Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA LIFUNZU 41

Tuntumiki Mungu Jojubi “Tajili Katika Rehema”

Tuntumiki Mungu Jojubi “Tajili Katika Rehema”

“Yehova jubi mwema kwa boa, na rehema yaki ibonikana katika kasi yake yote.”​—ZAB. 145:9, NWT.

NHAMBU 44 Sala ya Mtu wa Hali ya Chini

MUHTASARI *

1. Pangi tukawasila ki patunholale mundu muna rehema?

 TUNAPOMFIKIRIA mtu mwenye rehema, huenda tukamwazia mtu mwenye fadhili, mchangamfu, mwenye huruma, na mkarimu. Huenda tukakumbuka simulizi la Yesu kuhusu Msamaria mwema. Mwanamume huyo wa taifa lingine, alimtendea kwa rehema, Myahudi ambaye alivamiwa na wezi. Msamaria huyo ‘alimsikitikia’ Myahudi aliyeumizwa na kwa upendo akafanya mipango ili atunzwe. (Luka 10:29-37) Mfano huo unakazia sifa maridadi ya Mungu wetu—rehema. Mungu anatuonyesha rehema kwa sababu anatupenda, naye huonyesha sifa hiyo kila siku kupitia anavyoshughulika nasi.

2. Sifa ja rehema jiwesa kuonyeshwa kwi indela bo jenge?

2 Kuna njia nyingine ambayo mtu anaweza kuonyesha rehema. Inahusisha kutomwadhibu mkosaji kunapokuwa na msingi wa kufanya hivyo. Kwa kweli kwa njia hiyo, Yehova ametuonyesha sisi rehema. Mtunga Zaburi alisema hivi: “Hajatutendea kulingana na dhambi zetu.” (Zab. 103:10) Hata hivyo, nyakati nyingine huenda Yehova akatoa nidhamu thabiti kwa mkosaji.

3. Msitusungusa maswali bole?

3 Katika makala hii, tutazungumzia maswali matatu: Kwa nini Yehova huonyesha rehema? Je, kuna uhusiano kati ya nidhamu thabiti na rehema? Na ni nini kinachoweza kutusaidia kuonyesha rehema? Acheni tuone jinsi Neno la Mungu linavyojibu maswali hayo.

NDABA JAKI YEHOVA JULANGI REHEMA?

4. Ndaba jaki Yehova julangi rehema?

4 Yehova anapenda kuonyesha rehema. Mtume Paulo aliandika kwamba Mungu ni “tajiri katika rehema.” Katika muktadha huo, Paulo alikuwa akirejelea rehema ya Mungu aliyoonyesha kwa kuwapa tumaini la kuishi mbinguni, watumishi wake watiwa-mafuta wasio wakamilifu. (Efe. 2:4-7) Lakini rehema ya Yehova ni pana hata zaidi. Mtunga Zaburi Daudi aliandika hivi: “Yehova ni mwema kwa wote, na rehema zake zinaonekana katika kazi zake zote.” (Zab. 145:9) Kwa kuwa Yehova anawapenda watu, anaonyesha rehema kila wakati anapoona kuna msingi wa kufanya hivyo.

5. Yesu julibola bo kuhusu rehema jika Yehova?

5 Zaidi ya mtu mwingine yeyote, Yesu anajua jinsi ambavyo Yehova anapenda kuonyesha rehema. Baba na Mwana wake walikuwa pamoja mbinguni kwa maelfu ya miaka ya historia ya wanadamu. (Met. 8:30, 31) Katika pindi nyingi mbalimbali, Yesu aliona jinsi Baba yake alivyowaonyesha rehema wanadamu watenda dhambi. (Zab. 78:37-42) Katika mafundisho yake, mara nyingi Yesu alikazia sifa hiyo yenye kuvutia ya Baba yake.

