Hamia kwenye habari

Majumba mawili ya Ufalme yaliyoathiriwa na mafuriko huko Manila, Filipino

AGOSTI 5, 2024
FILIPINO

Mafuriko Yatokea Sehemu Nyingi Baada ya Kimbunga Gaemi Kuikumba Filipino

Mafuriko Yatokea Sehemu Nyingi Baada ya Kimbunga Gaemi Kuikumba Filipino

Mwishoni mwa Julai 2024, Kimbunga Gaemi a kilitokea katika maeneo mengi magharibi mwa Bahari ya Pasifiki. Ingawa kimbunga hicho chenye nguvu hakikuipiga Filipino, kilitokeza mvua kubwa kuliko kawaida na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa, mafuriko, na maporomoko ya ardhi katika mji mkuu wa Manila na maeneo ya karibu. Inakadiriwa kwamba watu milioni 4.8 waliathiriwa. Zaidi ya watu 600,000 wamelazimika kuhama kutoka nyumbani kwao, na watu 39 hivi wamekufa.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Hakuna ndugu au dada aliyekufa au kujeruhiwa

  • Wahubiri 155 walilazimika kuhama kutoka nyumbani kwao, lakini wengi tayari wamerudi

  • Nyumba 2 ziliharibiwa kabisa

  • Nyumba 11 zilipata uharibifu mkubwa

  • Nyumba 42 zilipata uharibifu mdogo

  • Majumba 11 ya Ufalme yalipata uharibifu mdogo

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Halmashauri 6 za Kutoa Msaada zimewekwa rasmi ili kuratibu kazi ya kutoa msaada

  • Waangalizi wa mzunguko na wazee wa maeneo hayo wanaandaa msaada wa kiroho na msaada wa kimwili kwa wale walioathiriwa na mafuriko

Kushoto: Ndugu na dada wakitayarisha misaada (juu) na maji ya kunywa (chini) kwa ajili ya walio na uhitaji

Kulia: Ndugu akifikisha misaada kwa dada aliyeathiriwa na mafuriko

Tutaendelea kusali kwa ajili ya wote walioathiriwa na kimbunga hicho, na tutaendelea kumshukuru Yehova kwa kuwa ‘tegemeo imara la nyakati zetu’ kadiri anavyowategemeza na kuwatunza ndugu na dada zetu.​—Isaya 33:6.

a Nchini Filipino kimbunga hicho kinajulikana kwa jina Kimbunga Carina.