Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 22

Tetheeria Aritwa Baaku ba Bibiria Bakinyĩre Ũbatithio

Tetheeria Aritwa Baaku ba Bibiria Bakinyĩre Ũbatithio

“Kila mmoja wenu abatizwe.”—MATH 2:38.

RWĨMBO 72 Kutangaza Ukweli wa Ufalme

MUHTASARI *

1. Nĩatĩa ntundu ĩnene kĩrĩ karine ya mbere yeeri ĩthithie?

UMATI mkubwa wa wanaume na wanawake kutoka nchi mbalimbali na wanaozungumza lugha tofauti-tofauti ulikuwa umekusanyika pamoja. Jambo fulani la pekee lilitukia siku hiyo. Kikundi cha Wayahudi wa kawaida tu kilikuwa kikizungumza lugha za kienyeji za watu hao! Ingawa jambo hilo lilikuwa linashangaza, jambo la pekee hata zaidi ni mambo ambayo Wayahudi hao walikuwa wakisema na mambo ambayo mtume Petro aliwaambia. Mambo aliyowaambia yalitia ndani ujumbe kwamba wangeweza kuokolewa kwa kumwamini Yesu Kristo. Umati huo uliguswa moyo sana na ujumbe huo. Watu hao walichochewa sana hivi kwamba waliuliza hivi: “Tufanye nini?” Petro aliwajibu hivi: “Kila mmoja wenu abatizwe.”—Mdo. 2:37, 38.

Ndugu, aliyeandamana na mke wake, akiongoza funzo la Biblia na mwanamume kijana mwenye nakala iliyochapishwa ya kitabu ‘Furahia Maisha Milele!’ (Tazama fungu la 2)

2. Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ? (Tega mbica karatacine ka mbere.)

2 Jambo lililotokea baadaye lilikuwa lenye kushangaza. Watu 3,000 walibatizwa siku hiyo na kuwa wanafunzi wa Kristo. Huo ulikuwa mwanzo wa kazi kubwa ya kufanya wanafunzi ambayo Yesu aliwaamuru wanafunzi wake wafanye. Kazi hiyo imeendelea kufanywa hadi karne ya 21. Katika siku zetu, hatuwezi kumsaidia mtu afikie hatua ya ubatizo kwa saa chache tu. Huenda ikachukua miezi au hata mwaka au zaidi ili mwanafunzi afikie hatua hiyo. Ikiwa unajifunza Biblia na mtu fulani, unaelewa kwamba kazi ya kufanya wanafunzi inahitaji jitihada. Katika makala hii, tutachunguza mambo unayoweza kufanya ili kumsaidia mwanafunzi wako wa Biblia afikie hatua ya ubatizo.

TETHEERIA MŨRITWA WAAKU WA BIBIRIA ATUMĨRE JARĨA AKWIRITANA

3. Ja ũrĩa kwoonanĩtue kĩrĩ Mathayo 28:19, 20, no mwanka mũritwa wa Bibiria athithie atĩa nĩkenda akinyĩra ũbatithio?

3 Kabla ya kubatizwa, ni lazima mwanafunzi wa Biblia atumie mambo ambayo Biblia inafundisha. (Soma Mathayo 28:19, 20.) Mwanafunzi anapotumia mambo anayojifunza, anakuwa kama mtu mwenye busara katika mfano wa Yesu ambaye alichimba kina kirefu ili ajenge nyumba yake kwenye mwamba. (Mt. 7:24, 25; Luka 6:47, 48) Tunaweza kumsaidiaje mwanafunzi atumie mambo anayojifunza? Acheni tuchunguze mapendekezo matatu.

4. Nĩatĩa tũũmba gũtetheeria mũritwa wa Bibiria ĩtagaaria kwa ĩtagaaria nĩkenda akinyĩra ũbatithio? (Tega kathandũkũ “Tetheeria Mũritwa Waaku wa Bibiria Gwĩka Mĩoroto na Kũmĩkinyĩra.”)