Baba hakumdhalilisha mwana wake mpotevu, alimkaribisha nyumbani (Tazama fungu la 6) *

6. Yesu jwatumia mfanu bo kutujangati kuelegwa rehema ja Ahengo bake?

6 Kama ilivyotajwa katika makala iliyotangulia, Yesu alitumia mfano wa mwana mpotevu ili kutusaidia tuelewe jinsi Yehova anavyopenda kuonyesha rehema. Mwana huyo aliondoka nyumbani na ‘kutumia vibaya mali yake kwa kuishi maisha ya anasa.’ (Luka 15:13) Baadaye, alitubu mwenendo wake mpotovu, akajinyenyekeza, na kurudi nyumbani. Baba yake angetendaje? Kijana huyo hakuhitaji kusubiri muda mrefu ili kujua. Yesu alisema hivi: “[Mwana huyo] akiwa mbali, baba yake akamwona na kumsikitikia, akakimbia, akamkumbatia na kumbusu kwa wororo.” Baba huyo hakumdhalilisha mwana wake. Badala yake, kwa rehema alimsamehe na kumkaribisha tena nyumbani. Mwana huyo mpotevu alikuwa ametenda dhambi kubwa, lakini kwa msingi wa toba yake, baba yake alimsamehe. Katika mfano huo, Yehova anafananishwa na baba huyo mwenye rehema. Kwa njia hiyo yenye kugusa moyo, Yesu anaonyesha utayari wa Baba yake wa kuwasamehe watenda dhambi wanaotubu kikweli.​—Luka 15:17-24.

7. Hekima jika Yehova jibonikana bo kupete jinsi ejulangi rehema?

7 Yehova huonyesha rehema kwa sababu ya hekima yake isiyo na kifani. Hekima ya Yehova si sifa inayohusisha tu akili bila hisia. Badala yake, Biblia inasema kwamba “hekima inayotoka juu” ni “yenye kujaa rehema na matunda mema.” (Yak. 3:17) Kama mzazi mwenye upendo, Yehova anajua kwamba rehema yake inawanufaisha watoto wake. (Zab. 103:13; Isa. 49:15) Rehema ya Mungu inawapa tumaini licha ya kutokamilika kwao. Hivyo, hekima ya Yehova isiyo na kifani inamchochea kuonyesha rehema wakati wowote anapoona kuna msingi wa kufanya hivyo. Wakati huohuo, Yehova anajua wakati wa kutoonyesha rehema. Kwa hekima, Yehova haonyeshi kamwe rehema ikiwa kufanya hivyo kutamaanisha kwamba anaachilia makosa ya mtenda dhambi.

8. Wakati gongi jibi hatua bo muhimu jejipaswa kujijukua, na ndaba jakike?

8 Tuseme mtumishi wa Mungu anaamua kuishi maisha mapotovu kimakusudi. Tunapaswa kufanya nini? Mtume Paulo akiongozwa na roho ya Mungu aliandika hivi: “Mwache kushirikiana” naye. (1 Kor. 5:11) Watenda dhambi wasiotubu hutengwa na ushirika wa kutaniko. Hatua hiyo ni muhimu ili kuwalinda ndugu na dada zetu waaminifu na kufuata njia takatifu za Yehova. Hata hivyo, baadhi ya watu hufikiri kwamba mtu anapotengwa na ushirika, Mungu hakumwonyesha rehema. Je, ni kweli? Acheni tuone.

BO, NIDHAMU THABITI JIWESA KUBA JINA REHEMA?

Kondoo anapokuwa mgonjwa huenda akatenganishwa na wengine, lakini bado ananufaika na utunzaji wa mchungaji (Tazama fungu la 9 hadi 11)

9-10. Kulengana na Waebrania 12:5, 6, ndaba jaki tuwesa kupwaga kwamba mpangu gu kutenga nu ushilika gubi uwonyeshu gwa rehema? Pia mfanu.

9 Tunaposikia tangazo kwenye mkutano wa Kikristo kwamba mtu fulani tunayemjua na kumpenda “si mmoja wa Mashahidi wa Yehova tena,” tunahuzunika sana. Huenda tukajiuliza ikiwa ilikuwa lazima kwa mpendwa wetu kutengwa na ushirika. Je, kweli kutenga na ushirika ni wonyesho wa rehema? Ndiyo. Kutomtia nidhamu mtu anayeihitaji, si jambo la hekima, lenye rehema, au upendo. (Met. 13:24) Je, kumtenga na ushirika kunaweza kumsaidia mtenda dhambi asiyetubu abadili mwenendo wake? Ndiyo. Wengi walioanguka katika dhambi nzito wamejionea kwamba hatua thabiti ambayo wazee walichukua, iliwasukuma na kuwasaidia warudiwe na fahamu, wabadili mwenendo wao, na wakarudi kwenye mikono ya Yehova yenye upendo.​—Soma Waebrania 12:5, 6.

