Hamia kwenye habari

APRILI 12, 2016
AZERBAIJAN

Polisi Nchini Azerbaijan Wakatisha Maadhimisho ya Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Polisi Nchini Azerbaijan Wakatisha Maadhimisho ya Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Machi 23, 2016, maofisa wa polisi jijini Gakh walikatisha kwa ghafula maadhimisho ya Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Hilo ndilo tukio la pekee zaidi la kidini la Mashahidi wa Yehova katika mwaka wote. Ukumbusho huo ulifanywa kwenye nyumba ya mtu binafsi. Maofisa hao wa polisi walionyesha kile walichodai kuwa amri kutoka mahakamani iliyowapa mamlaka ya kufanya upekuzi, na wakati wa upekuzi huo walipora nakala za kibinafsi za machapisho ya kidini ya watu waliohudhuria, kutia ndani Biblia. Isitoshe, maofisa hao waliwapeleka wahudhuriaji wote kwenye kituo cha polisi cha eneo hilo, wakawahoji na kuwaamuru waandike maelezo. Wahudhuriaji wote waliachiliwa baada ya polisi kuandikisha maelezo yaliyotiwa sahihi na wanaume sita ambao ni Mashahidi; maelezo hayo yanaweza kutumiwa kuwafungulia mashtaka kwa madai ya Kukiuka Sheria za Nchi.