Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA LIFUNZU 46

Mwaka Wenzi Anyai ba Ndoa​—Nndongulakya Mumaisha Utumishi Gwi Kuka Yehova

Mwaka Wenzi Anyai ba Ndoa​—Nndongulakya Mumaisha Utumishi Gwi Kuka Yehova

“Yehova ndo makili gango . . . Mwoju gwa guntumaini jwombi.”​—ZAB. 28:7.

NHAMBU 131 “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”

MUHTASARI *

1-2. (a) Kwa ndaba jaki wenzi anyai ba ndoa apaswa kuntumaini Yehova? (Zaburi 37:3, 4) (b) Musitusungusa ki mumakala jenzeno?

 JE, UNATAKA kufunga ndoa hivi karibuni, au umefunga ndoa hivi karibuni? Ikiwa ndivyo, hapana shaka unatazamia kwa hamu kufurahia maisha pamoja na mtu unayempenda sana. Bila shaka, ndoa ina changamoto zake, na kuna maamuzi muhimu yanayohitaji kufanywa. Jinsi mnavyokabiliana na changamoto hizo na maamuzi mnayofanya, itaathiri furaha yenu mkiwa wenzi kwa miaka mingi ijayo. Ikiwa mtamtegemea Yehova, mtafanya maamuzi yenye hekima, ndoa yenu itakuwa imara zaidi, na mtakuwa na furaha zaidi. Ikiwa mtashindwa kutumia ushauri wa Mungu, mtapata matatizo yatakayowaletea mkazo kwenye ndoa yenu, na hivyo mtakosa furaha.​—Soma Zaburi 37:3, 4.

2 Ingawa makala hii inazungumzia wenzi wapya wa ndoa, itazungumzia changamoto ambazo huenda wenzi wote wa ndoa wakakabiliana nazo. Itakazia mambo tunayoweza kujifunza kutokana na mifano iliyowekwa na baadhi ya wanaume na wanawake waaminifu katika Biblia. Mifano hiyo, inatufundisha mambo ambayo tunaweza kutumia katika nyanja mbalimbali za maisha yetu, kutia ndani ndoa. Pia, tutajifunza kutokana na mifano ya baadhi ya wenzi wa ndoa wa nyakati zetu.

IBI CHANGAMOTU BO AMBAYU WENZI ANYAI BA NDOA AWESA KUKABILE?

Ni maamuzi gani yanayoweza kuwazuia wenzi wapya wa ndoa kupanua utumishi wao kwa Yehova? (Tazama fungu la 3 na 4)

3-4. Pangi wenzi anyai ba ndoa awesa kukabili changamotu bole?

3 Huenda baadhi ya watu wakawatia moyo wenzi wapya wa ndoa waishi yale yanayoonwa kuwa maisha ya kawaida. Kwa mfano, huenda wazazi na watu wengine wa ukoo wakawashinikiza wenzi hao wapya wa ndoa waanze kupata watoto mara moja baada ya kufunga ndoa. Au rafiki na washiriki wa familia wenye nia nzuri huenda wakawahimiza wenzi wapya wa ndoa wanunue nyumba na kuijaza vitu vizuri.

4 Ikiwa hawatakuwa makini, huenda wenzi hao wapya wa ndoa wakafanya maamuzi ambayo yatawaingiza kwenye madeni yenye kulemea. Kisha, huenda mke na mume wakahitaji kufanya kazi kwa saa nyingi ili kulipia madeni hayo. Kazi ya kimwili inaweza kuanza kuchukua muda ambao wanapaswa kutumia katika funzo la Biblia la kibinafsi, ibada ya familia, na huduma. Huenda wenzi hao wapya wa ndoa hata wakakosa mikutano ili kufanya kazi muda wa ziada na kupata pesa zaidi au ili kuhakikisha kwamba hawapotezi kazi zao. Matokeo ni kwamba wanakosa fursa zenye kusisimua za kupanua utumishi wao kwa Yehova.

