Hamia kwenye habari

JUNI 3, 2021
JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo” Yatolewa Katika Kialur Nchini Kongo

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo” Yatolewa Katika Kialur Nchini Kongo

Mei 30, 2021, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yatolewa katika Kialur. Ndugu Hugues Kabitshwa, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kongo (Kinshasa), alitoa Biblia katika mfumo wa kielektroni katika programu iliyokuwa imerekodiwa mapema.

Mambo Makuu

  • Kialur ni lugha inayozungumzwa Afrika ya Kati, hasa katika eneo la kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na pia nchi jirani ya Uganda

  • Inakadiriwa kwamba watu 1,735,000 wanazungumza Kialur

  • Zaidi ya wahubiri 1,500 wanatumikia katika makutaniko na vikundi 48 vinavyozungumza lugha ya Alur

  • Watafsiri 6 walitumia muda wa miezi 12 kuikamilisha

Ndugu Christian Belotti, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kongo (Kinshasa) alisema hivi: “Wahubiri wanaozungumza Kialur watapenda kusoma Biblia hii. Itawasaidia kufafanua maandiko na kusaidia wengine wakuze uthamini mwingi kuelekea Neno la Mungu.”—Luka 24:32.

Tuna uhakika kwamba Biblia itawasaidia ndugu na dada zetu kuendelea kutangaza “habari njema ya milele.”—Ufunuo 14:6.