Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA LIFUNZU 45

Nhendalya Kulangiana Upalani Nkamulane

Nhendalya Kulangiana Upalani Nkamulane

“Nnhengania kuupalani nkamulani na lehema.”​—ZEK. 7:9.

NHAMBU 107 Mungu Kielelezo cha Upendo

MUHTASARI *

1-2. Tubi na sababu bo yasapi yukulangiana upalani nkamulane?

 TUNA sababu nzuri za kuonyeshana upendo mshikamanifu. Sababu zipi hizo? Ona jinsi methali zifuatazo zilizoongozwa na roho ya Mungu zinavyojibu swali hilo: “Usiruhusu upendo mshikamanifu na uaminifu zikuache. . . . Ndipo utakapopata kibali na ufahamu mzuri machoni pa Mungu na wanadamu.” “Mtu mwenye upendo mshikamanifu hujinufaisha.” “Yeyote anayefuatia uadilifu na upendo mshikamanifu atapata uzima.”​—Met. 3:3, 4; 11:17, maelezo ya chini; 21:21.

2 Methali hizo zinataja sababu tatu kwa nini tunapaswa kuonyesha upendo mshikamanifu. Kwanza, kuonyesha upendo mshikamanifu kunatufanya tuwe wenye thamani machoni pa Mungu. Pili, kwa kuonyesha upendo mshikamanifu tunajinufaisha sisi wenyewe. Kwa mfano, tunakuwa na urafiki unaodumu pamoja na wengine. Tatu, kufuatia upendo mshikamanifu kunaongoza kwenye baraka za wakati ujao, kutia ndani uzima wa milele. Kwa kweli, tuna sababu nzuri za kufuata kikumbusho hiki cha Yehova: “Mtendeane kwa upendo mshikamanifu na rehema.”​—Zek. 7:9.

3. Musitusungusa maswali bo mumakala jenzeno?

3 Katika makala hii, tutachunguza majibu ya maswali manne. Tunapaswa kuwaonyesha nani upendo mshikamanifu? Tunaweza kujifunza nini kutoka kwenye kitabu cha Ruthu kuhusu kuonyesha upendo mshikamanifu? Tunaweza kuonyeshaje upendo mshikamanifu leo? Wale wanaoonyesha upendo mshikamanifu wanapata faida gani?

TUPASWA KWALANGI AKANYA UPALANI NKAMULANE?

4. Tuwesa kunziga bo Yehova katika kulangi upalani nkamulane? (Marko 10:29, 30)

4 Kama tulivyojifunza katika makala iliyotangulia, Yehova anawaonyesha upendo mshikamanifu—hisia zake zinazodumu za upendo, zinazoshikamana na mtu—wale wanaompenda na kumtumikia. (Dan. 9:4) Tunataka kuwa “waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.” (Efe. 5:1) Hivyo, tunatamani kusitawisha hisia nyororo za upendo kwa ndugu na dada zetu wa kiroho, yaani, upendo wenye kina unaodumu na kushikamana na mtu.​—Soma Marko 10:29, 30.

5-6. Kwa kawaida linenu “ukamulani” limaanisha kike?

5 Bila shaka, utakubali kwamba kadiri tunavyoelewa zaidi maana ya upendo mshikamanifu, ndivyo tutakavyoweza kuwaonyesha kwa njia nzuri zaidi upendo huo mshikamanifu waabudu wenzetu. Ili kuuelewa zaidi upendo mshikamanifu, acheni tuulinganishe na sifa ya ushikamanifu katika muktadha unaotumiwa na wengi. Fikiria mfano huu.

 6 Leo, tunaweza kumfafanua mtu fulani ambaye amefanya kazi katika kampuni ileile kwa miaka mingi, kuwa mfanyakazi mshikamanifu. Hata hivyo, katika miaka yake yote pamoja na kampuni hiyo, huenda hajawahi kuonana na wakurugenzi wa kampuni hiyo. Huenda si nyakati zote atakubaliana na sera za kampuni hiyo. Na si kwamba anaipenda kampuni hiyo, lakini anafurahi kwamba ana kazi inayompatia mshahara. Ataendelea kufanya kazi na kampuni hiyo hadi atakapostaafu au hadi atakapopata kazi nzuri zaidi mahali pengine.

7-8. (a) Kibi ki sesunchoche mundu kulangi upalani nkamulane? (b) Kwa ndaba jaki twisungusa baazi jimistali mukitabu sika Ruthu?

