha sisi sote. Petro alitaja baadhi ya masomo hayo na mengine mengi katika barua mbili zilizoongozwa na roho ambazo alituma kwenye makutaniko katika karne ya kwanza. Makala inayofuata itazungumzia baadhi ya mambo yaliyo kwenye barua hizo na jinsi tunavyoweza kuyatumia leo.

RWĨMBO 126 Uwe Macho, Simama Imara, Uwe na Nguvu

a Makala hii imekusudiwa kuwahakikishia wale wanaopambana na udhaifu fulani kwamba wanaweza kuushinda na kuendelea kuwa watumishi waaminifu wa Yehova.

b Maandiko mengi yaliyonukuliwa katika makala hii yanapatikana katika Kitabu cha Injili cha Marko. Inaonekana ni mambo aliyokuwa amesikia kutoka kwa Petro, ambaye alijionea matukio hayo yeye mwenyewe.

c Tazama simulizi la maisha la Horst Henschel, “Nilichochewa na Uaminifu-Mshikamanifu wa Familia Yangu kwa Mungu” katika Amkeni!, Februari 22, 1998.

d MAELEZO YA PICHA: Kama inavyoonyeshwa kwenye igizo, wazazi wa Horst Henschel walisali pamoja naye na kuimarisha azimio lake la kusimama imara.