5. Gulibola ki kubokana nu mfanu guka Klaus na Marisa?

5 Mifano mingi inaonyesha kwamba kukazia maishani kupata vitu vya kimwili hakuleti furaha. Fikiria kile ambacho Klaus na Marisa, wenzi wa ndoa, walijifunza kuhusu hilo. * Mwanzoni mwa ndoa yao, wote wawili walifanya kazi ya muda wote ili waweze kuishi maisha yenye kustarehesha. Hata hivyo, moyoni hawakuwa na furaha ya kweli na kuridhika. Klaus anakiri hivi: “Tulikuwa na vitu vingi vya kimwili zaidi ya tulivyohitaji, lakini hatukuwa na malengo ya kiroho. Kusema kweli, maisha yalijaa mambo mengi na yalikuwa yenye mkazo.” Labda wewe pia umetambua kwamba kukazia fikira kupata vitu vya kimwili hakujakuletea furaha ya kweli. Ikiwa ndivyo, usivunjike moyo. Kuchunguza mifano mizuri ya wengine kunaweza kukusaidia ufanye mabadiliko yanayohitajika. Kwanza, acheni tuchunguze mambo ambayo waume wanaweza kujifunza kutokana na mfano wa Mfalme Yehoshafati.

NTUMAINIA YEHOVA KAMA MFALME YEHOSHAFATI

6. Kupatana nilishauli lelipatikana mu Methali 3:5, 6, Mfalme Yehoshafati jwashugulakya bo changamotu ngolongu jejwakabiliaje?

6 Enyi waume, je, nyakati nyingine mnahisi kulemewa na majukumu yenu? Ikiwa ndivyo, mnaweza kunufaika na mfano wa Mfalme Yehoshafati. Akiwa mfalme, Yehoshafati alikuwa anawajibika ilipohusu hali njema ya taifa zima. Alishughulikiaje wajibu huo wa pekee sana? Yehoshafati alifanya yote aliyoweza ili kuwalinda watu wote waliokuwa chini ya uangalizi wake. Alijenga ngome katika majiji ya Yuda na kukusanya wanajeshi hodari zaidi ya 1,160,000. (2 Nya. 17:12-19) Baadaye, Yehoshafati alikabili changamoto kubwa. Jeshi kubwa la Waamoni, Wamoabu, na wanaume wa eneo la milimani la Seiri walimtishia yeye, familia yake, na watu wake. (2 Nya. 20:1, 2) Yehoshafati alifanya nini? Alimwomba Yehova amsaidie na kumpa nguvu. Kufanya hivyo kulipatana na shauri lenye hekima linalopatikana kwenye Methali 3:5, 6. (Soma.) Sala ya unyenyekevu ya Yehoshafati, inayopatikana kwenye 2 Mambo ya Nyakati 20:5-12, inafunua jinsi alivyomtumaini sana Baba yake wa mbinguni mwenye upendo. Yehova alijibuje sala ya Yehoshafati?

7. Yehova jwajibwa bo sala jika Yehoshafati?

7 Yehova alizungumza na Yehoshafati kupitia Mlawi aliyeitwa Yahazieli. Yehova alisema hivi: “Simameni mahali penu, simameni tuli, muuone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu.” (2 Nya. 20:13-17) Kwa hakika, hiyo si njia ya kawaida ya kupigana vita! Hata hivyo, maagizo hayo hayakutoka kwa mwanadamu; yalitoka kwa Yehova. Akiwa anamtumaini kabisa Yehova, Yehoshafati alifanya kama alivyoambiwa. Yeye na watu wa Yuda walipoenda kukutana na adui, mbele ya kikosi chake aliwatanguliza waimbaji wasio na silaha, badala ya wanajeshi wenye uzoefu zaidi. Yehova hakumtamausha Yehoshafati; Alilishinda jeshi hilo la adui.​—2 Nya. 20:18-23.

Wenzi wapya wa ndoa wanaweza kutanguliza maishani utumishi wao kwa Yehova kwa kusali na kujifunza Neno lake (Tazama fungu la 8 na 10)

8. Akanalomi awesa kulibola ki kubokana numfanu guka Yehoshafati?

8 Enyi waume, mnaweza kujifunza kutokana na mfano wa Yehoshafati. Ni wajibu wenu kuhangaikia hali njema ya familia zenu, hivyo mnafanya kazi kwa bidii ili kuzilinda na kuzitegemeza familia zenu. Mnapokabili changamoto, huenda mkahisi kwamba mna uwezo wa kuishughulikia changamoto hiyo wenyewe. Hata hivyo, usitegemee nguvu zako mwenyewe. Badala yake, sali kibinafsi ili Yehova akusaidie. Pia, sali kwa bidii pamoja na mke wako. Tafuta mwongozo kutoka kwa Yehova kwa kujifunza Biblia na machapisho yanayoandaliwa na tengenezo la Mungu, na utumie shauri unalopata. Huenda wengine wasikubaliane na uamuzi unaofanya ambao unategemea Biblia, na hata huenda wakakuambia kwamba unatenda kipumbavu. Huenda wakasema kwamba pesa na vitu ambavyo inaweza kununua, ndivyo vitakavyoipatia ulinzi bora zaidi familia yako. Lakini kumbuka mfano wa Yehoshafati. Alimtumaini Yehova, na alithibitisha hilo kupitia matendo yake. Yehova hakumwacha mwanamume huyo mshikamanifu, naye hatakuacha wewe pia. (Zab. 37:28; Ebr. 13:5) Wenzi wa ndoa wanaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba wanakuwa na maisha yenye kuthawabisha pamoja?