4 Msaidie mwanafunzi wako ajiwekee malengo. Kwa nini unapaswa kufanya hivyo? Fikiria mfano huu: Ikiwa unapanga kusafiri kwenda mbali, huenda ukaamua kusimama njiani kwenye maeneo yanayovutia. Kwa kufanya hivyo, huenda safari hiyo isionekane kuwa ndefu na yenye kulemea. Vivyo hivyo, mwanafunzi wa Biblia anapojiwekea malengo ya muda mfupi na kuyafikia, huenda akatambua kwamba anaweza kufikia lengo lake la kubatizwa. Tumia sehemu ya “Lengo” kwenye kitabu Furahia Maisha Milele! ili kumsaidia mwanafunzi wako afanye maendeleo. Mwishoni mwa kila soma, zungumzia jinsi lengo hilo linavyohusiana na mambo ambayo mwanafunzi ametoka kujifunza. Ikiwa una lengo tofauti kwa ajili ya mwanafunzi wako, liandike kwenye sehemu “Lengo Lingine.” Tumia kwa ukawaida sehemu hii ya funzo ili kupitia pamoja na mwanafunzi wako malengo yake ya muda mfupi na ya muda mrefu.

5. Ja ũrĩa kwoonanĩtue kĩrĩ Mariko 10:17-22, nĩatĩa Jesũ eerĩre muntũ mũrũme gĩtonga, na nĩkĩ?

5 Msaidie mwanafunzi wako afanye mabadiliko maishani. (Soma Marko 10:17-22.) Yesu alijua kwamba ingekuwa vigumu kwa yule mwanamume tajiri kuuza mali zake zote. (Marko 10:23) Hata hivyo, Yesu alimwambia mwanamume huyo afanye badiliko hilo kubwa maishani mwake. Kwa nini? Kwa sababu Yesu alimpenda. Nyakati fulani, huenda hatumtii moyo mwanafunzi atumie mambo anayojifunza kwa sababu tunahisi kwamba hayuko tayari kufanya mabadiliko yanayohitajika. Huenda ikachukua muda kwa watu kuvua utu wao wa zamani na kuvaa utu mpya. (Kol. 3:9, 10) Lakini kadiri unavyozungumzia mapema badiliko analohitaji kufanya, ndivyo mwanafunzi atakavyoweza kufanya mabadiliko haraka. Kuzungumzia jambo hilo pamoja naye, kunaonyesha kwamba unamjali.—Zab. 141:5; Met. 27:17.

6. Nĩkĩ tũtumĩre biũria biria bigatũtetheeria kũmenya ũrĩa muntũ akũthũgaania?

6 Swali la maoni ni swali ambalo linatusaidia kujua fikira au maoni ya mwanafunzi kuhusu jambo fulani. Tumia maswali hayo ili kutambua mambo ambayo mwanafunzi wako anaelewa na kuamini. Ikiwa unafanya hivyo kwa ukawaida, itakuwa rahisi zaidi kuzungumzia mambo mazito wakati ujao. Kitabu Furahia Maisha Milele! kina maswali mengi ya maoni. Kwa mfano, somo la 4 linauliza: “Unafikiri Yehova anahisije unapolitumia jina lake?” Somo la 9 linauliza: “Wewe ungependa kusali kuhusu mambo gani?” Huenda mwanzoni ikawa vigumu kwa mwanafunzi wako kujibu maswali ya maoni. Unaweza kumsaidia kwa kumzoeza afikiri kuhusu maandiko na picha zilizo kwenye kitabu.

7. Nĩatĩa ũũmba gũtumĩra mantũ jarĩa antũ bacionerete ũtũũrone bwao na njĩra ĩrĩ na maumĩĩra?

7 Mwanafunzi wako atakapoelewa jambo analohitaji kufanya, tumia simulizi halisi la maisha ili kumtia moyo afanye jambo hilo. Kwa mfano, ikiwa mwanafunzi wako hahudhurii mikutano kwa ukawaida, unaweza kumwonyesha video Yehova Alinitunza kwenye sehemu ya “Chunguza Zaidi” ya somo la 14. Kwenye masomo mengi ya kitabu Furahia Maisha Milele! utapata masimulizi kama hayo kwenye sehemu ya “Chimba Zaidi” au “Chunguza Zaidi.” * Uwe mwangalifu usimlinganishe mwanafunzi wako na mtu mwingine kwa kumwambia, “Ikiwa yeye alifaulu, na wewe unaweza pia.” Mruhusu mwanafunzi afikie uamuzi wake mwenyewe. Zungumzia mambo hususa ambayo yalimsaidia mhusika huyo katika video atumie mafundisho ya Biblia. Labda unaweza kukazia andiko moja la msingi au jambo fulani muhimu lililofanywa. Kadiri inavyowezekana, kazia jinsi ambavyo Yehova alimsaidia mtu huyo.

