Hamia kwenye habari

FEBRUARI 15, 2019
AUSTRALIA

Mafuriko Yasababisha Madhara Kwenye Eneo la Queensland, Australia

Mafuriko Yasababisha Madhara Kwenye Eneo la Queensland, Australia

Mvua kubwa imesababisha mafuriko yenye madhara kaskazini mashariki ya Australia. Maji ya mafuriko yamewalazimisha maelfu ya wakaaji wahame na yameharibu majengo na kufanya umeme ukatike.

Ofisi ya tawi ya Australasia inaripoti kwamba kwa sababu ya mafuriko, wahubiri 58 kutoka makutaniko matatu walilazimika kuhama nyumbani kwao na kwenda kwenye nyumba za watu wa familia au Mashahidi wengine. Nyumba kumi hivi za ndugu zetu ziliingiwa na maji ya mafuriko, mbili kati ya hizo zimeharibiwa kabisa.

Ofisi ya tawi imeanzisha Halmashauri ya Kutoa Misaada, na mwangalizi wa mzunguko pamoja na wazee wa kutaniko wa eneo hilo wanawafanyia wahubiri walioathiriwa ziara za uchungaji. Tunasali kwamba ndugu na dada zetu waendelee kuvumilia na kufarijiwa chini ya utunzaji wa wachungaji hao wenye upendo.—1 Petro 5:2.