Hamia kwenye habari

Waziri msaidizi Claudio Romero (kushoto) akimpa cheti Ndugu Miguel Puchetti (kulia), ambaye ni mshiriki wa Halmashauri ya Ofisi ya Tawi ya Argentin

DESEMBA 31, 2019
ARGENTINA

Wenye Mamlaka Jijini Buenos Aires Wawatunuku Mashahidi wa Yehova Cheti kwa Sababu ya Kusanyiko la Kimataifa la 2019

Wenye Mamlaka Jijini Buenos Aires Wawatunuku Mashahidi wa Yehova Cheti kwa Sababu ya Kusanyiko la Kimataifa la 2019

Kusanyiko la kimataifa la 2019 limechaguliwa na wenye mamlaka jijini Buenos Aires kuwa tukio lililovutia watu zaidi jijini kwao katika nyanja za kijamii, kitamaduni na kidini. Desemba 12, 2019, katika mkutano pamoja na wana habari, wenye mamlaka jijini huko waliwatunuku ndugu zetu cheti kilichoonyesha umuhimu wa kusanyiko hilo.

Wawakilishi wawili wa serikali, Claudio Romero na Federico Pugliese, waliwapongeza Mashahidi wa Yehova kwa kazi wanayofanya jijini Buenos Aires. Claudio Romero alisema hivi: “Ningependa kukubali wazi umuhimu wa viwango vya kidini na utamaduni wenye amani na umoja mnaochangia katika jamii. Ninataka mjue dini yenu inanivutia sana kwa sababu mna roho ya kuwa tayari na kujitolea katika kazi yenu. Upendo na bidii mliyo nayo katika kazi ya kufundisha watu kuhusu imani yenu inastahili kuheshimiwa.” Federico Pugliese alisema hivi: “Leo, mmekusanyika mkiwa na ujumbe unaotia moyo , ‘Upendo Haushindwi Kamwe.’ Ninajua mnatenda kwa upendo, si katika siku za kusanyiko tu, lakini kila siku kwa sababu mnaongozwa na sifa hiyo.”

Tendo hilo la kutambuliwa rasmi ni uthibitisho mzuri wa upendo ambao ndugu na dada zetu huwaonyesha jirani zao ambao unastahili pongezi. Hata hivyo, kusudi letu la kuonyesha upendo kwa njia hii si ili kutambuliwa na serikali bali kumletea utukufu Mungu wetu mwenye upendo, Yehova.—1  Yohana 4:8.