Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 24

No Uume Mĩtegone ya Nkoma!

No Uume Mĩtegone ya Nkoma!

‘Uuma mũtegone jwa Nkoma.’—2 TIM. 2:26.

RWĨMBO 36 Tuulinde Moyo Wetu

MUHTASARI *

1. Nĩkĩ tũũmba kũgerekania Nkoma na mũthoogi?

LENGO la mwindaji ni moja tu—kumnasa au kumuua mnyama. Anaweza kutumia aina mbalimbali za mitego, kama tu mmoja wa wafariji wa uwongo wa Ayubu alivyosema. (Ayu. 18:8-10) Mwindaji anaweza kumshawishi jinsi gani mnyama aingie kwenye mtego wake? Anamchunguza mnyama huyo. Anaenda wapi? Mnyama huyo anavutiwa na nini? Anaweza kunaswa na mtego gani? Shetani ni kama mwindaji huyo. Anatuchunguza. Anaangalia tunapoenda na mambo tunayovutiwa nayo. Kisha, anaweka mtego ambao anatumaini utatunasa bila sisi kutambua. Hata hivyo, Biblia inatuhakikishia kwamba ikiwa tumenaswa na mtego tunaweza kutoka. Pia, inatufundisha jinsi tunavyoweza kuepuka kunaswa na mitego hiyo.

Kiburi na Pupa ni mitego miwili ya Shetani ambayo imethibitika kuwa na matokeo sana (Tazama fungu la 2) *

2. Nĩ mĩtego ĩrĩkũ Nkoma oombanĩte gũtumĩra?

2 Mitego miwili ya Shetani ambayo ina matokeo sana ni kiburi na pupa. * Kwa maelfu ya miaka, Shetani amefanikiwa kuwanasa watu kwa kutumia sifa hizo mbaya. Shetani ni kama mwindaji anayemshawishi ndege aingie kwenye mtego au kumnasa kwa wavu. (Zab. 91:3) Lakini si lazima tunaswe na Shetani. Kwa nini? Kwa sababu Yehova ametufunulia mbinu ambazo Shetani hutumia.—2 Kor. 2:11.

Tunaweza kujifunza kutokana na mifano ya kuonya na hivyo kuepuka au kutoka kwenye mitego ya Ibilisi (Tazama fungu la 3) *

3. Nĩkĩ Jehova etĩkĩĩrĩĩrie ngerekano imwe ciandĩkwa Bibiriene?

3 Njia moja ambayo Yehova anatuonya kuhusu kiburi na pupa, ni kwa kututia moyo tujifunze kutokana na masimulizi halisi ya maisha. Katika mifano tutakayochunguza, ona kwamba Shetani alifaulu kuwanasa hata watumishi wakomavu wa Yehova. Je, hilo linamaanisha kwamba hatuwezi kufaulu? Hapana. Yehova aliruhusu mifano hiyo iandikwe katika Biblia ili iwe “onyo kwetu.” (1 Kor. 10:11) Anajua kwamba tunaweza kujifunza kutokana na mifano hiyo yenye kuonya, na hivyo kuepuka au kutoka kwenye mitego ya Ibilisi.

MŨTEGO JWA RWIKUMIO

Tazama fungu la 4

4. Rwikumio rũũmba kwĩthĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ?

4 Shetani anataka tusitawishe sifa ya kiburi. Anajua kwamba ikiwa tutaruhusu kiburi kitutawale, tutakuwa kama yeye na kupoteza tumaini la kuishi milele. (Met. 16:18) Hivyo, mtume Paulo alionya kwamba mtu anaweza kuwa “na kiburi na kuanguka katika hukumu aliyohukumiwa Ibilisi.” (1 Tim. 3:6, 7) Mtu yeyote anaweza kuanguka kwenye mtego huo, iwe ni mpya katika kweli au amekuwa akimtumikia Yehova kwa miaka mingi.

