Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 1

RWĨMBO 2 Jina Lako Ni Yehova

Eeni Jehova Ũkumio

Eeni Jehova Ũkumio

ĨANDĨKO RĨETŨ RĨA MWAKA JWA 2025: “Eeni Jehova ũkumio bũrĩa bwagĩrĩte riĩtwa rĩawe.”ZAB. 96:8, NWT.

JAMBO KUU

Kujifunza jinsi tunavyoweza kumpa Yehova utukufu anaostahili.

1. Nĩmbi antũ babaingĩ narua bagwĩka mbere?

 JE, UMETAMBUA kwamba watu wengi leo wanajikazia uangalifu kupita kiasi? Kwa mfano, baadhi ya watu hutumia muda mwingi sana kwenye mitandao ya kijamii wakijigamba na kuwaonyesha wengine mafanikio yao. Hata hivyo, leo, ni watu wachache wanaompa Yehova Mungu utukufu. Katika makala hii, tutazungumzia inamaanisha nini kumpa Yehova utukufu na ni nini kinachopaswa kutuchochea kufanya hivyo. Pia, tutajifunza jinsi tunavyoweza kumpa Mungu utukufu ambao anastahili na jinsi yeye mwenyewe atakavyolitukuza jina lake hivi karibuni.

KWAA JEHOVA ŨKUMIO NĨ KUUGA ATĨA?

2. Nĩatĩa Jehova oonanĩrie ũkumio bwawe Kĩrĩmene gĩa Sinai? (Tega kinya mbica karatacine ka mbere.)

2 Utukufu ni nini? Katika Biblia, neno “utukufu” linaweza kurejelea jambo lolote linalomfanya mtu awe mwenye kustaajabisha. Yehova alionyesha utukufu wake kwa njia ya pekee muda mfupi baada ya taifa la Israeli kuokolewa kutoka katika utumwa nchini Misri. Wazia tukio hilo: Mamilioni ya Waisraeli wanakusanyika chini ya Mlima Sinai ili kusikiliza kile ambacho Mungu wao angewaambia. Wingu zito linafunika mlima. Kisha, ghafla tetemeko kubwa la ardhi linatokea—inaelekea likiambatana na milipuko ya volkano—na linatetemesha ardhi mahali waliposimama huku radi, ngurumo, na sauti kubwa sana ya pembe ikisikika kotekote. (Kut. 19:​16-18; 24:17; Zab. 68:8) Wazia jinsi Waisraeli hao walivyostaajabishwa Yehova alipoonyesha utukufu wake kwa njia hiyo kubwa.

Katika Mlima Sinai, Yehova aliwaonyesha Waisraeli utukufu wake kwa njia kubwa (Tazama fungu la 2)


3. Kwaa Jehova ũkumio nĩ kuuga atĩa?

3 Lakini namna gani kuhusu wanadamu? Je, kweli tunaweza kumpa Yehova utukufu? Ndiyo, tunaweza. Njia moja tunayompa Yehova utukufu ni kwa kuwaeleza wengine kuhusu nguvu zake zenye kustaajabisha na sifa zake zenye kuvutia. Pia, tunampa Mungu utukufu tunapomwelekezea yeye sifa kwa mambo anayotusaidia kutimiza. (Isa. 26:12) Mfalme Daudi ni mfano wa pekee wa mtu aliyempa Yehova utukufu. Katika sala yake ambayo alitoa mbele ya kutaniko la Waisraeli, Daudi alimwambia Mungu hivi: “Ee Yehova, ukuu ni wako na nguvu na uzuri na fahari na utukufu, kwa maana kila kitu mbinguni na duniani ni chako.” Baada ya Daudi kumaliza sala yake, “kutaniko lote likamsifu Yehova.”—1 Nya. 29:​11, 20.

