Hamia kwenye habari

OKTOBA 15, 2018
HAITI

Tetemeko la Ardhi Laikumba Haiti Kaskazini

Tetemeko la Ardhi Laikumba Haiti Kaskazini

Jumamosi, Oktoba 6, 2018, tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 5.9 lilitokea katika eneo la kaskazini mwa Haiti, na kusababisha vifo vya watu 17 na kuwajeruhi zaidi ya 300.

Hakuna ndugu ambaye ameripotiwa kuwa amekufa; hata hivyo, wahubiri wawili walijeruhiwa kidogo. Ripoti za awali kutoka kwa waangalizi wa mzunguko zinaonyesha kwamba nyumba 44 na Majumba 4 ya Ufalme yaliharibiwa. Katika jiji la Port-de-Paix, ndugu 50 na washiriki wa familia zao walilazimika kuhama kutoka nyumba zao kwa kuwa hazikuwa salama. Familia hizo zinatunzwa na makutaniko ya eneo hilo. Mshiriki wa Halmashauri ya Tawi la Haiti alitembelea eneo hilo lililoathiriwa akiwa na ndugu wawili wa Idara ya Usanifu Majengo na Ujenzi ili kukagua madhara na kuwatia moyo akina ndugu. Halmashauri ya Kutoa Msaada Wakati wa Misiba imeanzishwa ili kufanya mipango ya jinsi ya kutoa msaada.

Tunaendelea kuwafikiria na kusali kwa ajili ya ndugu zetu nchini Haiti. Tunashukuru kwamba Baba yetu wa mbinguni ameahidi kuwafariji watumishi wake waaminifu kupitia upendo wake mshikamanifu.—Zaburi 119:76.