Hamia kwenye habari

Ndugu Chávez na Ndugu López wakizungumza na maofisa kwenye kituo cha wazima-moto cha Coatepeque, Guatemala

DESEMBA 23, 2019
GUATEMALA

Maofisa wa Polisi na Wazima-Moto nchini Guatemala Wanufaika na Vikao Vinavyotegemea Biblia

Maofisa wa Polisi na Wazima-Moto nchini Guatemala Wanufaika na Vikao Vinavyotegemea Biblia

Mei 2019, wenye mamlaka nchini Guatemala waliwapa kibali ndugu zetu wawe na vikao na maofisa wa polisi na wazima-moto kuhusu kanuni za Biblia. Kwa sasa, maofisa wa polisi na wazima-moto 450 wameshiriki katika vikao hivyo kwenye majiji ya Coatepeque, Colomba Costa Cuca, Malacatán, na San Rafael Petzal.

Maofisa wakichukua machapisho kwenye kigari cha machapisho, baada ya kikao huko Colomba Costa Cuca, Guatemala

Juan Carlos Rodas, ambaye ni mzee aliyeshiriki katika vikao hivyo, alisema: “Kwa zaidi ya miaka 15, Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakijifunza na wafungwa katika magereza matatu tofauti nchini Guatemala. Maofisa wa magereza walitambua kwamba wafungwa waliojifunza Biblia nasi walibadilika na kuwa watu wenye tabia nzuri. Na hili likawachochea kupendekeza kwamba tufanye mazungumzo hayo ya Biblia pamoja na maofisa wa polisi na wazima-moto ili wapate mafunzo haya yanayotegemea Biblia.”

Tumekuwa tukifanya vikao hivyo vya dakika 15 hivi mara mbili kwa wiki, chini ya mwongozo wa Ofisi ya Tawi ya Amerika ya Kati. Vinahusu mambo kama vile kuboresha mahusiano na wengine, kutumia mamlaka kwa njia inayofaa, na kufanya kazi pamoja. Ndugu waliokuwa wakiongoza mazungumzo hayo waliwaachia machapisho na pia waliwaonyesha video zilizo kwenye tovuti yetu na kuwaonyesha jinsi ya kutafuta habari mbalimbali kwenye programu ya JW Library.

Mashahidi wa Yehova wanafurahi sana kupata fursa ya kufanya vikao hivi pamoja na maofisa wa polisi na wazima-moto. Tunatumaini kwamba wataendelea kunufaika kutokana na hekima inayopatikana kwenye Biblia.—2 Timotheo 3:16.