Hamia kwenye habari

JANUARI 29, 2021
ERITREA

Mamlaka za Eritrea Zamwachilia Huru Shahidi wa Yehova Kutoka Gerezani

Mamlaka za Eritrea Zamwachilia Huru Shahidi wa Yehova Kutoka Gerezani

Januari 29, 2021, ndugu yetu mmoja ameachiliwa huru baada ya kufungwa gerezani kwa zaidi ya miaka 12 kwa sababu ya imani yake. Hatua hii inakuja baada ya Mashahidi wengine 28 kuachiliwa Desemba 4, 2020. Tunashangilia kwamba ndugu yetu ameachiliwa huru. Tunaendelea kusali kwa ajili ya ndugu na dada 23 ambao bado wamefungwa gerezani nchini Eritrea.—Waebrania 13:3.