7 Tofauti kati ya ushikamanifu unaotajwa kwenye  fungu la 6, na upendo mshikamanifu ni nia ya mtu. Katika Biblia, matendo ya upendo mshikamanifu miongoni mwa watu wa Mungu yalichochewa na jambo gani hasa? Wale walioonyesha upendo mshikamanifu, walifanya hivyo si kwa sababu walilazimika kufanya hivyo, bali kwa sababu walichochewa kutoka moyoni. Fikiria mfano wa Daudi. Moyo wake ulimchochea kumwonyesha upendo mshikamanifu Yonathani, rafiki yake mpendwa, hata ingawa baba ya Yonathani alitaka kumuua Daudi. Miaka mingi baada ya Yonathani kufa, Daudi aliendelea kumwonyesha upendo mshikamanifu Mefiboshethi, mwana wa Yonathani.​—1 Sam. 20:9, 14, 15; 2 Sam. 4:4; 8:15; 9:1, 6, 7.

8 Tunaweza kujifunza mengi kuhusu upendo mshikamanifu kwa kuchunguza baadhi ya mistari katika kitabu cha Biblia cha Ruthu. Tunaweza kujifunza mambo gani kuhusu upendo mshikamanifu kutokana na watu wanaotajwa katika kitabu hicho? Tunaweza kutumiaje mambo hayo katika kutaniko letu? *

KI SETUWESA KULIBOLA KUHUMA MUKITABU SIKA RUTHU KUHUSU KULANGI UPALANI NKAMULANE?

9. Kwa ndaba jaki Naomi jwahikila nkataa kwamba Yehova jwabya antenda kumpenga?

9 Katika kitabu cha Ruthu, tunasoma kuhusu Naomi, Ruthu, binti mkwe wake, na mwanamume aliyemwogopa Mungu aliyeitwa Boazi, ambaye alikuwa mtu wa ukoo wa mume wa Naomi. Kwa sababu ya njaa iliyotokea Israeli, Naomi, mume wake, na wana wao wawili walihamia Moabu. Wakiwa huko, mume wa Naomi alikufa. Wana wake wawili walioa, lakini inasikitisha kwamba wao pia walikufa. (Rut. 1:3-5; 2:1) Matatizo hayo yalimfanya Naomi akate tamaa hata zaidi. Alilemewa sana na hisia za uchungu hivi kwamba akafikia mkataa kwamba Yehova alikuwa akimpinga. Ona jinsi alivyoeleza hisia zake kumhusu Mungu. Alisema hivi: “Mkono wa Yehova umegeuka dhidi yangu, Mweza-Yote amefanya maisha yawe machungu sana kwangu.” Pia aliongeza hivi: “Yehova ndiye aliyenipinga na Mweza-Yote ndiye aliyeniletea msiba.”​—Rut. 1:13, 20, 21.

10. Yehova jwahenga bo pajwajogwa manenu guusungu gika Naomi?

10 Yehova alitendaje aliposikia maneno ya uchungu ya Naomi? Hakumwacha mtumishi wake huyo aliyevunjika moyo. Badala yake, alimwonyesha hisia mwenzi. Yehova anaelewa kwamba “ukandamizaji unaweza kumfanya mtu mwenye hekima ashikwe na wazimu.” (Mhu. 7:7) Hata hivyo, bado Naomi alihitaji msaada ili kuona kwamba Yehova alikuwa upande wake. Mungu alimwandalia msaada gani? (1 Sam. 2:8) Alimchochea Ruthu amsaidie Naomi na kumwonyesha upendo mshikamanifu. Kwa utayari na upole, Ruthu alimsaidia mama mkwe wake arudie hali nzuri kihisia na kiroho. Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Ruthu?

11. Kwa ndaba jaki aka ndugu na dada baabi na fazili bajangati baataabika?

11 Upendo mshikamanifu unatuchochea tuwasaidie wanaotaabika. Leo, kama tu Ruthu alivyoshikamana na Naomi, ndugu na dada wenye fadhili wako tayari kushikamana na wenye huzuni au walioshuka moyo. Wanawapenda ndugu na dada zao, na wanatamani kufanya yote wanayoweza ili kuwasaidia. (Met. 12:25, maelezo ya chini; 24:10) Hilo linapatana na himizo hili la mtume Paulo: “Wafarijini wale walioshuka moyo, wasaidieni walio dhaifu, iweni na subira kwa watu wote.”​—1 The. 5:14.