8. Nĩatĩa tũũmba gũtetheeria mũritwa wa Bibiria eenda Jehova?

8 Msaidie mwanafunzi wako ampende Yehova. Jinsi gani? Tafuta fursa za kukazia sifa za Yehova. Msaidie mwanafunzi wako amwone Yehova kuwa Mungu mwenye furaha ambaye huwategemeza wale wanaompenda. (1 Tim. 1:11; Ebr. 11:6) Mwonyeshe mwanafunzi kwamba atanufaika kwa kutumia habari anayojifunza na umweleze kwamba manufaa yoyote anayopata yanaonyesha kwamba Yehova anampenda. (Isa. 48:17, 18) Mwanafunzi wako atachochewa zaidi kufanya mabadiliko yanayohitajika kadiri upendo wake kwa Yehova unavyoongezeka.—1 Yoh. 5:3.

TETHEERIA MŨRITWA WA BIBIRIA AMENYANE NA ATAANA NA AARĨ BA BAABA

9. Kũringana na Mariko 10:29, 30, nĩmbi kĩũmba gũtetheeria mũritwa wa Bibiria aciejana nĩkenda akinyĩra ũbatithio?

9 Ili afikie hatua ya ubatizo, mwanafunzi wa Biblia atahitaji kujidhabihu. Kama mwanamume tajiri aliyetajwa awali, huenda baadhi ya wanafunzi wakahitaji kudhabihu vitu fulani vya kimwili. Ikiwa kazi yao ya kimwili haipatani na kanuni za Biblia, huenda wakahitaji kutafuta kazi nyingine. Wengi wao huenda wakahitaji kuacha kushirikiana na rafiki zao ambao hawampendi Yehova. Wengine huenda wakatelekezwa na watu wa familia ambao hawawapendi Mashahidi wa Yehova. Yesu alisema kwamba huenda ikawa vigumu kwa baadhi ya watu kujidhabihu kwa njia hiyo. Lakini aliahidi kwamba wale wanaomfuata hawatatamaushwa. Watathawabishwa sana kwa kupata familia ya kiroho yenye upendo. (Soma Marko 10:29, 30.) Unaweza kumsaidiaje mwanafunzi wako wa Biblia anufaike kutokana na zawadi hiyo nzuri?

10. Nĩmbi ũkwiritana kuumania na mantũ jarĩa Manuel acioneere?

10 Sitawisha urafiki pamoja na mwanafunzi wako. Ni muhimu kumwonyesha mwanafunzi wako kwamba unamjali. Kwa nini? Fikiria maelezo ya Manuel anayeishi nchini Mexico. Akikumbuka alipokuwa akijifunza Biblia anasema hivi: “Kabla ya kila kipindi cha funzo, mwalimu wangu angenijulia hali. Alinisaidia kutulia na kuniruhusu nijieleze kuhusu jambo lolote. Nilihisi ananijali sana.”

11. Nĩatĩa aritwa beetũ ba Bibiria boomba kũgunĩka twethĩrwa na kaanya nabo?

11 Tumia wakati pamoja na wanafunzi wako kama Yesu alivyofanya na wafuasi wake. (Yoh. 3:22) Ikiwa inawezekana, mwalike mwanafunzi wako wa Biblia anayefanya maendeleo nyumbani kwako ili mfurahie kikombe cha kahawa au mlo au kutazama mojawapo ya programu zetu za JW Broadcasting®. Huenda mwanafunzi wako akathamini mwaliko huo hasa wakati wa sikukuu, ambapo huenda akahisi upweke. Kazibwe, anayeishi nchini Uganda, anasema hivi: “Ninafikiri nilijifunza pia mambo mengi kumhusu Yehova kwa kutumia wakati pamoja na mwalimu wangu, kama tu nilivyojifunza kupitia kipindi cha funzo. Nilijionea jinsi ambavyo Yehova anawajali sana watu wake na jinsi walivyo na furaha. Hayo ndiyo maisha niliyoyataka.”

