Hamia kwenye habari

AGOSTI 5, 2022
FILIPINO

Tetemeko Kubwa Lakumba Filipino Kaskazini

Tetemeko Kubwa Lakumba Filipino Kaskazini

Julai 27, 2022, tetemeko lenye kipimo cha 7.0 lilitokea katika kisiwa cha Luzon, nchini Filipino. Mkoa wa Abra ndio ulioathiriwa zaidi. Mji wa Manila ulio kilomita 400 hivi kutoka Luzon pia ulipatwa na matetemeko madogo. Tetemeko hilo la ardhi lilifuatiwa na matetemeko mengine madogo-madogo zaidi ya 2,000.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Hakuna ndugu au dada aliyejeruhiwa

  • Wahubiri 4 walipata majeraha madogo

  • Familia 42 zililazimika kuhama makazi yao

  • Nyumba 63 zilipata uharibifu mdogo

  • Nyumba 1 ilipata uharibifu mkubwa

  • Majumba 13 ya Ufalme yamepata uharibifu

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Halmashauri 1 ya Kutoa Msaada iliteuliwa ili kusimamia kazi ya kutoa msaada

  • Wazee wa eneo hilo wanawafanyia ziara za uchungaji wale walioathiriwa

  • Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kupatana na miongozo ya kujilinda na COVID-19

Bila kukawia, ofisi ya tawi ilituma bidhaa mbalimbali za msaada kwa ndugu na dada kwenye maeneo yaliyoathiriwa na kuwaandalia makazi ya muda. Katika maeneo hayo, wahubiri walisaidiana wenyewe licha ya kwamba wote walikuwa wameathiriwa na tetemeko hilo.

Tuna imani kabisa kwamba Yehova atawaokoa ndugu na dada zetu katika ‘wakati huu wa taabu.’​—Zaburi 50:15.