5. O ta ũrĩa Mutumiiria 7:16, 20 yoonanĩtie, nĩatĩa muntũ oomba kwonania rwikumio?

5 Watu wenye kiburi wana ubinafsi. Shetani hujaribu kutushawishi tuwe wabinafsi, na tujifikirie wenyewe kupita kiasi badala ya Yehova, hasa tunapokuwa tunakabili changamoto. Kwa mfano, je, umeshutumiwa kimakosa? Au umetendewa kwa njia isiyo ya haki? Shetani angependa kukuona ukimlaumu Yehova au ndugu zako. Na Ibilisi angependa ufikiri kwamba njia pekee ya kusuluhisha tatizo ni kufanya mambo kwa njia yako mwenyewe, badala ya kufuata mwongozo ambao Yehova anakupatia katika Neno lake.—Soma Mhubiri 7:16, 20.

6. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na mantũ jarĩa mwarĩ-o-baaba ũmwe kuuma nthĩgũrũ ya Netherlands acioneere?

6 Fikiria kisa cha dada kutoka nchini Uholanzi ambaye alikasirishwa na udhaifu wa wengine. Aliamua kwamba hataweza kuendelea kuvumilia hali hiyo. Anasema hivi: “Nilijihisi mpweke sana na nilishindwa kubadili hisia zangu. Nilimwambia mume wangu kwamba tulihitaji kuhamia kutaniko lingine.” Kisha, alitazama programu ya Machi 2016 ya JW Broadcasting®. Programu hiyo ilitoa mapendekezo ya jinsi ya kushughulika na kutokamilika kwa wengine. Anaendelea kusema hivi: “Niliona kwamba nilihitaji kuchunguza kwa unyoofu na unyenyekevu makosa yangu mwenyewe badala ya kujaribu kuwabadilisha ndugu na dada kutanikoni. Programu hiyo ilinisaidia kumkazia fikira Yehova na enzi yake kuu.” Je, umetambua jambo kuu? Unapokabili jaribu, endelea kumkazia fikira Yehova. Mwombe akusaidie uwaone wengine kama yeye anavyowaona. Baba yako wa mbinguni anaona makosa yao; hata hivyo, yuko tayari kuwasamehe. Anataka wewe pia ufanye hivyo.—1 Yoh. 4:20.

Tazama fungu la 7

7. Nĩmbi biagwatĩre Mũnene Uzia?

7 Kiburi kilimfanya Mfalme Uzia wa Yuda akatae shauri na kutenda kwa kimbelembele. Uzia alikuwa mwanamume mwenye uwezo mwingi. Alifanikiwa vitani, alijenga majiji mengi, na alikuwa na mashamba mengi. “Mungu wa kweli alimfanikisha.” (2 Nya. 26:3-7, 10) Biblia inasema: “Hata hivyo, mara tu alipokuwa na nguvu, moyo wake ukawa na kiburi ambacho kilisababisha aangamie.” Awali, Yehova alikuwa ameamuru kwamba ni makuhani pekee waliopaswa kufukiza uvumba hekaluni. Lakini kwa kimbelembele Mfalme Uzia alienda hekaluni na kuvukiza uvumba. Yehova hakupendezwa na jambo hilo na akampiga kwa ukoma mwanamume huyo aliyekuwa na kiburi. Uzia aliendelea kuwa na ukoma maisha yake yote.—2 Nya. 26:16-21.

8. Kũringana na 1 Akorintho 4:6, 7, nĩatĩa tũũmba gũciebania na rwikumio?

8 Je, kiburi kinaweza kutufanya tunaswe kwenye mtego uliomnasa Uzia? Fikiria mfano wa José. Alikuwa mfanyabiashara aliyefanikiwa sana, aliyetumikia akiwa mzee anayeheshimika kutanikoni. Alitoa hotuba makusanyikoni na waangalizi wa mzunguko walikuwa wakimwomba ushauri. Anakiri hivi: “Lakini nilitegemea uzoefu na uwezo wangu mwenyewe. Nilikuwa nimemweka Yehova kando. Nilidhani nilikuwa imara, hivyo sikusikiliza maonyo na shauri la Yehova.” José alitenda dhambi nzito na kutengwa na ushirika. Alirudishwa miaka kadhaa iliyopita. Sasa anasema hivi: “Yehova amenifundisha kwamba jambo muhimu si kuwa na cheo fulani, bali ni kufanya mambo anayotaka tufanye.” Acheni tukumbuke kwamba vipawa vyovyote tulivyo navyo na mapendeleo yoyote tuliyo nayo kutanikoni yanatoka kwa Yehova. (Soma 1 Wakorintho 4:6, 7.) Ikiwa tuna kiburi Yehova hatatutumia.

