Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 4

Ndaba Jaki Tuhuzuli Ukumbusho?

Ndaba Jaki Tuhuzuli Ukumbusho?

“Nnhendalya kuhenga ana kukungomboka ne.”​—LUKA 22:19.

NHAMBU 20 Ulimtoa Mwana Wako Mpendwa

MUHTASARI *

1-2. (a) Lile, hasa patunkomboka mpendwa jwitu jojuwile? (b) Yesu jwaanzisa ki ikilu ja mwisu kabla ja kuwa kwake?

 HATA iwe wapendwa wetu walikufa zamani sana, bado tunawakumbuka. Tarehe waliyokufa inapofika huwa tunawakumbuka sana.

2 Kila mwaka, tunakuwa miongoni mwa mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanaokusanyika ili kukumbuka kifo cha mtu tunayempenda sana​—Yesu Kristo. (1 Pet. 1:8) Tunakusanyika kumkumbuka yule aliyetoa uhai wake uwe fidia ili kutukomboa kutokana na dhambi na kifo. (Mt. 20:28) Isitoshe, Yesu aliwaagiza wafuasi wake wakumbuke kifo chake. Usiku wa kabla ya kifo chake, alianzisha mlo wa pekee wa jioni na akaamuru hivi: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.” *​—Luka 22:19.

3. Musitulongalya ki mumakala jenzeno?

3 Idadi ndogo ya watu wanaohudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo wana tumaini la kuishi mbinguni. Lakini mamilioni walio na tumaini la kuishi duniani wanahudhuria pia. Katika makala hii, tutachunguza kwa nini vikundi vyote viwili vinatazamia kwa hamu kuhudhuria Ukumbusho kila mwaka. Pia, tutachunguza jinsi tunavyonufaika kwa kuhudhuria. Acheni tuanze kwa kuchunguza baadhi ya sababu zinazowafanya Wakristo watiwa-mafuta wahudhurie.

NDABA JAKI AKRISTO ATIWA MAFUTA AHUZULIA?

4. Ndaba jaki akristo atiwa mafuta ashiliki kula nkati na kunywa divai wakati gu Ukumbusho?

4 Kila mwaka, Wakristo watiwa-mafuta wanapohudhuria Ukumbusho, wao hushiriki kula mkate na kunywa divai. Kwa nini wanastahili kula mkate na kunywa divai? Ili kujibu swali hilo, fikiria mambo yaliyotukia katika usiku wa mwisho wa maisha ya Yesu duniani. Baada ya mlo wa Pasaka, Yesu alianzisha mwadhimisho unaoitwa Mlo wa Jioni wa Bwana. Alipitisha mkate na divai kwa mitume wake waaminifu 11 na kuwaambia wale na kunywa. Yesu aliwaambia kuhusu maagano, au makubaliano mawili​—agano jipya na agano la Ufalme. * (Luka 22:19, 20, 28-30) Maagano hayo yalifungua njia kwa mitume hao na idadi ndogo ya watu wengine kuwa wafalme na makuhani mbinguni. (Ufu. 5:10; 14:1) Mabaki * ya Wakristo watiwa-mafuta walio katika maagano hayo mawili, ndio hushiriki kula mkate na kunywa divai kwenye Ukumbusho.

5. Atiwa mafuta amanya ki kuhusu litumaini labo?

5 Kuna sababu nyingine inayofanya watiwa-mfuta wahudhurie Ukumbusho: Wanapohudhuria wanapata fursa ya kufikiria kuhusu tumaini lao. Yehova amewapa tumaini la pekee sana​—kufurahia uhai usioweza kufa wala kuharibika mbinguni, kutumikia pamoja na Yesu Kristo aliyetukuzwa na wale 144,000 wenzao, na zaidi ya yote, kuwa mbele za Yehova Mungu! (1 Kor. 15:51-53; 1 Yoh. 3:2) Watiwa-mafuta wanatambua kwamba wamealikwa ili wakafurahie mapendeleo hayo mbinguni. Lakini ili waruhusiwe kwenda mbinguni ni lazima waendelee kuwa waaminifu hadi kifo chao. (2 Tim. 4:7, 8) Watiwa-mafuta wanafurahi sana wanapotafakari kuhusu tumaini lao la mbinguni. (Tito 2:13) Namna gani kuhusu “kondoo wengine”? (Yoh. 10:16) Ni sababu gani zinazowafanya wahudhurie Ukumbusho?