4. Nĩatĩa Jesũ aaere Jehova ũkumio?

4 Yesu alipokuwa duniani, alimtukuza Baba yake kwa kuwaeleza watu kwamba Yehova ndiye Chanzo cha miujiza yake. (Marko 5:​18-20) Pia, Yesu alimtukuza Yehova kupitia jinsi alivyomzungumzia Baba yake na jinsi alivyowatendea wengine. Pindi moja, Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi. Kati ya wale waliokuwa wakimsikiliza, kulikuwa na mwanamke ambaye alikuwa na roho mwovu kwa miaka 18. Roho huyo mwovu alisababisha mwili wake upindike na hivyo hangeweza kusimama wima. Hiyo ilikuwa hali yenye kutaabisha sana! Akichochewa na huruma, Yesu alimfuata mwanamke huyo na kumwambia hivi kwa wororo: “Mwanamke, umefunguliwa kutoka kwa udhaifu wako.” Kisha, akaweka mikono yake juu ya yule mwanamke na mara moja akanyooka na “kuanza kumtukuza Mungu.” Afya yake ikawa nzuri tena! (Luka 13:​10-13) Mwanamke huyo alikuwa na sababu nzuri za kumpa Yehova utukufu, na sisi pia tunazo.

NĨKĨ TWEJAGA JEHOVA ŨKUMIO?

5. Tũrĩna itũmi birĩkũ bia kwaa Jehova gĩtĩĩo?

5 Tunampa Yehova utukufu kwa sababu tunamheshimu sana. Tuna sababu nyingi za kumheshimu. Yehova ni Mweza-Yote; ana nguvu zisizo na mipaka. (Zab. 96:​4-7) Hekima yake nyingi inaonekana wazi katika vitu alivyoumba. Yeye ndiye Chanzo cha uhai wetu na anatupatia kila kitu tunachohitaji ili tuishi. (Ufu. 4:11) Yeye ni mshikamanifu. (Ufu. 15:4) Kila jambo analofanya linafanikiwa, na sikuzote anatimiza ahadi zake. (Yos. 23:14) Haishangazi kwamba Yeremia alisema hivi kumhusu Yehova: “Kati ya watu wote wenye hekima wa mataifa na kati ya falme zao zote, hakuna yeyote yule aliye kama wewe”! (Yer. 10:​6, 7) Kwa hakika, tuna sababu nzuri za kumheshimu Baba yetu wa mbinguni. Lakini Yehova anafanya mengi zaidi ya kustahili tu heshima yetu—anatuchochea tumpende pia.

6. Nĩkĩ twendete Jehova?

6 Tunampa Yehova utukufu kwa sababu tunampenda sana. Fikiria sifa kadhaa zinazotuchochea tumpende. Yeye ni mwenye rehema na huruma. (Zab. 103:13; Isa. 49:15) Ni mwenye hisia mwenzi; tunapoumia, yeye pia anaumia. (Zek. 2:8) Anafanya iwe rahisi kwetu kumkaribia akiwa Rafiki yetu. (Zab. 25:14; Mdo. 17:27) Na ni mnyenyekevu; Yeye “huinama chini ili atazame mbingu na dunia, akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini.” (Zab. 113:​6, 7) Hivyo basi, mtu anawezaje kukataa kumpa utukufu Mungu wetu mkuu?—Zab. 86:12.

7. Nĩ kaanya karĩkũ ka mwanya tũrĩ nako?

7 Tunampa Yehova utukufu kwa sababu tunataka wengine wamjue. Watu wengi hawajui ukweli kumhusu Yehova. Kwa nini? Kwa sababu Shetani amepofusha akili zao kwa kueneza uwongo mbaya kumhusu. (2 Kor. 4:4) Shetani amefanya watu waamini kwamba Yehova ni mwenye kulipiza kisasi, hajali, na anasababisha matatizo mengi yanayofanya watu wateseke. Lakini tunajua ukweli kumhusu Mungu wetu! Tuna fursa ya kuwasaidia watu wasahihishe maoni yao yasiyo ya kweli na hivyo kumpa Yehova utukufu. (Isa. 43:10) Zaburi ya 96 inakazia kumpa Yehova utukufu. Tunapochunguza baadhi ya maneno yaliyoongozwa na roho katika zaburi hiyo, fikiria kuhusu njia ambazo unaweza kumpa Yehova utukufu ambao kwa kweli anastahili.