MŨTEGO JWA ŨKOROKU

Tazama fungu la 9

9. Nĩatĩa ũkoroku bwatũmĩre Nkoma na Hawa bathithia?

9 Tunapofikiria sifa ya pupa, huenda tukamkumbuka Shetani Ibilisi. Akiwa malaika wa Yehova, ni lazima Shetani alikuwa na mapendeleo mengi mazuri. Lakini alitamani mengi zaidi. Alitaka ibada ambayo ni Yehova tu anayestahili. Shetani anataka tuwe kama yeye, hivyo anajaribu kutufanya tusiridhike na mambo tuliyo nayo. Mara ya kwanza Shetani kujaribu kufanya hivyo ni alipozungumza na Hawa. Kwa upendo, Yehova alikuwa amemwandalia Hawa na mume wake vyakula vingi vyenye kushibisha—waliweza “kula matunda ya kila mti katika bustani” isipokuwa mmoja. (Mwa. 2:16) Hata hivyo, Shetani alimdanganya Hawa afikiri kwamba alihitaji kula matunda kutoka kwenye mtu huo waliokatazwa. Hawa hakuthamini mambo aliyokuwa nayo, alitaka mengi zaidi. Tunajua matokeo yalikuwa nini. Hawa alitenda dhambi na mwishowe akafa.—Mwa. 3:6, 19.

Tazama fungu la 10

10. Nĩatĩa ũkoroku bwaere mũtego kĩrĩ Mũnene Daudi?

10 Pupa ilimfanya Mfalme Daudi asahau mambo ambayo Yehova alikuwa amempatia, kutia ndani utajiri, umashuhuri, na ushindi aliopata dhidi ya maadui wake wengi. Daudi alitambua kwamba zawadi za Mungu zilikuwa ‘nyingi sana kwake kusimulia!’ (Zab. 40:5) Lakini pindi moja, Daudi alisahau mambo ambayo Yehova alikuwa amempatia. Hakuridhika na mambo hayo; alitaka mengi zaidi. Ingawa Daudi alikuwa na wake kadhaa, aliruhusu tamaa mbaya kwa ajili ya mke wa mtu mwingine isitawi moyoni mwake. Mwanamke huyo alikuwa Bath-sheba, na mume wake alikuwa Uria. Kwa sababu ya ubinafsi Daudi alifanya ngono na Bath-sheba, naye akapata mimba. Kufanya uzinzi lilikuwa jambo baya, lakini Daudi alifanya jambo baya hata zaidi kwa kupanga Uria auawe! (2 Sam. 11:2-15) Daudi alikuwa akifikiria nini? Je, alikuwa anawazia kwamba Yehova hangeona? Mtumishi huyo mwaminifu wa Yehova alinaswa kwenye mtego wa pupa na akapatwa na matokeo mabaya sana. Hata hivyo, inafurahisha kwamba baada ya muda alikiri dhambi yake na kutubu. Alishukuru sana kupata tena kibali cha Yehova!—2 Sam. 12:7-13.

