Hamia kwenye habari

DESEMBA 31, 2018
BRAZILI

Moto Wateketeza Manaus, Brazili

Moto Wateketeza Manaus, Brazili

Mapema asubuhi ya Desemba 18, moto uliwaka katika jiji la Manaus, Brazili, na kuharibu nyumba 600 hivi. Ingawa hakuna mtu yeyote aliyekufa, watu 4 walijeruhiwa na watu zaidi ya 2,000 wamelazimika kuhama.

Ofisi ya tawi ya Brazili inaripoti kwamba hakuna ndugu au dada waliouawa au kujeruhiwa na moto huo. Hata hivyo, nyumba 10 za ndugu zetu ziliharibiwa, na kufanya wahubiri 18 na watu wao wa ukoo wapoteze makao. Chini ya uangalizi wa ofisi hiyo, Halmashauri ya Kutoa Misaada inatunza mahitaji ya wahubiri walioathiriwa.

Tuna uhakika kwamba ndugu na dada zetu walioathiriwa na moto huo wataendelea kumtegemea Yehova, ambaye kwetu ni “kimbilio salama katika nyakati za taabu.”—Zaburi 9:9, 10.