Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 17, 2019
JAPANI

Kimbunga Faxai Chapiga Japani

Kimbunga Faxai Chapiga Japani

Septemba 9, 2019, Kimbunga Faxai kilichokuwa na nguvu sana kilipiga eneo lililo karibu na Tokyo, Japani. Kimbunga hicho kilikuwa na pepo zilizovuma kwa mwendo wa kilomita 180 kwa saa na kusababisha umeme ukatike katika nyumba 580,000. Watu watatu hivi walikufa.

Ofisi ya tawi ya Japani inaripoti kwamba hakuna wahubiri waliokufa lakini ndugu na dada zetu saba walijeruhiwa. Tathmini za awali zinaonyesha kwamba dhoruba hiyo iliharibu nyumba 895 za akina ndugu, Majumba 28 ya Ufalme, na Jumba moja la Kusanyiko katika eneo la Chiba.

Ofisi ya tawi inaendelea kuchunguza kadiri ambavyo ndugu zetu waliathiriwa na Kimbunga Faxai. Tunasali kwamba Yehova, “Mungu anayetoa uvumilivu na faraja,” aendelee kuwategemeza ndugu na dada zetu walioathiriwa na msiba huo.—Waroma 15:5.