KAMA NABII ISAYA NUNHANAMUNDU, NNDONGULAKYA MUMAISHA UTUMISHI GWI KUKA YEHOVA

9. Tuwesa kupwaga ki kuhusu nabii Isaya nu nhanamundo?

9 Nabii Isaya na mke wake walitanguliza maishani utumishi wao kwa Yehova. Isaya alikuwa nabii, na inawezekana kwamba mke wake alikuwa na migawo yake mwenyewe ya kinabii, kwa kuwa aliitwa “nabii wa kike.” (Isa. 8:1-4) Inaonekana kwamba wakiwa wenzi wa ndoa, Isaya na mke wake walikazia fikira ibada yao kwa Yehova. Waliwawekea mfano bora sana wenzi wa ndoa leo!

10. Kulibola unabii gwa Bibilia kuwesa kwajangati bo wenzi ba ndoa aazimia kuhenga goti gaawesa kwaajili jika Yehova?

10 Leo, wenzi wa ndoa wanaweza kutanguliza maishani utumishi wao kwa Yehova kwa kufanya yote wanayoweza katika utumishi wake. Wanaweza kuimarisha tumaini lao katika Yehova kwa kujifunza unabii wa Biblia pamoja, na kuona jinsi unavyotimia sikuzote. * (Tito 1:2) Wanaweza kutafakari kuhusu sehemu waliyo nayo katika utimizo wa unabii mbalimbali wa Biblia. Kwa mfano, wanaweza kushiriki katika kutimiza unabii wa Yesu kwamba habari njema itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kabla ya mwisho kufika. (Mt. 24:14) Kadiri wenzi wa ndoa wanavyokuwa na uhakika zaidi kwamba unabii wa Biblia unatimia, ndivyo watakavyoazimia hata zaidi kufanya yote wawezayo kwa ajili ya Yehova.

KAMA PRISILA NA AKILA, NNDONGULAKYA MUMAISHA MASILAI GUUFALME

11. Prisila na Akila bawesa kuhenga ki, na kwa ndaba jaki?

11 Wenzi wapya wa ndoa wanaweza kujifunza kutoka kwa Prisila na Akila, wenzi wa ndoa Wayahudi walioishi katika jiji la Roma. Walikuwa wamesikia habari njema kumhusu Yesu, na kuwa Wakristo. Bila shaka, waliridhika na maisha yao. Hata hivyo, maisha yao yalibadilika pasipo kutarajia wakati Maliki Claudio alipoamuru kwamba Wayahudi wote waondoke Roma. Fikiria hilo lilimaanisha nini kwa Akila na Prisila. Wangehitaji kuhama eneo walilolizoea, kuhamia nyumba mpya, na kuanzisha biashara yao ya kutengeneza mahema katika eneo jipya. Je, wangeruhusu mabadiliko hayo yawafanye wasiendelee kutanguliza masilahi ya Ufalme maishani? Bila shaka, unajua jibu la swali hilo. Wakiwa kwenye makao yao mapya huko Korintho, Akila na Prisila waliweza kushirikiana na kutaniko la huko, na kufanya kazi pamoja na mtume Paulo ili kuwaimarisha akina ndugu. Baadaye, walihamia katika miji mingine iliyokuwa na uhitaji mkubwa wa wahubiri. (Mdo. 18:18-21; Rom. 16:3-5) Bila shaka, walifurahia pamoja maisha hayo yenye kuridhisha sana!