11. Kũringana na Aefeso 5:3, 4, nĩmbi kĩũmba gũtũteethia kũrũa na ũkoroku?

11 Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Daudi? Tunajifunza kwamba tunaweza kushinda pupa ikiwa tutaendelea kuwa wenye shukrani kwa mambo yote ambayo Yehova ametupatia. (Soma Waefeso 5:3, 4.) Ni lazima turidhike na vitu tulivyo navyo. Tunapoanza kujifunza Biblia pamoja na watu, tunawatia moyo wafikirie baraka moja hususa waliyopata kutoka Yehova na kumshukuru kwa baraka hiyo. Ikiwa mtu anafanya hivyo kila siku kwa juma moja, inamaanisha kwamba atakuwa amesali kuhusu mambo saba tofauti. (1 The. 5:18) Je, wewe unafanya hivyo? Ikiwa unatafakari kuhusu mambo yote ambayo Yehova amefanya kwa ajili yako, utachochewa kuwa mwenye shukrani. Na unapokuwa mwenye shukrani, unaridhika. Na unaporidhika, hutanaswa na mtego wa pupa.

Tazama fungu la 12

12. Nĩatĩa ũkoroku bwatongererie Judasi Muisikariota?

12 Pupa ilimfanya Yuda Iskariote awe msaliti mwovu. Lakini mwanzoni hakuwa hivyo. (Luka 6:13, 16) Yesu alimchagua Yuda kuwa mtume. Ni wazi kwamba Yuda alikuwa mwenye uwezo na alitegemeka, kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa anatunza sanduku la pesa. Yesu na mitume walitumia pesa hizo kwa ajili ya matumizi yao katika kazi ya kuhubiri. Pesa hizo zilikuwa kama michango ya kazi ya ulimwenguni pote leo. Lakini baada ya muda fulani, Yuda alianza kuiba licha ya kumsikia Yesu akionya kuhusu pupa tena na tena. (Marko 7:22, 23; Luka 11:39; 12:15) Yuda alipuuza maonyo hayo.

13. Nĩrĩ ũkoroku bwa Judasi bwaciumĩrĩrie?

13 Pupa ya Yuda ilionekana wazi kwenye tukio fulani muda mfupi kabla ya Yesu kuuawa. Yesu na wanafunzi wake, kutia ndani Maria na dada yake, Martha, walikuwa wageni wa Simoni mwenye ukoma. Wakati wa mlo, Maria alisimama na kumimina mafuta yenye marashi ya bei ghali kwenye kichwa cha Yesu. Yuda na wanafunzi wengine walikasirika sana. Huenda wanafunzi wengine walihisi kwamba pesa hizo zingetumiwa vizuri zaidi katika huduma. Lakini nia ya Yuda ilikuwa tofauti. “Alikuwa mwizi” na alitaka kuiba pesa kwenye kisanduku. Baadaye, pupa ilimchochea Yuda kumsaliti Yesu kwa bei ya mtumwa.—Yoh. 12:2-6; Mt. 26:6-16; Luka 22:3-6.

14. Nĩatĩa antũ bamwe bagũrene batumĩĩre kĩthoomo kĩrĩa gĩkwonora kĩrĩ Luka 16:13?

14 Yesu aliwakumbusha wafuasi wake kweli hii ya msingi: “Hamwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.” (Soma Luka 16:13.) Bado hilo ni kweli. Fikiria jinsi ambavyo wenzi fulani wa ndoa nchini Romania walivyotumia maneno ya Yesu. Walikuwa wamepata kazi ya muda mfupi katika nchi yenye uchumi mkubwa zaidi. Wanasema hivi: “Tulikuwa na mkopo mkubwa wa benki ambao tulihitaji kulipa, hivyo mwanzoni tulifikiri kwamba kazi hiyo ilikuwa baraka kutoka kwa Yehova.” Hata hivyo, kulikuwa na tatizo. Kazi hiyo ingeathiri utumishi wao kwa Yehova. Baada ya kusoma makala “Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Kamili” katika gazeti Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 2008, walifanya uamuzi. Wanasema hivi: “Ikiwa nia yetu ya kufanya kazi katika nchi nyingine ingekuwa kupata pesa zaidi, tungekuwa tukiupa uhusiano wetu na Yehova nafasi ya pili maishani. Tulisadiki kwamba hali yetu ya kiroho ingeathirika.” Hivyo walikataa kazi hiyo. Hali ikawaje? Mume alipata kazi ambayo ingetosheleza mahitaji yao. Mke anasema: “Kamwe mkono wa Yehova si mfupi.” Wenzi hao wa ndoa wanafurahi kwa sababu walimfanya Yehova kuwa Bwana wao badala ya pesa.

