Hamia kwenye habari

MEI 4, 2015
ANGOLA

Mashahidi watoa msaada baada ya mafuriko nchini Angola

Mashahidi watoa msaada baada ya mafuriko nchini Angola

Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la Lobito lilijaa kimo cha sentimita 70 za matope na maji.

LUANDA, Angola—Kuanzia Machi 11, 2015, mvua kubwa ilinyesha na kusababisha mafuriko yaliyoua watu 85 na kuharibu nyumba 119 katika jimbo la Benguela, kilomita 500 kutoka mji mkuu, Luanda. Ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Angola iliripoti kwamba hakuna Shahidi aliyekufa, lakini nyumba 11 za Mashahidi ziliharibiwa. Katika mji wa Lobito, Jumba la Ufalme moja—nyumba ya ibada—liliharibiwa na mafuriko.

Asubuhi iliyofuata baada ya mvua hiyo, Mashahidi walifanyiza halmashauri ya kutoa misaada ili kutathmini uharibifu uliotokea na kutoa msaada kwa waliohitaji. Walitoa msaada kwa waamini wenzao na kwa wengine ambao si Mashahidi. Katika Jumba la Ufalme la Lobito, wajitoleaji walitoa kimo cha sentimita 70 za matope na maji pamoja na kulirekebisha ajili ya mkutano wa pekee uliyokuwa umepangwa mwisho juma uliofuata mvua hiyo kubwa. Wawakilishi kutoka ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Angola walisafiri kutoka Luanda kwa ajili ya mkutano huo na mingine, ili kutoa faraja ya kiroho na kitia moyo kwa Mashahidi wa eneo hilo.

Mashahidi wenyeji walijitolea kusafisha na kurekebisha Jumba la Ufalme la Lobito.

Msemaji wa Mashahidi wa Yehova nchini Angola, Todd Peckham, alisema hivi: “Tunasikitika pamoja na walioathiriwa na mafuriko hayo. Ofisi ya tawi ya Angola itaendelea kusimamia kazi ya halmashauri ya kutoa misaada na kuwategemeza walio katika jamii.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Angola: Todd Peckham, simu +244 222 460 192