Hamia kwenye habari

Moja kati nyumba 195 za ndugu zetu zilizoharibiwa vibaya

NOVEMBA 18, 2019
FILIPINO

Matetemeko Kadhaa ya Ardhi Yakumba Kusini Mwa Filipino

Matetemeko Kadhaa ya Ardhi Yakumba Kusini Mwa Filipino

Mfuatano wa matetemeko kadhaa ya ardhi yenye nguvu yamepiga kusini mwa Filipino kuanzia Oktoba 16, 2019. Watu 21 wamekufa, 400 wamejeruhiwa, na zaidi ya watu 35,000 wamelazimika kuhama makao yao. Angalau matetemeko matatu yameripotiwa kuwa na ukubwa wa 6.0. Matetemeko madogo yanaendelea kutokea katika eneo hilo. Hakuna ndugu au dada yeyote aliyekufa, ingawa dada mmoja alijeruhiwa kidogo.

Majumba manne ya Ufalme na nyumba 195 ya ndugu zetu ziliharibiwa vibaya; Majumba 9 ya Ufalme na nyumba 351 ziliharibika kidogo. Wengi kati ya ndugu zetu wanaishi katika mahema kwa sababu si salama kuishi ndani ya nyumba zao.

Ofisi ya tawi ya Filipino imeweka rasmi halmashauri mbili za kutoa msaada ili kuratibu jitihada za kutoa msaada. Wawakilishi sita wa ofisi ya tawi, kutia ndani washiriki watatu wa Halmashauri ya Tawi, wametembelea eneo hilo lililoathiriwa ili kuwatia moyo kiroho walioathiriwa.

Tunasali kwamba Yehova aendelee kuwasaidia ndugu zetu walioathiriwa na matetemeko hayo ya ardhi.—Zaburi 70:5.