Hamia kwenye habari

NOVEMBA 22, 2018
AZERBAIJAN

Mashahidi wa Yehova Waandikishwa Kuwa Shirika la Kidini Jijini Baku, Azerbaijan

Mashahidi wa Yehova Waandikishwa Kuwa Shirika la Kidini Jijini Baku, Azerbaijan

Novemba 8, 2018, Baraza la Taifa la Kuchunguza Mashirika ya Kidini nchini Azerbaijan liliwaandikisha kisheria Mashahidi wa Yehova katika jiji la Baku, mji mkuu wa Azerbaijan. Sasa ndugu zetu wanafurahia ulinzi wa kisheria wa kuabudu na kuhubiri kwa uhuru jijini humo.

Tunatumaini kwamba uamuzi huu wa kutuunga mkono utaandaa msingi wa kufuatwa katika maeneo mengine nchini ili waabudu wenzetu waandikishwe kisheria. Tunamshukuru Yehova kwamba maofisa wa serikali wenye moyo mzuri wameandikisha kisheria ibada yetu jijini Baku.—Wafilipi 1:7.