Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 13, 2018
JAPANI

Kimbunga Jebi Chapiga Japani

Kimbunga Jebi Chapiga Japani

Jumanne, Septemba 4, 2018, eneo la mashariki la Japani liliathiriwa na kimbunga kibaya zaidi kupiga nchi hiyo kwa miaka zaidi ya 20. Wenye mamlaka waliwaagiza watu wahame, na kama ilivyotarajiwa, kimbunga hicho kiliharibu vitu vingi.

Ofisi ya tawi ya Japani imethibitisha kwamba hakuna Shahidi wa Yehova aliyekufa. Hata hivyo, ndugu na dada 15 hivi walipata majeraha, na nyumba 538 hivi zimeharibiwa. Uchunguzi wa kwanza ulionyesha pia kwamba Majumba ya Ufalme 44 hivi yameharibiwa.

Halmashauri za Kutoa Msaada za Osaka na Sakai zinashirikiana kutoa msaada, ambao utatia ndani kukarabati nyumba zilizoharibiwa na kazi muhimu ya kufanya ziara za uchungaji.

Tunashukuru kwamba Yehova anaelewa hali ngumu ambazo waabudu wenzetu wanakabili na anawategemeza kupitia akina ndugu.—Zaburi 34:19.