NĨATĨA TŨŨMBA KWAA JEHOVA ŨKUMIO BŨRĨA AKŨBATARA?

8. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ tũũmba kwaa Jehova ũkumio? (Zaburi 96:1-3)

8 Soma Zaburi 96:​1-3. Tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia mambo ambayo tunasema kumhusu. Katika mistari hiyo, watu wa Yehova wanaalikwa ‘kumwimbia Yehova,’ ‘kulisifu jina lake,’ “kutangaza habari njema za wokovu wake,” na “kutangaza utukufu wake miongoni mwa mataifa.” Hizo ni njia ambazo tunaweza kumpa utukufu Baba yetu wa mbinguni kupitia mambo tunayosema. Wayahudi waaminifu na Wakristo wa karne ya kwanza hawakusita kuwaeleza wengine kuhusu mambo yote mazuri ambayo Yehova alikuwa amewafanyia na kutetea sifa yake. (Dan. 3:​16-18; Mdo. 4:29) Tunawezaje kufanya hivyo pia?

9-10. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya Angelena? (Tega kinya mbica.)

9 Fikiria kisa cha Angelena, a dada anayeishi nchini Marekani. Kwa ujasiri alitetea sifa ya Yehova katika kampuni aliyokuwa akifanya kazi. Akiwa mfanyakazi mpya, Angelena alialikwa kwenye mkutano ambao wafanyakazi wapya wa kampuni hiyo walipewa fursa ya kuwaeleza wafanyakazi wenzao kuhusu historia ya maisha yao. Angelena alipanga kuonyesha picha zinazoonyesha shangwe aliyo nayo akiwa Shahidi wa Yehova. Hata hivyo, kabla tu ya zamu yake kufika, mfanyakazi mwenzake alijitambulisha kwamba alilelewa na wazazi ambao ni Mashahidi wa Yehova. Alianza kudhihaki mambo ambayo tunaamini. Angelena anasema hivi: “Moyo wangu ulianza kudunda kwa kasi. Lakini nikajiambia hivi: ‘Je, nitaruhusu mtu huyu aseme uwongo kumhusu Yehova? Au je, nitamtetea Yehova?’”

10 Mfanyakazi mwenzake alipomaliza kujitambulisha, Angelena alitoa sala fupi, kimyakimya. Kisha, kwa fadhili akamwambia: “Malezi yangu yanafanana na yako. Mimi pia nililelewa na wazazi ambao ni Mashahidi wa Yehova, na bado mimi ni Shahidi wa Yehova hadi leo.” Ingawa hali hiyo ilimpa mkazo mkubwa, Angelena aliendelea kuwa mtulivu alipokuwa akionyesha picha zenye kugusa moyo za matukio ya kiroho ambayo alikuwa amehudhuria na kwa busara akatetea imani yake. (1 Pet. 3:15) Matokeo yalikuwaje? Kufikia wakati ambao Angelena alimaliza kuzungumza, yule mwanamume alikuwa mtulivu. Hata alikubali kwamba alikuwa na kumbukumbu nzuri za mambo aliyojionea aliposhirikiana na Mashahidi wa Yehova akiwa mtoto. Angelena anasema hivi: “Yehova anastahili kutetewa. Ni pendeleo kulitetea jina lake.” Sisi pia tuna pendeleo la kumsifu Yehova na kumpa utukufu hata wengine wanapomvunjia heshima.

Tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia mambo tunayosema, vitu vyetu vyenye thamani, na mwenendo wetu (Tazama fungu la 9-10) b


11. Kuuma karaaja, nĩ na njĩra ĩrĩkũ athathayia ba mma bethĩrĩtwe bakĩthingata ũritani bũrĩa bũrĩ kĩrĩ Zaburi 96:8?

11 Soma Zaburi 96:8. Tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia vitu vyetu vyenye thamani. Sikuzote waabudu wa kweli wamemheshimu Yehova kwa njia hiyo. (Met. 3:9) Kwa mfano, Waisraeli walitoa michango kwa ajili ya ujenzi na udumishaji wa hekalu. (2 Fal. 12:​4, 5; 1 Nya. 29:​3-9) Baadhi ya wanafunzi wa Kristo walimhudumia yeye na mitume wake “kwa mali zao.” (Luka 8:​1-3) Pia, Wakristo wa karne ya kwanza walitoa msaada kwa ajili ya ndugu na dada zao wa kiroho. (Mdo. 11:​27-29) Leo, sisi pia tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia michango yetu ya hiari.

12. Nĩatĩa mĩũthi yeetũ ĩretagĩra Jehova ũkumio? (Tega kinya mbica.)

12 Fikiria mfano mmoja unaoonyesha jinsi michango yetu inavyompa Yehova utukufu. Ripoti moja ya 2020 ilifafanua madhara ya ukame wa muda mrefu uliotokea nchini Zimbabwe. Mamilioni ya watu walikuwa karibu kufa njaa, kutia ndani dada anayeitwa Prisca. Licha ya ukame huo, Prisca aliendelea na ratiba yake ya kuhubiri kila Jumatano na Ijumaa, hata wakati wa majira ya kulima mashamba. Jirani zake walimdhihaki kwa sababu alienda utumishi badala ya kufanya kazi shambani, wakimwambia, “Utakufa njaa.” Sikuzote Prisca aliwajibu hivi kwa uhakika: “Yehova hajawahi kamwe kushindwa kuwatunza watumishi wake.” Baada ya muda mfupi alipokea msaada uliotolewa na tengenezo letu. Msaada huo ulipatikana kupitia michango yetu. Majirani wa Prisca walishangaa, na kumwambia hivi, “Mungu hajawahi kushindwa kukutunza, kwa hiyo tungependa kujifunza mengi zaidi kumhusu.” Majirani wake saba walianza kuhudhuria mikutano.

Tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia vitu vyetu vyenye thamani (Tazama fungu la 12) c


13. Nĩatĩa mĩtĩre yeetũ yũũmba kũretera Jehova ũkumio? (Zaburi 96:9)

13 Soma Zaburi 96:9. Tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia mwenendo wetu. Makuhani waliotumikia katika hekalu la Yehova walipaswa kuwa safi kimwili. (Kut. 40:​30-32) Hata hivyo, zaidi ya kuwa safi kimwili ni muhimu kuwa na mwenendo safi. (Zab. 24:​3, 4; 1 Pet. 1:​15, 16) Tunahitaji kujitahidi sana ili kuvua “utu wa zamani,” yaani, mitazamo na mazoea machafu, na kujivika “utu mpya,” yaani, kufikiri na kutenda kwa njia inayoonyesha kwamba tunamwiga Yehova na sifa zake nzuri. (Kol. 3:​9, 10) Kwa msaada wa Yehova, hata watu wenye maadili mapotovu sana na wakatili wanaweza kubadilika na kuvaa utu mpya.

14. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya Jack? (Tega kinya mbica.)