10 Fikiria mfano huu. Mchungaji anatambua kwamba kondoo wake mmoja ni mgonjwa. Anajua kwamba ili kutibu ugonjwa wa kondoo wake anahitaji kumtenga kondoo huyo na kondoo wengine. Hata hivyo, kondoo wanapenda kuwa pamoja. Huenda wakahangaika na kukosa utulivu wanapotengwa na kondoo wengine. Hata hivyo, je, inamaanisha kwamba mchungaji ni katili au anatenda kwa ukali kwa kumtenga kondoo huyo na wengine? Bila shaka, la. Anajua kwamba ikiwa atamruhusu kondoo huyo achangamane na kondoo wengine, ugonjwa utaenea. Kwa kumtenga kondoo mgonjwa, analilinda kundi zima.​—Linganisha Mambo ya Walawi 13:3, 4.

11. (a) Kubi katika indela bo mundu joantengiki nu ushilika juwesa kulengana ni ling’oi ligonzo? (b) Babatengiki nu ushilika awesa kupata maandalizi nu nsaada bole?

11 Mkristo anapotengwa na ushirika, tunaweza kumfananisha na kondoo mgonjwa. Yeye ni mgonjwa katika maana ya kiroho. (Yak. 5:14) Kama magonjwa mengine, ugonjwa wa kiroho unaweza kuambukiza kwa urahisi. Hivyo, katika visa fulani ni muhimu kumtenga na kutaniko mtu ambaye ni mgonjwa kiroho. Nidhamu hiyo ni wonyesho wa upendo wa Yehova kwa washiriki waaminifu wa kundi Lake, na huenda ikaugusa moyo wa mtenda dhambi na kumfanya atubu. Akiwa ametengwa na ushirika, anaweza kuhudhuria mikutano, mahali ambapo anaweza kulishwa na kuimarishwa kiroho. Pia, yuko huru kupokea machapisho kwa ajili ya matumizi yake binafsi na kutazama JW Broadcasting®. Na wazee wanapoendelea kuchunguza maendeleo yake, huenda mara kwa mara wakampatia shauri la kibinafsi na mwongozo utakaomsaidia arudishe uhusiano wake pamoja na Yehova ili aweze kurudishwa na kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova tena. *

12. Lijambu bo lina upalani na rehema ambalu azee awesa kuhenga kwa ajili jika ntenda dhambi jwangakutubo?

12 Ni muhimu kukumbuka kwamba watenda dhambi wasiotubu ndio wanaotengwa na ushirika. Wazee wanajua kwamba kutenga na ushirika ni jambo zito, ambalo hawalichukulii kivivi hivi. Wanajua kwamba Yehova hutoa nidhamu “kwa kiwango kinachofaa.” (Yer. 30:11) Wanawapenda ndugu zao na hawataki kufanya jambo lolote litakalowasababishia madhara ya kiroho. Hata hivyo, pindi fulani, njia ya kumwonyesha mtenda dhambi upendo na rehema ni kumwondoa kutanikoni kwa kipindi fulani cha wakati.

13. Ndaba jaki Mkristo fulani ju Kukorintho jwahitajia kutengwa nu ushilika?

13 Fikiria jinsi mtume Paulo alivyoshughulika na mtenda dhambi asiyetubu katika karne ya kwanza. Mkristo fulani huko Korintho, alikuwa akifanya uasherati na mke wa baba yake. Jambo lenye kushtua sana! Kuhusu jambo hilo, Yehova alikuwa amewaambia hivi Waisraeli wa kale: “Mwanamume anayefanya ngono na mke wa baba yake amemwaibisha baba yake. Ni lazima wote wawili wauawe.” (Law. 20:11) Bila shaka, Paulo hangeweza kuamuru mwanamume huyo auawe. Lakini aliwaagiza Wakorintho wamtenge na ushirika. Mwenendo mpotovu wa mwanamume huyo ulikuwa ukiwaathiri wengine kutanikoni, ambao baadhi yao hata hawakuaibika kwa sababu ya mwenendo huo wenye kushtua!​—1 Kor. 5:1, 2, 13.