Unaweza kumsaidia ndugu au dada aliyevunjika moyo kwa kumsikiliza (Tazama fungu la 12)

12. Mala yingi jibi indela bo jejibi jasapi ngani jukunzangati ndugu au dada jojutunwiki mwojo?

12 Mara nyingi njia nzuri zaidi unayoweza kumsaidia ndugu au dada aliyevunjika moyo, ni kwa kumsikiliza na kumhakikishia kwamba unampenda. Unapomkazia uangalifu kondoo wa Yehova mwenye thamani, Mungu wetu anaona jambo hilo. (Zab. 41:1) Methali 19:17 inasema: “Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, naye Atamlipa kwa anayotenda.”

Ruthu anashikamana na Naomi, mama mkwe wake, huku Orpa akirudi Moabu. Ruthu anamwambia hivi Naomi: “Mahali utakapoenda nitaenda.” (Tazama fungu la 13)

13. Ruthu na Orpa bahenga kwiindela bo tofauti, na kwa ndaba jaki uamuzi guka Ruthu gwabya litendu luupalani nkamulane? (Linga picha pilijalada.)

13 Tunajifunza mengi zaidi kuhusu upendo mshikamanifu kwa kuchunguza mambo ambayo Naomi alipitia baada ya kifo cha mume wake na wana wake wawili. Naomi alipotambua kwamba “Yehova alikuwa amewaelekezea uangalifu watu Wake kwa kuwapa chakula,” aliamua kurudi nyumbani. (Rut. 1:6) Binti zake wakwe walianza safari hiyo pamoja naye. Hata hivyo, wakiwa njiani, mara tatu Naomi aliwahimiza wanawake hao warudi Moabu. Nini kilichotokea? Tunasoma hivi: “Orpa akambusu mama mkwe wake na kwenda zake. Lakini Ruthu akashikamana naye.” (Rut. 1:7-14) Kwa kuchagua kurudi, Orpa alifuata maagizo ya Naomi, alifanya jambo alilotarajiwa afanye. Hata hivyo, Ruthu alifanya mengi zaidi ya hayo. Alikuwa huru kurudi, lakini kwa sababu ya upendo mshikamanifu, aliamua kubaki ili kumsaidia Naomi aliyekuwa na uhitaji. (Rut. 1:16, 17) Ruthu alichagua kushikamana na Naomi, si kwa sababu alilazimika kufanya hivyo, bali kwa sababu alitaka kufanya hivyo. Uamuzi wa Ruthu ulikuwa tendo la upendo mshikamanifu wa kweli. Tunajifunza nini kutokana na simulizi hilo?

14. (a) Lelenu, akandugu na dada baabi nuupalani ahenga uamuzi bole? (b) Kulengana na Waebrania 13:16, ibi zabihu ya aina bo yeyumfa Mungo?

14 Upendo mshikamanifu unapita kile kinachotarajiwa. Leo, kama ilivyokuwa zamani, ndugu na dada zetu wengi wamechagua kuwaonyesha upendo mshikamanifu waamini wenzao, hata wale ambao hawawajui kibinafsi. Kwa mfano, wanaposikia kwamba janga la asili limetokea, haraka wanataka kujua jinsi wanavyoweza kusaidia. Mtu fulani kutanikoni anapokabili hali ngumu ya kiuchumi, wanawasiliana naye ili kujua jinsi wanavyoweza kumsaidia kwa njia hususa. Kama Wamakedonia wa karne ya kwanza, wanafanya mengi zaidi ya kinachotarajiwa. Wanajidhabihu kibinafsi, wakitoa hata “kupita uwezo wao” ili kuwasaidia ndugu zao waliopatwa na hali ngumu. (2 Kor. 8:3) Ni lazima Yehova anapendezwa sana na roho hiyo ya upendo!​—Soma Waebrania 13:16.

TUWESA KULANGI BO UPALANI NKAMULANI LELENO?

15-16. Ruthu jwalangia bo kwamba ngasejwakatiki tamaa?

15 Tunaweza kujifunza mambo mengi mazuri kwa kuchunguza jinsi Ruthu alivyomsaidia Naomi. Acheni tuzungumzie machache kati ya hayo.