14 Fikiria mfano wa Jack, mwanamume mkatili na hatari ambaye jina lake la utani lilikuwa Roho Mwovu. Kwa sababu ya uhalifu wake, Jack alihukumiwa kifo. Hata hivyo, alipokuwa akisubiri hukumu hiyo itekelezwe, alikubali kujifunza Biblia pamoja na ndugu aliyetembelea gereza ambalo Jack alikuwa amefungwa. Licha ya malezi yake, Jack alivua utu wake wa zamani na baada ya muda akastahili kubatizwa. Jack alibadilika sana hivi kwamba siku ambayo alipaswa kuuawa, baadhi ya walinzi wa gereza walitokwa na machozi walipokuwa wakimuaga. Askari mmoja aliyekuwa akifanya kazi kwenye gereza hilo alisema hivi: “Mwanzoni Jack alikuwa mfungwa mbaya zaidi mahali hapa. Sasa ni miongoni mwa wafungwa bora zaidi.” Juma lililofuata baada ya Jack kuuawa, ndugu aliyerudi gerezani ili kuongoza mkutano wa kila juma alikutana na mfungwa ambaye alikuwa akihudhuria mkutano kwa mara ya kwanza. Ni nini kilichomchochea mfungwa huyo kuhudhuria? Alikuwa amevutiwa na jinsi Jack alivyobadili mwenendo wake na alitaka kujua mambo anayopaswa kufanya ili amwabudu Yehova. Ni wazi kwamba mwenendo wetu unaweza kumpa utukufu Baba yetu wa mbinguni!—1 Pet. 2:12.

Tunaweza kumpa Yehova utukufu kupitia mwenendo wetu (Tazama fungu la 14) d


NĨATĨA JEHOVA AGAKUMITHIA RIĨTWA RĨAWE ĨGIITA RĨTĨ KŨRAAJA?

15. Nĩatĩa Jehova agakumithia riĩtwa rĩawe na njĩra ĩnene, ĩgiita rĩtĩ kũraaja? (Zaburi 96:​10-13)

15 Soma Zaburi 96:​10-13. Mistari hii ya mwisho ya Zaburi ya 96 inamfafanua Yehova kuwa Hakimu na Mfalme mwadilifu. Yehova atalitukuzaje jina lake hivi karibuni? Kupitia hukumu zake. Hivi karibuni, atamwangamiza Babiloni Mkubwa kwa sababu ya kuliletea suto jina lake takatifu. (Ufu. 17:​5, 16; 19:​1, 2) Baadhi ya watu watakaojionea kuharibiwa kwa Babiloni Mkubwa huenda watajiunga nasi katika ibada ya kweli. Hatimaye, katika vita vya Har–​Magedoni, Yehova atauangamiza mfumo wote wa Shetani, na kuwaondoa wale wote wanaompinga na kukufuru jina lake, lakini atawaokoa wale wote wanaompenda na kumtii na wanaojivunia kumpa utukufu. (Marko 8:38; 2 The. 1:​6-10) Baada ya Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo na jaribu la mwisho, Yehova atakuwa amelitakasa jina lake kikamili. (Ufu. 20:​7-10) Wakati huo, “dunia itajaa ujuzi wa utukufu wa Yehova kama maji yanavyoifunika bahari.”—Hab. 2:14.

16. Nĩatĩa ũtuĩte kũthithia? (Tega kinya mbica.)

16 Kitakuwa kipindi chenye kusisimua sana wakati kila mtu aliye hai atampa Yehova utukufu ambao jina lake linastahili! Lakini hadi siku hiyo ifike, tunaweza kufanya sehemu yetu kwa kumpa Mungu wetu utukufu kila tunapopata fursa. Ili kukazia suala hilo muhimu, Baraza Linaloongoza limechagua Zaburi ya 96:8 kuwa andiko letu la mwaka wa 2025: Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.”

Hatimaye, kila mtu aliye hai atampa Yehova utukufu ambao jina lake linastahili! (Tazama fungu la 16)

RWĨMBO 12 Mungu Mkuu, Yehova

a Baadhi ya majina yamebadilishwa.

b MAELEZO YA PICHA: Igizo la simulizi la Angelena.

c MAELEZO YA PICHA: Igizo la simulizi la Prisca.

d MAELEZO YA PICHA: Igizo la simulizi la Jack.