CIEBANIE NA MĨTEGO YA NKOMA

15. Nĩatĩa tũũmba kwĩthĩrwa na mma atĩ twomba kuuma kĩrĩ mĩtego ya Nkoma?

15 Namna gani ikiwa tumegundua kwamba tumenaswa na mtego wa kiburi au pupa? Tunaweza kuponyoka! Paulo alisema kwamba wale ambao ‘wamenaswa na Ibilisi wakiwa hai,’ bado wanaweza kutoka kwenye mtego. (2 Tim. 2:26) Isitoshe, Daudi alimsikiliza Nathani alipomkaripia, akatubu kwa sababu ya kusitawisha pupa, na akarudisha uhusiano wake mzuri pamoja na Yehova. Usisahau kamwe kwamba Yehova ana nguvu kuliko Shetani. Hivyo, ikiwa tutakubali msaada wa Yehova tunaweza kutoka kwenye mtego wowote ambao Ibilisi ametega.

16. Nĩmbi kĩũmba gũtũteethia gũciebania na mĩtego ya Nkoma?

16 Bila shaka, badala kujiruhusu kunaswa na mitego ya Shetani na kisha kutoka, tunapaswa kuiepuka kabisa. Tunaweza kufanya hivyo kwa msaada wa Yehova tu. Hata hivyo, hatupaswi kujiamini! Hata watumishi wa muda mrefu wa Yehova wamenaswa na mtego wa kiburi au pupa. Hivyo, kila siku msihi Yehova akusaidie kutambua ikiwa sifa hizo mbaya zimeanza kuathiri njia yako ya kufikiri na matendo yako. (Zab. 139:23, 24) Kamwe usikubali kunaswa na kiburi na pupa!

17. Nĩmbi gĩkagwata mũnthũ wetũ Nkoma kagita gatĩ kũraaja?

17 Kwa maelfu ya miaka, Shetani amekuwa mwindaji. Lakini hivi karibuni, atafungwa na mwishowe kuharibiwa. (Ufu. 20:1-3, 10) Tunaisubiri kwa hamu siku hiyo. Hadi wakati huo ufike, uwe macho kutambua mitego ya Shetani. Jitahidi sana kuzuia kiburi na pupa visikutawale. Azimia ‘kumpinga Ibilisi naye atakukimbia.’—Yak. 4:7.

RWĨMBO 127 Napaswa Kuwa Mtu wa Namna Gani?

^ gic. 5 Shetani ni kama mwindaji stadi. Anajaribu kututega haidhuru tumemtumikia Yehova kwa muda gani. Katika makala hii, tutajifunza jinsi Shetani anavyotumia kiburi na pupa ili kuharibu uhusiano wetu pamoja na Mungu. Pia, tutajifunza kutoka kwa watu ambao walinaswa na mtego wa kiburi na pupa, na tutaona jinsi tunavyoweza kuepuka mitego hiyo.

^ gic. 2 UFAFANUZI WA MANENO: Makala hii inazungumzia sifa ya kiburi. Kiburi ni hisia ya mtu kujiona kuwa yeye ni bora kuliko wengine. Pia, tutazungumzia pupa. Pupa ni tamaa inayopita kiasi ya kutaka kuwa na pesa nyingi zaidi, mamlaka nyingi zaidi, au kufanya ngono zaidi, au mambo mengine kama hayo.

^ gic. 53 MAELEZO YA PICHA: Kwa kiburi ndugu anakataa mwongozo wenye hekima. Dada aliye na vitu vingi anatamani kujipatia vitu vingi hata zaidi.

^ gic. 55 MAELEZO YA PICHA: Kiburi kilimwathiri mwana wa kiroho wa Mungu na Mfalme Uzia. Pupa ilimchochea Hawa ale matunda kutoka kwenye mti uliokatazwa, Daudi afanye uzinzi na Bath-sheba, na Yuda aibe pesa.