12. Kwa ndaba jaki wenzi ba ndoa apaswa kulibeke malengu gikiloho?

12 Leo, wenzi wa ndoa wanaweza kuwaiga Prisila na Akila kwa kutanguliza maishani masilahi ya Ufalme. Muda bora zaidi wa kuzungumzia malengo yao maishani ni wakati wanapochumbiana. Wenzi wa ndoa wanapofanya maamuzi pamoja na kujitahidi kufikia malengo ya kiroho waliyoweka pamoja, wana fursa nyingi zaidi za kuona roho ya Yehova ikifanya kazi maishani mwao. (Mhu. 4:9, 12) Fikiria kisa cha Russell na Elizabeth. Russell anasema hivi: “Wakati wa uchumba, tulizungumzia kihususa malengo yetu ya kiroho.” Elizabeth anasema hivi: “Tulizungumzia jambo hilo ili baadaye tulipofanya maamuzi mbalimbali, tungehakikisha kwamba maamuzi yetu hayatuzuii kufikia malengo hayo.” Hali za Russell na Elizabeth ziliwaruhusu kuhamia Micronesia, ili kutumikia eneo lenye uhitaji mkubwa wa wahubiri.

Wenzi wapya wa ndoa wanaweza kutanguliza maishani utumishi wao kwa Yehova kwa kujiwekea malengo ya kiroho (Tazama fungu la 13)

13. Kulengana na Zaburi 28:7, twipata matokeu bo patuntumaini Yehova?

13 Kama Russell na Elizabeth, wenzi wengi wa ndoa wamefanya uamuzi wa kutojiingiza katika mambo mengi ambayo yanaweza kuwazuia kutumia muda mwingi zaidi katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Wenzi wa ndoa wanapojiwekea malengo mazuri katika utumishi wa Yehova na kushirikiana ili kuyafikia, watapata matokeo mzuri sana. Watajionea jinsi Yehova anavyowatunza, watamtumaini zaidi, na watakuwa na furaha ya kweli.​—Soma Zaburi 28:7.

KAMA MTUMI PETRO NU NHANAMUNDU, TUMAINIA AHADI IKA YEHOVA

14. Mtumi Petro nu nhanamundu balangia bo kwamba batumainia ahadi jejipatikana mu Mathayo 6:25, 31-34?

14 Wenzi wa ndoa wanaweza pia kujifunza kutokana na mfano uliowekwa na mtume Petro na mke wake. Miezi sita hadi mwaka mmoja hivi baada ya kukutana na Yesu kwa mara ya kwanza, mtume Petro alihitaji kufanya uamuzi muhimu. Petro alikuwa akiitegemeza familia yake kupitia biashara ya uvuvi. Hivyo, Yesu alipomwalika awe mfuasi wake wa wakati wote, Petro alihitaji kuzingatia hali ya familia yake. (Luka 5:1-11) Petro alichagua kuandamana na Yesu katika kazi yake ya kuhubiri. Alifanya uchaguzi wa hekima! Na tuna sababu nzuri ya kufikia mkataa kwamba mke wa Petro aliunga mkono uamuzi wake. Biblia inaonyesha kwamba baada ya Yesu kufufuliwa, alisafiri pamoja na Petro kwa angalau kipindi fulani cha wakati. (1 Kor. 9:5) Bila shaka, mfano wake mzuri akiwa mke Mkristo, ulimfanya Petro awe na uhuru wa usemi na kuandika shauri lililoongozwa na roho ya Mungu kwa ajili ya waume na wake Wakristo. (1 Pet. 3:1-7) Ni wazi kwamba Petro na mke wake walitumaini ahadi ya Yehova kwamba angewaandalia mahitaji yao ikiwa wangetafuta kwanza Ufalme maishani mwao.​—Soma Mathayo 6:25, 31-34.

15. Gulibola ki kubokana nilisimulizi lika Tiago na Esther?

15 Ikiwa ulifunga ndoa miaka michache iliyopita, unaweza kuendeleaje kusitawisha tamaa ya kupanua huduma yako? Njia moja ni kwa kujifunza kutokana na masimulizi ya wenzi wengine wa ndoa. Kwa mfano, unaweza kusoma mfululizo “Walijitoa Wenyewe kwa Hiari.” Makala hizo, zilimsaidia Tiago na Esther, wenzi wa ndoa kutoka Brazili, kusitawisha tamaa kubwa ya kutumikia kwenye eneo lenye uhitaji mkubwa wa wahubiri. Tiago anaeleza hivi: “Tuliposoma masimulizi kuhusu jinsi Yehova alivyowasaidia watumishi wake katika siku zetu, sisi pia tulitaka kuuona mkono wa Yehova ukituongoza na kututunza.” Hatimaye, walihamia Paraguai, ambako wamekuwa wakitumikia katika eneo la lugha ya Kireno tangu mwaka wa 2014. Esther anasema hivi: “Andiko moja ambalo sote tunalipenda sana ni Waefeso 3:20. Tena na tena tumejionea maneno hayo yakitimia katika utumishi wetu kwa Yehova.” Katika barua hiyo kwa Waefeso, Paulo aliahidi kwamba Yehova angetuandalia kwa wingi zaidi kupita mambo tunayoomba. Kwa kweli, ahadi hiyo imetimizwa mara nyingi!