KWA NDABA JAKI AKAKONDOO BANGI AHUZULIA

6. Ndaba jaki akakondoo bangi ahuzuli Ukumbushu Kila mwaka?

6 Ingawa hawashiriki kula mkate na kunywa divai, kondoo wengine wanahudhuria Ukumbusho wakiwa watazamaji. Mwaka wa 1938, wale walio na tumaini la kuishi duniani kwa mara ya kwanza walialikwa kihususa kuhudhuria Ukumbusho. Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 1938, lilisema hivi: “Ni jambo sahihi na linalofaa kabisa kwa [kondoo wengine] kuhudhuria mkutano huo na kutazama kinachoendelea. . . . Wao pia wanapaswa kushangilia wakati huo.” Kama wageni walioalikwa wanavyofurahia kuwa watazamaji kwenye sherehe ya harusi, kondoo wengine wanafurahi kuhudhuria Ukumbusho wakiwa watazamaji.

7. Ndaba jaki akakondoo bangi alende kwa hamu kupelakane otuba Juukumbusho?

7 Kondoo wengine pia wanafikiria kuhusu tumaini lao. Wanatazamia kwa hamu kusikiliza kwa makini hotuba ya Ukumbusho, kwa sababu habari nyingi zinahusu mambo ambayo Kristo na watawala wenzake 144,000, watawafanyia wanadamu waaminifu wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja. Wakiongozwa na Mfalme Yesu Kristo, watawala hao wa mbinguni watasaidia kuibadili dunia kuwa paradiso na kuwasaidia wanadamu watiifu wafikie ukamilifu. Mamilioni ya watazamaji wanaohudhuria Ukumbusho wanasisimka kuwazia jinsi unabii wa Biblia utakavyotimizwa wakati ujao, kama vile unabii unaopatikana kwenye Isaya 35:5, 6; 65:21-23; na Ufunuo 21:3, 4. Wanapojiwazia pamoja na wapendwa wao wakiwa katika ulimwengu mpya, wanaimarisha tumaini lao kwa ajili ya wakati ujao na azimio lao la kuendelea kumtumikia Yehova bila kuacha.​—Mt. 24:13; Gal. 6:9.

8. Jibi sababu bo jengi jejafanya akakondoo bangi ahuzulia Ukumbusho?

8 Fikiria sababu nyingine inayowafanya kondoo wengine wahudhurie Ukumbusho. Wanataka kuonyesha kwamba wanawapenda na kuwaunga mkono watiwa-mafuta. Neno la Mungu lilitabiri kwamba watiwa-mafuta wangekuwa na uhusiano wa karibu pamoja na wale walio na tumaini la kuishi duniani. Jinsi gani? Acheni tuzungumzie mifano michache.

9. Unabii gogupatikana mu Zekaria 8:23 gulangi bo jinsi akakondoo bangi eahisi kwahusu akristo atiwa-mafuta?

9 Soma Zekaria 8:23. Unabii huo unafafanua kwa njia nzuri jinsi kondoo wengine wanavyohisi kuhusu ndugu na dada zao watiwa-mafuta. Neno “Myahudi” na neno “nanyi” yanarejelea kikundi kilekile, yaani, watiwa-mafuta waliobaki duniani. (Rom. 2:28, 29) “Watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa” wanafananisha kondoo wengine. “Wanashika kwa nguvu,” yaani, wanashikamana na watiwa-mafuta kwa ushikamanifu, wakijiunga nao katika ibada safi. Hivyo, siku ya Ukumbusho, wanaonyesha uhusiano wao wa karibu na watiwa-mafuta kwa kuhudhuria.

10. Yehova juhengiki ki ili kutimisa unabii gogupatikana mu Ezekieli 37:15-19, 24, 25?

10 Soma Ezekieli 37:15-19, 24, 25. Yehova ametimiza unabii huo, kwa kufanya watiwa-mafuta na kondoo wengine wafanye kazi kwa ushirikiano na umoja. Unabii huo ulitaja vijiti viwili. Wale wenye tumaini la kuishi mbinguni ni kama kijiti “kwa ajili ya Yuda” (kabila ambalo lilitokeza wafalme wa Israeli), na wale walio na tumaini la kuishi duniani ni kama kijiti “cha Efraimu.” * Yehova angeviunganisha vikundi hivyo viwili ili viwe “kijiti kimoja.” Hilo linamaanisha kwamba wanatumikia kwa umoja chini ya Mfalme wao mmoja, Kristo Yesu. Kila mwaka, Wakristo watiwa-mafuta na kondoo wengine wanahudhuria Ukumbusho, si kama vikundi viwili, bali kama “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja.”​—Yoh. 10:16.