Kadiri unavyoandamana na wahubiri tofauti-tofauti kwenye funzo la Biblia, ndivyo mwanafunzi wako atakavyovutiwa zaidi kuhudhuria mikutano (Tazama fungu la 12) *

12. Nĩkĩ tũbuĩrĩte gwĩta na atũmĩĩria mwanya mwanya rĩrĩa tũgũtongeeria wiritani bwa Bibiria?

12 Waalike wahubiri tofauti-tofauti kwenye funzo la Biblia. Nyakati nyingine, huenda tukahisi kwamba ni rahisi zaidi kwenda kuongoza funzo peke yetu au na mhubiri yuleyule kila mara. Ingawa huenda ikawa rahisi zaidi kufanya hivyo, inaelekea mwanafunzi wetu wa Biblia atanufaika zaidi ikiwa mara kwa mara tutaenda na wahubiri tofauti-tofauti. Dmitrii, anayeishi nchini Moldova, anasema hivi: “Kila mhubiri aliyekuja kwenye funzo langu angeeleza mambo kwa njia ya pekee. Jambo hilo lilinisaidia kuona njia nyingine ambazo ningeweza kutumia mambo niliyokuwa nikijifunza. Pia, sikuwa mwenye haya sana nilipohudhuria mkutano kwa mara ya kwanza, kwa kuwa tayari nilikuwa ninafahamiana na ndugu na dada wengi.”

13. Nĩkĩ tũbuĩrĩte gũtetheeria mũritwa weetũ eeje mĩcemanione?

13 Msaidie mwanafunzi wako ahudhurie mikutano ya kutaniko. Kwa nini? Kwa sababu Yehova anawaamuru waabudu wake wakutanike pamoja; ni sehemu ya ibada yetu. (Ebr. 10:24, 25) Pia, ndugu na dada zetu ni familia yetu ya kiroho. Tunapokuwa pamoja nao kwenye mikutano, ni kana kwamba tunashiriki pamoja mlo mtamu. Unapomsaidia mwanafunzi wako wa Biblia kuhudhuria mikutano, utakuwa ukimsaidia kuchukua mojawapo ya hatua muhimu zaidi za kufikia ubatizo. Lakini huenda ikawa vigumu kwake kuchukua hatua hiyo. Kitabu Furahia Maisha Milele! kinaweza kumsaidiaje mwanafunzi wako kushinda changamoto zozote ambazo huenda akakabili?

14. Nĩatĩa tũũmba kuurutĩĩra mũritwa eeja mĩcemanione?

14 Ili kumchochea mwanafunzi wako, tumia somo la 10 la kitabu Furahia Maisha Milele! Wahubiri wenye uzoefu walioombwa wafanyie majaribio somo hilo kabla kitabu hakijatolewa, walifanikiwa sana kuwasaidia wanafunzi wao wa Biblia wahudhurie mikutano. Bila shaka, huhitaji kusubiri hadi mfike somo la 10 ili umwalike mwanafunzi wako wa Biblia kuhudhuria mikutano yetu. Mwalike mapema iwezekanavyo na uendelee kufanya hivyo kwa ukawaida. Kila mwanafunzi anakabili changamoto tofauti. Hivyo, zingatia mahitaji ya mwanafunzi wako na uone ikiwa unaweza kumsaidia. Usivunjike moyo ikiwa hataanza kuhudhuria mikutano haraka. Uwe na subiri na usichoke kumwalika.

TETHEERIA MŨRITWA WAAKU WA BIBIRIA KŨŨMBANA NA ŨGUAA

15. Aritwa beetũ ba Bibiria boomba kwĩthĩrwa na ũguaa bũrĩkũ?

15 Je, unakumbuka kuhisi woga kidogo ulipotaka kuwa Shahidi wa Yehova? Huenda ulihisi kwamba hutaweza kamwe kuhubiri hadharani. Au labda uliogopa kwamba watu wa familia au marafiki watakupinga. Ikiwa ndivyo, unaweza kuelewa hisia za mwanafunzi wako wa Biblia. Yesu alisema kwamba huenda baadhi ya watu wangekuwa na woga kama huo. Hata hivyo, aliwahimiza wafuasi wake wasiruhusu woga uwazuie kumtumikia Yehova. (Mt. 10:16, 17, 27, 28) Yesu aliwasaidiaje wafuasi wake washinde woga? Na tunaweza kuigaje mfano wake?

