Hamia kwenye habari

FEBRUARI 3, 2021
INDONESIA

Mafuriko Makubwa Nchini Indonesia

Mafuriko Makubwa Nchini Indonesia

Eneo

Kalimantan Kusini, Sulawesi Kaskazini, na Moluccas Kaskazini

Janga

  • Katikati mwa Januari 2021, mafuriko makubwa na maporomoko ya ardhi yalitokeza uharibifu mkubwa na kuwalazimisha watu kuhama

Athari ambazo ndugu na dada zetu wamepata

  • Wahubiri 90 hivi walihitaji kuhama kwa muda

Uharibifu wa mali

  • Nyumba 3 ziliharibiwa kidogo

Jitihada za kutoa msaada

  • Wazee wa kutaniko walitenda upesi kuwasaidia wahubiri kuhama. Pia wazee walipanga wahubiri wapate mahali pa kuishi kwa muda, chakula, na mahitaji mengine

  • Wahubiri katika makutano ya eneo hilo wanasaidia kufanya usafi na kurekebisha nyumba zilizoharibiwa

  • Waangalizi wa mzunguko wanaandaa utegemezo wa kiroho na faraja kwa wahubiri walioathiriwa

  • Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kupatana na miongozo ya kujilinda dhidi ya ugonjwa wa COVID-19

Tunashukuru kwamba Yehova anawaandalia msaada ndugu na dada zetu wapendwa katika “nyakati za taabu.”—Methali 17:17.