14. Paulo andangia bo rehema mwanalomi jojwabya antengiki nu ushilika Kukorintho, na ndaba jakike? (2 Wakorintho 2:5-8, 11)

14 Muda fulani baadaye, Paulo alikuja kujua kwamba mwanamume huyo alikuwa amefanya mabadiliko makubwa. Mtenda dhambi huyo alikuwa ametubu kikweli! Ingawa mwanamume huyo alikuwa ameliletea suto kutaniko, Paulo aliwaambia wazee kwamba hakutaka kuwa “mkali mno.” Aliwaagiza: ‘Wamsamehe kwa fadhili na kumfariji.’ Ona sababu ya Paulo: “Ili asilemewe na huzuni inayopita kiasi.” Paulo alimsikitikia mwanamume huyo aliyetubu. Paulo hakutaka mwanamume huyo alemewe sana au avunjike moyo kabisa, kwa sababu ya mambo aliyofanya hivi kwamba akate tamaa na asitafute msamaha.​—Soma 2 Wakorintho 2:5-8, 11.

15. Azee awesa kulangi bo uthabiti na rehema ku usawaziko?

15 Kama Yehova, wazee wanapenda pia kuonyesha rehema. Wanakuwa thabiti inapolazimu kufanya hivyo, lakini wanaonyesha rehema inapowezekana, ikiwa kuna msingi wa kufanya hivyo. Vinginevyo, hawatakuwa wakionyesha rehema, bali watakuwa wakiachilia kosa. Hata hivyo, je, ni wazee peke yao wanaohitaji kuonyesha rehema?

KI SEKIWESA KUTUJANGATI TWE TWABOA KULANGI REHEMA?

16. Kulengana na Methali 21:13, Yehova jwahenge bo basindwa kulangi rehema?

16 Wakristo wote wanajitahidi kuiga rehema ya Yehova. Kwa nini? Sababu moja ni kwamba Yehova hatawasikiliza wale wanaoshindwa kuwaonyesha wengine rehema. (Soma Methali 21:13.) Hakuna yeyote kati yetu ambaye angependa Yehova aache kusikiliza sala zake, hivyo kwa uangalifu tunaepuka kusitawisha moyo mgumu. Badala ya kukataa kumsikiliza Mkristo mwenzetu anayeteseka, sikuzote ni lazima tuwe tayari kusikia “kilio cha mtu wa hali ya chini.” Vivyo hivyo, tunajitahidi kutumia shauri hili lililoongozwa na roho ya Mungu: “Yule asiye na mazoea ya kuonyesha rehema atahukumiwa bila rehema.” (Yak. 2:13) Ikiwa tunakumbuka kwa unyenyekevu ni kwa kadiri gani tunahitaji rehema, tutawaonyesha wengine rehema hata zaidi. Hasa tungependa kumwonyesha rehema mtenda dhambi anaporudi kutanikoni.

17. Mfalme Daudi jwalangia bo rehema kuhuma mmwojo?

17 Mifano ya Biblia inaweza kutusaidia kuonyesha rehema na kuepuka kutenda kwa ukali. Kwa mfano, mfikirie Mfalme Daudi. Mara nyingi alionyesha rehema kutoka moyoni. Ingawa Sauli alitaka kumuua, Daudi alimwonyesha rehema mfalme mtiwa-mafuta wa Mungu, kamwe hakulipiza kisasi au kumdhuru.—1 Sam. 24:9-12, 18, 19.

18-19. Katika visa bo ibeli Daudi jwasindwa kulangi rehema?

18 Hata hivyo, Daudi hakuwa mwenye rehema sikuzote. Kwa mfano, Nabali, mwanamume aliyekuwa na tabia ya ukali, alipozungumza bila heshima na kukataa kumpatia Daudi na wanaume wake chakula, Daudi alikasirika sana na kuamua kumuua mwanamume huyo na wanaume wote katika nyumba yake. Lakini Daudi aliepuka hatia ya damu kwa sababu ya uamuzi wa haraka uliofanywa na Abigaili, mke mwenye ustahimilivu wa Nabali.—1 Sam. 25:9-22, 32-35.

19 Katika kisa kingine, nabii Nathani alimsimulia Daudi kuhusu mwanamume tajiri ambaye alimnyang’anya jirani yake maskini kondoo aliyekuwa anampenda. Akiwa amekasirika sana, Daudi alijibu hivi: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, mwanamume aliyefanya hivyo anastahili kufa!” (2 Sam. 12:1-6) Daudi alijua Sheria ya Musa. Mtu aliyeiba kondoo mmoja alipaswa kulipa kondoo wanne. (Kut. 22:1) Lakini je, alistahili hukumu ya kifo? Hiyo ilikuwa hukumu kali sana. Kihalisi, Nathani alikuwa akisimulia kisa cha mfano kuonyesha mfululizo wa dhambi nzito hata zaidi—ambazo Daudi mwenyewe alikuwa amefanya! Na Yehova alithibitika kuwa mwenye rehema nyingi zaidi kumwelekea Daudi, kuliko ambavyo Daudi angekuwa kumwelekea mwizi wa kondoo katika mfano wa Nathani!​—2 Sam. 12:7-13.