11. “Akakondoo” ba balogo mu Mathayo 25:31-36, 40 alangi bo kwamba ba ungankonu akandugu bika Kristo?

11 Soma Mathayo 25:31-36, 40. “Kondoo” wanaotajwa kwenye mfano huo wanafananisha waadilifu katika siku za mwisho ambao wanatumaini la kuishi duniani, yaani, kondoo wengine. Wanawaunga mkono kwa ushikamanifu ndugu za Kristo watiwa-mafuta waliobaki, hasa kwa kuwasaidia kutimiza jukumu kubwa sana, yaani, kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi ulimwenguni pote.​—Mt. 24:14; 28:19, 20.

12-13. Akakondoo bangi ba ungankonu akandugu bika Kristo katika indela bo jenge?

12 Kila mwaka, majuma kadhaa kabla ya Ukumbusho, kondoo wengine wanaonyesha kwamba wanawaunga mkono ndugu za Kristo kwa kushiriki kikamili katika kampeni ya ulimwenguni pote ya kuwaalika watu wanaopendezwa kwenye Ukumbusho. (Tazama sanduku “ Je, Unajitayarisha Mapema kwa Ajili ya Majira ya Ukumbusho?”) Pia, wanasaidia kufanya mipango yote inayohitajika ili Ukumbusho ufanywe katika kila kutaniko ulimwenguni pote, hata ingawa makutaniko mengi hayana watiwa-mafuta. Kondoo wengine wanafurahi kuwaunga mkono ndugu za Kristo kwa njia hiyo. Kondoo hao wanajua kwamba Yesu anaona mambo wanayofanya kwa ajili ya ndugu zake waliotiwa mafuta ni kana kwamba wanamfanyia yeye mwenyewe.​—Mt. 25:37-40.

13 Ni sababu gani nyingine ambazo zinatufanya sisi sote tuhudhurie Ukumbusho haidhuru tuna tumaini gani?

NDABA JAKI TWE TWABOA TUHUZULIA?

14. Yehova na Yesu butulangi bo upalani nkolongo?

14 Tunamshukuru Yehova na Yesu kwa ajili ya upendo ambao wametuonyesha. Yehova ametuonyesha upendo katika njia nyingi, lakini kuna njia moja ambayo ni ya pekee. Mungu wetu alionyesha upendo mkubwa wa kujidhabihu kwa kumtuma Mwana wake mpendwa ateseke na kufa kwa ajili yetu. (Yoh. 3:16) Pia, tunatambua kwamba Yesu alionyesha upendo mkubwa kwa kuwa tayari kutoa uhai wake kwa ajili yetu. (Yoh. 15:13) Hatuwezi kamwe kumlipa Yehova na Yesu kwa upendo ambao wametuonyesha. Lakini tunaweza kuonyesha shukrani zetu kupitia maisha yetu ya kila siku. (Kol. 3:15) Na tunahudhuria Ukumbusho ili tukumbuke upendo waliotuonyesha na pia kuonyesha kwamba tunawapenda.

15. Ndaba jaki akristo atiwa-mafuta na akakondoo bangi alangi kwamba athamini ngani zawadi ja fidia?

15 Tunathamini sana zawadi ya fidia. (Mt. 20:28) Watiwa-mafuta wanathamini fidia kwa sababu inafanya tumaini lao la pekee liwezekane. Kwa sababu ya imani yao katika dhabihu ya Kristo, Yehova amewatangaza kuwa waadilifu na amewafanya kuwa watoto wake. (Rom. 5:1; 8:15-17, 23) Kondoo wengine wanathamini pia fidia. Kwa msingi wa imani yao katika damu ya Kristo iliyomwagwa, wana msimamo safi mbele za Mungu, wanaweza kumtolea utumishi mtakatifu, na wana tumaini la ‘kutoka katika ile dhiki kuu.’ (Ufu. 7:13-15) Njia moja ambayo watiwa-mafuta na kondoo wengine wanaonyesha shukrani kwa ajili ya fidia ni kwa kuhudhuria Ukumbusho kila mwaka.