16. Nĩatĩa tũũmba kũmenyerithia mũritwa weetũ wa Bibiria kwĩĩra bangĩ bwegie wĩtĩkio bwawe?

16 Hatua kwa hatua mzoeze mwanafunzi wako awaeleze wengine kuhusu imani yake. Huenda wanafunzi wa Yesu walikuwa na wasiwasi alipowatuma wakahubiri. Lakini Yesu aliwasaidia kwa kuwaambia mahali na ujumbe wa kuhubiri. (Mt. 10:5-7) Unaweza kumwigaje Yesu? Msaidie mwanafunzi wako atambue watu anaoweza kuwahubiria. Kwa mfano, muulize ikiwa anamjua mtu anayeweza kufaidika na kweli fulani ya Biblia. Kisha msaidie kutayarisha habari ya kusema, kwa kumwonyesha njia rahisi ya kuwaeleza wengine kweli fulani rahisi. Inapofaa, unaweza kumzoeza kwa kutumia sehemu “Watu Fulani Husema” na “Huenda Akauliza” zinazopatikana kwenye kitabu Furahia Maisha Milele! Unapofanya hivyo, kazia fikira kumzoeza mwanafunzi wako jinsi ya kutumia Biblia ili kuwajibu watu kwa njia rahisi na yenye busara.

17. Nĩatĩa tũũmba gũtumĩra Mathayo 10:19, 20, 29-31, rĩrĩa tũgũtetheeria mũritwa weetũ eerĩgĩĩra Jehova?

17 Msaidie mwanafunzi wako amtumaini Yehova. Yesu aliwahakikishia wanafunzi wake kwamba Yehova angewasaidia kwa sababu aliwapenda. (Soma Mathayo 10:19, 20, 29-31.) Mkumbushe mwanafunzi wako kwamba Yehova atamsaidia yeye pia. Unaweza kumsaidia amtegemee Yehova kwa kusali pamoja naye kuhusu malengo yake. Franciszek, anayeishi nchini Poland, anasema hivi: “Mara nyingi mwalimu wangu alitaja malengo yangu katika sala zake. Nilipoona jinsi Yehova alivyojibu sala za mwalimu wangu, haraka mimi pia nilianza kusali. Nilijionea msaada wa Yehova nilipohitaji kuomba ruhusa kwenye kazi niliyotoka tu kuajiriwa, ili nihudhurie mikutano na kusanyiko.”

18. Nĩatĩa Jehova aigagua bwegie ngũgĩ ya kũritana ĩrĩa Akristũ bathiithagia?

18 Yehova anawajali sana wanafunzi wetu wa Biblia. Anathamini kazi ngumu ya kufundisha inayofanywa na Wakristo ili kuwasaidia watu wamkaribie zaidi, na kwa sababu hiyo anawapenda. (Isa. 52:7) Ikiwa kwa sasa huongozi funzo la Biblia, bado unaweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia kufanya maendeleo na kufikia hatua ya ubatizo kwa kuandamana na wahubiri wengine wanapoongoza mafunzo yao ya Biblia.

RWĨMBO 60 Ni Uzima Kwao

^ gic. 5 Makala hii itazungumzia jinsi Yesu alivyowasaidia watu kuwa wanafunzi wake na jinsi tunavyoweza kumwiga. Pia, tutazungumzia baadhi ya sehemu za kitabu kipya Furahia Maisha Milele! Kitabu hicho kimeandaliwa ili kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia wafikie hatua ya ubatizo.

^ gic. 7 Pia, unaweza kupata masimulizi halisi ya maisha kwenye (1) Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova chini ya kichwa “Biblia,” kisha “Manufaa,” na mwishowe “‘Biblia Inabadili Maisha’ (Mfululizo katika Mnara wa Mlinzi)” au kwenye (2) JW Library® sehemu ya midia kwenye “Mahojiano na Mambo Yaliyoonwa.”

^ gic. 62 MAELEZO YA PICHA: Ndugu akiwa ameandamana na mke wake, anajifunza na mwanamume kijana. Nyakati nyingine, akina ndugu tofauti-tofauti wanaandamana naye anapoongoza funzo hilo.