16 Endelea kusisitiza. Ruthu alipojitolea kuandamana na mama mkwe wake kuelekea Yuda, mwanzoni Naomi alikataa. Lakini Ruthu aliendelea kusisitiza. Matokeo yalikuwaje? “Naomi alipoona kwamba Ruthu anasisitiza kwenda naye, hakuendelea kumsihi asimfuate.”​—Rut. 1:15-18.

17. Kibi ki sesatujangatya twikata tamaa kanyata?

17 Somo: Subira inahitajika ili kuwasaidia wale walioshuka moyo, lakini hatupaswi kukata tamaa. Huenda mwanzoni dada aliye na uhitaji akakataa msaada wetu. * Hata hivyo, upendo mshikamanifu utatuchochea kufanya yote tunayoweza ili kushikamana naye. (Gal. 6:2) Tunatumaini kwamba mwishowe atakubali msaada wetu na kuturuhusu tumfariji ili apunguze huzuni yake.

18. Lasima libi lijambu bo lelunhumisa Ruthu?

18 Usikwazike. Naomi na Ruthu walipowasili Bethlehemu, Naomi alikutana na jirani zake wa zamani. Aliwaambia hivi: “Mikono yangu ilikuwa imejaa nilipoenda, lakini Yehova amenifanya nirudi mikono mitupu.” (Rut. 1:21) Wazia jinsi ambavyo lazima Ruthu alihisi aliposikia maneno hayo kutoka kwa Naomi! Ruthu alikuwa amefanya yote aliyoweza ili kumsaidia Naomi. Ruthu alikuwa amelia pamoja naye, alikuwa amemfariji, na alikuwa ametembea pamoja naye kwa siku nyingi. Licha ya hayo yote, Naomi alisema: “Yehova amenifanya nirudi mikono mitupu.” Kwa maneno hayo, Naomi hata hakuonyesha kwamba Ruthu aliyekuwa amesimama kando yake, alimtegemeza. Ni lazima jambo hilo lilimuumiza sana Ruthu! Hata hivyo, alishikamana na Naomi.

19. Ndo ki sesatujangatya kukamulana na ndugu au dada jojutaabika?

19 Somo: Leo, huenda mwanzoni dada anayetaabika akazungumza nasi kwa njia inayoumiza, licha ya jitihada zetu zote za kumsaidia. Lakini tunajitahidi kutokwazika. Tunashikamana na dada yetu mwenye uhitaji na tunamwomba Yehova atusaidie kupata njia ya kumfariji.​—Met. 17:17.

Leo, wazee Wakristo wanaweza kumwigaje Boazi? (Tazama fungu la 20 na 21

20. Kibi ki sesumpekia Ruthu makili gajwapala Ili kuendale kunzangati Naomi?

20 Toa kitia-moyo kwa wakati unaofaa. Ruthu alikuwa amemwonyesha upendo mshikamanifu Naomi, lakini sasa Ruthu mwenyewe alihitaji kitia-moyo. Na Yehova alimchochea Boazi amtie moyo. Boazi alimwambia hivi Ruthu: “Yehova na akuthawabishe kwa yale uliyofanya, na upate malipo kamili kutoka kwa Yehova Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kutafuta kimbilio chini ya mabawa yake.” Maneno hayo yenye kugusa moyo yalimfariji sana Ruthu. Ruthu alimjibu hivi Boazi: “Umenifariji na kunitia moyo.” (Rut. 2:12, 13) Maneno hayo yaliyosemwa na Boazi kwa wakati unaofaa yalimpa Ruthu nguvu alizohitaji ili aendelee kumsaidia Naomi.

21. Kama eafafanu mu Isaya 32:1, 2, azee bilikutaniku ba ajali bihenga kike?

21 Somo: Wale wanaowaonyesha wengine upendo mshikamanifu, nyakati nyingine wao pia huhitaji kitia-moyo. Kama tu Boazi alivyomhakikishia Ruthu kwamba fadhili aliyoonyesha ilithaminiwa, leo wazee wa kutaniko walio makini wanaonyesha wanathamini kutoka moyoni msaada ambao ndugu na dada wenye upendo wanatoa. Pongezi hizo za kutoka moyoni zinazotolewa kwa wakati unaofaa, zitawapa ndugu na dada nguvu wanazohitaji ili kuendelea kutoa msaada.​—Soma Isaya 32:1, 2.

