Hamia kwenye habari

AGOSTI 5, 2019
KAMERUN

Mashahidi wa Yehova Watoa Biblia ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Katika Lugha ya Kibasa Nchini Kamerun

Mashahidi wa Yehova Watoa Biblia ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Katika Lugha ya Kibasa Nchini Kamerun

Mashahidi wa Yehova walitoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kibasa kwenye kusanyiko la eneo huko Douala, Kamerun, mnamo Agosti 2, 2019. Kazi ya kutafsiri toleo hilo la Maandishi ya Kigiriki ilichukua miezi 18. Hii ndio mara ya kwanza kwa Mashahidi wa Yehova kutafsiri Biblia katika mojawapo ya lugha za kienyeji za nchini Kamerun.

Ndugu Peter Canning, mshiriki wa Halmashauri ya Ofisi ya Tawi ya Kamerun, alitangaza kutolewa kwa Biblia hiyo siku ya kwanza ya kusanyiko la eneo katika Jumba la Kusanyiko huko Logbessou ambako watu 2,015 walihudhuria.

Kabla ya kutolewa kwa toleo hilo la Maandiko ya Kigiriki, ndugu na dada zetu wanaozungumza Kibasa walitumia tafsri iliyo ngumu kuelewa na iliyokuwa ghali sana. Mmoja kati ya watafsiri katika kikundi kilichotafsiri Biblia ya Kibassa anasema hivi: “Tafsiri hii mpya itawasaidia wahubiri kuielewa Biblia kwa urahisi. Itawasiaidia kumpenda Yehova na tengenezo lake zaidi.”

Inakadiriwa kwamba watu 300,000 wanazungumza Kibassa nchini Kamerun. Kuna wahubiri 1,909 wanaozungumza Kibasa kwenye eneo la ofisi ya tawi ya Kamerun.

Tuna hakika kwamba tafsiri hii iliyo sahihi na rahisi kueleweka itawasaidia wasomaji kuona kwamba “neno la Mungu liko hai.”—Waebrania 4:12.