Wenzi wapya wa ndoa wanaweza kutanguliza maishani utumishi wao kwa Yehova kwa kutafuta ushauri kutoka kwa ndugu na dada wakomavu (Tazama fungu la 16)

16. Wenzi ba ndoa akakombu awesa kuloba ushauli kuhuma kuka nya paachanganu malengu gabu mumaisha?

16 Leo, wenzi wa ndoa vijana wanaweza kunufaika kutokana na masimulizi ya wengine ambao wamejifunza kumtegemea Yehova. Baadhi ya wenzi wa ndoa huenda wametumikia kwa miaka mingi katika utumishi wa wakati wote. Kwa nini usiombe ushauri wao ikiwa unahisi unahitaji kuchanganua malengo yako? Hiyo ni njia nyingine ya kuonyesha kwamba unamtumaini Yehova. (Met. 22:17, 19) Wazee wa kutaniko pia wanaweza kuwasaidia wenzi wa ndoa vijana wajiwekee na kufikia malengo ya kiroho.

17. Kwabya bo kuka Klaus na Marisa, na tulibola ki kubokana na kisa sabo?

17 Hata hivyo, huenda nyakati nyingine uamuzi wa kupanua utumishi wetu usitimie kama tulivyotarajia. Fikiria mfano wa Klaus na Marisa, waliotajwa mapema. Miaka mitatu baada ya kufunga ndoa, walihama kutoka nyumbani na kujitolea katika kazi ya ujenzi kwenye ofisi ya tawi ya Finland. Hata hivyo, walijulishwa kwamba hawangeruhusiwa kukaa hapo kwa zaidi ya miezi sita. Mwanzoni, walivunjika moyo. Lakini muda mfupi baada ya hapo, walialikwa kuhudhuria darasa la kujifunza Kiarabu, na sasa wanatumikia kwa furaha katika nchi nyingine kwenye eneo ambalo watu wanazungumza Kiarabu. Anapokumbuka wakati huo, Marisa anakiri hivi: “Inaogopesha sana kufanya mambo ambayo hujawahi kufanya na kumtumaini Yehova kikamili. Lakini nimejionea jinsi sikuzote Yehova ametusaidia kwa njia ambazo hatukutarajia. Baada ya kujionea jambo hilo, sasa ninamtumaini zaidi Yehova.” Kama kisa hicho kinavyoonyesha, unaweza kuwa na hakika kwamba sikuzote Yehova atakuthawabisha ikiwa unamtumaini kabisa.

18. Wenzi ba ndoa awesa kuhenga ki Ili kuendale kuntumaini Yehova?

18 Ndoa ni zawadi kutoka kwa Yehova. (Mt. 19:5, 6) Anataka wenzi wa ndoa wafurahie zawadi hiyo. (Met. 5:18) Enyi wenzi wa ndoa vijana, kwa nini msichanganue jinsi mnavyotumia maisha yenu? Je, mnafanya yote mnayoweza ili kumwonyesha Yehova jinsi mnavyothamini zawadi ambazo amewapatia? Zungumzeni na Yehova katika sala. Tafuteni katika Neno lake kanuni zinazofaa hali yenu. Kisha mtumie ushauri ambao Yehova anawapatia. Muwe na hakika kwamba mtakuwa na maisha yenye furaha na kuridhisha ikiwa mtatanguliza kumtumikia Yehova katika ndoa yenu!

NHAMBU 132 Sasa Tumekuwa Mwili Mmoja

[Maelezo ya Chini]

^ ekichweka 5 Baadhi ya maamuzi tunayofanya yanaweza kuathiri muda na nguvu tunazoweza kutumia katika utumishi wa Yehova. Kihususa, wenzi wapya wa ndoa wanahitaji kufanya maamuzi ambayo yanaweza kuwa na matokeo ya muda mrefu maishani mwao. Makala hii, itawasaidia kufanya maamuzi yenye hekima yanayoongoza kwenye maisha yenye furaha na kusudi.

^ ekichweka 5 Baadhi ya majina yamebadilishwa.