BA ALANGI UPALANI NKAMULANI ANUFAIKA BOLE?

22-23. Ntazamu guka Naomi gwabadilika jinsi bo, na kwa ndaba jakike? (Zaburi 136:23, 26)

22 Baada ya muda fulani kupita, Boazi alimpatia Ruthu na Naomi zawadi kubwa ya chakula. (Rut. 2:14-18) Naomi aliitikiaje ukarimu wa Boazi? Alisema hivi: “Na abarikiwe na Yehova, ambaye hajawahi kamwe kukosa kuwatendea kwa upendo mshikamanifu walio hai na waliokufa.” (Rut. 2:20a) Mtazamo wa Naomi ulikuwa umebadilika kabisa! Mwanzoni, alikuwa amelia hivi kwa uchungu: “Yehova ndiye aliyenipinga,” lakini sasa alisema hivi kwa shangwe, “Yehova . . . hajawahi kamwe kukosa kuwatendea kwa upendo mshikamanifu walio hai na waliokufa.” Huenda ni nini kilichomsaidia Naomi abadili mtazamo wake?

23 Hatimaye, Naomi alianza kuona mkono wa Yehova katika maisha yake. Yehova alikuwa amemtumia Ruthu ampe utegemezo aliohitaji katika safari yake kuelekea Yuda. (Rut. 1:16) Pia, Naomi aliona mkono wa Yehova pindi Boazi, aliyekuwa kati ya ‘watu wanaoweza kuwakomboa,’ alipowapatia kwa ukarimu chakula wanawake hao wawili. * (Rut. 2:19, 20b) Huenda aliwaza hivi, ‘Sasa ninaelewa kwamba Yehova hakuniacha kamwe. Amekuwa pamoja nami wakati huu wote!’ (Soma Zaburi 136:23, 26.) Ni lazima Naomi alikuwa mwenye shukrani sana kwamba Ruthu na Boazi hawakukata tamaa! Tunaweza kuwazia jinsi wote watatu walivyoshangilia, Naomi alipopata tena shangwe na nguvu za kumtumikia Yehova.

24. Kwa ndaba jaki tupala kuendale kwalangi upalani nkamulani aabudu ajito?

24 Tumejifunza nini katika kitabu cha Ruthu kuhusu upendo mshikamanifu? Upendo mshikamanifu unatuchochea tusikate tamaa haraka inapohusu ndugu na dada zetu wanaotaabika. Pia, unatuchochea tujidhabihu ili kuwasaidia. Kwa wakati unaofaa, wazee wa kutaniko wanahitaji kuwatia moyo kutoka moyoni wale wanaowaonyesha wengine upendo mshikamanifu. Tunapowaona wale walio na uhitaji wakirudia hali nzuri ya kiroho tunapata shangwe kubwa. (Mdo. 20:35) Hata hivyo, sababu muhimu zaidi inayotufanya tuendelee kuonyesha upendo mshikamanifu ni ipi? Ni kwa sababu tunataka kumwiga na kumpendeza Yehova ambaye ana “upendo mwingi mshikamanifu.”​—Kut. 34:6; Zab. 33:22.

NHAMBU 130 Uwe Mwenye Kusamehe

[Maelezo ya Chini]

^ ekichweka 5 Yehova anataka tuwaonyeshe upendo mshikamanifu ndugu na dada zetu kutanikoni. Tunaweza kuongeza kina cha uelewaji wetu kuhusu maana ya upendo mshikamanifu kwa kuchunguza jinsi baadhi ya watumishi wa Mungu wa wakati uliopita walivyoonyesha sifa hiyo. Katika makala hii, tutachunguza mambo tunayoweza kujifunza kutokana na kielelezo cha Ruthu, Naomi, na Boazi.

^ ekichweka 8 Ili kunufaika kikamili na makala hii, tunakutia moyo usome kibinafsi sura ya 1 na ya 2 ya kitabu cha Ruthu.

^ ekichweka 17 Tunawarejelea akina dada wenye uhitaji kwa sababu tunazungumzia mfano wa Naomi. Lakini mambo tunayojifunza katika makala hii yanawahusu pia akina ndugu.

^ ekichweka 23 Kwa habari zaidi kuhusu jukumu la Boazi akiwa mkombozi, tazama makala “Igeni Imani Yao​—‘Mwanamke Bora,’” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 2012 ukurasa wa 20.