Hamia kwenye habari

OKTOBA 5, 2023
ANGOLA

Vitabu vya Mathayo na Matendo Vyatolewa Katika Lugha ya Ishara ya Angola

Vitabu vya Mathayo na Matendo Vyatolewa Katika Lugha ya Ishara ya Angola

Septemba 23, 2023, Ndugu Johannes De Jager, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Angola, alitangaza kutolewa kwa vitabu vya Biblia vya Mathayo na Matendo ya Mitume katika Lugha ya Ishara ya Angola (LAS) wakati wa programu ya pekee. Watu 1,881 hivi walihudhuria programu hiyo kwenye Jumba la Kusanyiko huko Luanda, Angola. Vitabu hivyo vipya vya Biblia vingeweza kupakuliwa mara moja kwenye jw.org na JW Library Sign Language.

Inakadiriwa kwamba kuna viziwi 360,000 hivi nchini Angola. Kutaniko la kwanza la LAS lilianzishwa mwaka wa 2010. Leo, kuna zaidi ya wahubiri 1,000 wanaotumikia katika makutaniko 37 ya LAS, vikundi 7, na kikundi kimoja kidogo kotekote nchini Angola.

Hii ndiyo mara ya kwanza kwa vitabu vyovyote vya Biblia kutafsiriwa katika LAS. Ndugu mmoja alisema hivi baada ya kutazama kitabu cha Matendo: “Tafsiri yenye kusisimua ya Matendo 8:26-30, kuhusu Filipo akikimbia ili kumfikia ofisa Mwethiopia, imenisaidia kuelewa vizuri zaidi kwa nini ninapaswa kuendelea kutia jitihada nyingi katika huduma.”

Tuna uhakika kwamba vitabu hivyo viwili vya Biblia vilivyotolewa katika LAS vitawasaidia watu wengi zaidi kuhisi kwamba Yehova anawapenda na kwamba ‘anawaangazia nuru ya uso wake.’​—Hesabu 6:25.