16. Jibi sababu bo jengi jejutufanya tuhuzulia Ukumbisho?

16 Sababu nyingine inayofanya tuhudhurie Ukumbusho ni kwamba tunataka kumtii Yesu. Haidhuru tumaini letu la wakati ujao, kila mmoja wetu anataka kutii amri hii ambayo Yesu alitoa jioni aliyoanzisha Ukumbusho: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”​—1 Kor. 11:23, 24.

JINSI TWE TWABOA ETUNUFAIKA KUKUHUZULIA

17. Ukumbushu gutujangati bo kunhegale Yehova ngane?

17 Tunamkaribia zaidi Yehova. (Yak. 4:8) Kama ambavyo tumejifunza, Ukumbusho unatupatia nafasi ya kufikiria tumaini ambalo Yehova ametupatia na kutafakari upendo mkubwa ambao ametuonyesha. (Yer. 29:11; 1 Yoh. 4:8-10) Tunapotafakari tumaini letu hakika la wakati ujao na upendo wa Mungu usioshindwa kwa ajili yetu, tunampenda Yehova hata zaidi na kuimarisha urafiki wetu pamoja naye.​—Rom. 8:38, 39.

18. Kutafakali mfanu guka Yesu kutuchoche tuhenga kike?

18 Tunachochewa kuiga mfano wa Yesu. (1 Pet. 2:21) Siku kadhaa kabla ya Ukumbusho, tunachunguza masimulizi ya Biblia kuhusu juma la mwisho la maisha ya Yesu duniani, kifo chake, na ufufuo wake. Kisha, siku ya Ukumbusho, hotuba inatukumbusha upendo wa Yesu kwa ajili yetu. (Efe. 5:2; 1 Yoh. 3:16) Tunaposoma kuhusu jinsi Yesu alivyojidhabihu na kutafakari mfano wake, tunachochewa “kutembea kama huyo alivyotembea.”​—1 Yoh. 2:6.

19. Tuwesa kudumu katika upendu guka Mungu jinsi bole?

19 Tunaazimia hata zaidi kudumu katika upendo wa Mungu. (Yuda 20, 21) Tunadumu katika upendo wa Mungu kwa kufanya yote tunayoweza ili kumtii, kulitakasa jina lake, na kufurahisha moyo wake. (Met. 27:11; Mt. 6:9; 1 Yoh. 5:3) Kuhudhuria Ukumbusho kunatuchochea kuazimia kuishi kila siku kwa njia inayomwonyesha Yehova kwamba tunataka kudumu katika upendo wake milele!

20. Tubi na sababu bo muhimu yukuhuzuli Ukumbusho?

20 Iwe tuna tumaini la kuishi milele mbinguni au duniani, tuna sababu nzuri za kuhudhuria Ukumbusho. Kila mwaka tunapokusanyika pamoja tarehe hiyo, tunakumbuka kifo cha mtu tunayempenda, Yesu Kristo. Zaidi ya yote, tunakumbuka tendo kubwa zaidi la upendo, yaani, upendo ambao Yehova alituonyesha kwa kumtoa Mwana wake awe fidia. Mwaka huu, Ukumbusho utafanywa jioni siku ya Ijumaa, Aprili 15, 2022. Tunampenda Yehova na Mwana wake, hivyo siku ya kukumbuka kifo cha Yesu, jambo muhimu zaidi kwetu litakuwa kuhudhuria Ukumbusho.

NHAMBU 16 Msifuni Yah kwa Mwana Wake Mtiwa Mafuta

^ Iwe tuna tumaini la kuishi mbinguni au katika dunia paradiso, kila mwaka tunatazamia kwa hamu kuhudhuria Ukumbusho. Katika makala hii, tutazungumzia sababu nzuri za Kimaandiko zinazoonyesha kwa nini tunahudhuria na faida tunazopata kwa kufanya hivyo.

^ Maneno haya yametafsiriwa “Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu” (Union Version).

^ Kwa habari zaidi kuhusu agano jipya na agano la Ufalme, tazama makala “Mtakuwa ‘Ufalme wa Makuhani’” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 2014, ukurasa wa 15-17.

^ UFAFANUZI WA MANENO: Neno mabaki linarejelea Wakristo watiwa-mafuta ambao bado wako duniani.

^ Kwa habari zaidi kuhusu unabii wa vijiti viwili unaopatikana kwenye Ezekieli sura ya 37, tazama kitabu Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!, ukurasa wa 130-135, fungu la 3-17.