Mfalme Daudi hakuonyesha rehema aliposikia mfano wa Nathani (Tazama fungu la 19 na 20) *

20. Tuwesa kulibola ki kubokana nu mfanu guka Daudi?

20 Ona kwamba alipoongozwa na hasira yake, alimhukumu Nabali na wanaume wake wote kwamba walistahili kifo. Na baadaye, Daudi alikuwa tayari kumhukumu mwanamume aliyetajwa katika mfano wa Nathani kwamba alistahili kifo. Katika kisa cha pili, huenda tukajiuliza kwa nini mwanamume huyo ambaye kwa kawaida alikuwa mwenye fadhili, angeweza kutoa hukumu kali hivyo? Fikiria muktadha wa simulizi hilo. Wakati huo, Daudi alikuwa na dhamiri yenye hatia. Roho ya kuwahukumu wengine vikali, si ishara ya hali nzuri ya kiroho. Ni kinyume kabisa. Yesu aliwaonya hivi kwa uthabiti wafuasi wake: “Acheni kuhukumu ili msihukumiwe; kwa maana kwa hukumu mnayohukumu, mtahukumiwa.” (Mt. 7:1, 2) Hivyo, acheni tujitahidi kadiri tuwezavyo kuepuka kutenda kwa ukali na tuwe “tajiri katika rehema,” kama Mungu wetu.

21-22. Katika indela bo hususa tuwesa kulangi rehema?

21 Rehema haihusishi tu hisia. Isitoshe, rehema imefafanuliwa kuwa “huruma yenye matendo.” Hivyo, sisi sote tunaweza kuchunguza kwa uangalifu ni nani anayehitaji msaada wetu kwenye familia, kutanikoni, au jamii yetu. Bila shaka, kuna fursa nyingi za kuonyesha rehema! Je, kuna mtu anayehitaji faraja? Je, tunaweza kutoa msaada hususa, labda kuandaa mlo au kumfanyia tendo fulani la fadhili? Je, inawezekana kwamba Mkristo aliyerudishwa karibuni anahitaji faraja na ushirika wenye kujenga? Je, tunaweza kuwaambia wengine ujumbe wenye kufariji wa habari njema? Kuhubiri ni mojawapo ya njia bora zaidi ya kumwonyesha rehema kila mtu tunayekutana naye.​—Ayu. 29:12, 13; Rom. 10:14, 15; Yak. 1:27.

22 Ikiwa tutakuwa macho kutambua uhitaji wa wengine, tutaona kwamba kuna fursa nyingi za kuonyesha rehema. Tunapoonyesha rehema, hapana shaka tunamfurahisha Baba yetu wa mbinguni, Mungu aliye “tajiri katika rehema”!

NHAMBU 43 Sala ya Shukrani

^ ekichweka 5 Rehema ni mojawapo ya sifa zenye kuvutia zaidi za Yehova, na ni sifa ambayo kila mmoja wetu anahitaji kusitawisha. Katika makala hii, tutachunguza kwa nini Yehova huonyesha rehema, kwa nini tunaweza kusema kwamba nidhamu yake ni yenye rehema, na jinsi tunavyoweza kuonyesha sifa hiyo maridadi.

^ ekichweka 11 Ili kujua jinsi ambavyo waliorudishwa kutanikoni wanaweza kurudisha uhusiano wao pamoja na Mungu na jinsi wazee wa kutaniko wanavyoweza kuwasaidia, tazama makala “Kujenga Upya Urafiki Wako Pamoja na Yehova” katika toleo hili.

^ ekichweka 60 MAELEZO YA PICHA: Akiwa kwenye paa la nyumba yake, baba anamwona mwana wake mpotevu akirudi nyumbani, naye anakimbia haraka kwenda kumkumbatia.

^ ekichweka 64 MAELEZO YA PICHA: Kwa sababu ya kuhangaishwa na dhamiri yenye hatia, Mfalme Daudi alitoa hukumu iliyopita kiasi aliposikia mfano wa Nathani na kwa hasira alisema kwamba yule mwanamume tajiri alistahili kufa.