Hamia kwenye habari

Mawimbi makubwa yakipiga karibu na barabara kusini-magharibi mwa Japani

OKTOBA 10, 2019
JAPANI

Kimbunga Tapah Chapiga Kusini mwa Japani

Kimbunga Tapah Chapiga Kusini mwa Japani

Kuanzia Septemba 21 hadi 23, 2019, Kimbunga Tapah kilipiga kusini mwa Japani kwa pepo zenye nguvu na mvua. Kimbunga hicho kilifanya safari za ndege na za treni ziahirishwe na kuacha zaidi ya nyumba 30,000 bila umeme. Zaidi ya watu 50 walijeruhiwa katika visiwa vya Okinawa na Kyushu.

Ofisi ya tawi ya Japani inaripoti kwamba wahubiri watano wamejeruhiwa, kutia ndani dada mmoja ambaye amelazwa hospitalini. Zaidi ya nyumba 50 za ndugu zetu ziliharibiwa. Halmashauri ya Kutoa Msaada pamoja na ndugu wengine wanaosimamia mambo wanaendelea kutoa msaada wa kimwili na wa kiroho kwa wahubiri walioathiriwa. Ofisi ya tawi ya Japani itaendelea kuwa macho kuona madhara yanayotokezwa na kimbunga hicho na kutoa msaada unaohitajika.

Tunasali kwamba ndugu zetu nchini Japani waendelee kumtegemea Yehova ili awape faraja katika kipindi hiki kigumu.—Zaburi 94:19.