Hamia kwenye habari

Wenzi wa ndoa mapainia, Ndugu na Dada Mudaheranwa, wakielekea kazini

APRILI 6, 2020
KANADA

Amani Katika Kipindi Chenye Mshtuko

Amani Katika Kipindi Chenye Mshtuko

Ndugu Jean-Yves na mke wake, Vasthie Mudaheranwa, wanawasaidia watu wanaoumwa ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya corona huko Montreal, Kanada. Ndugu Mudaheranwa ni daktari wa mfumo wa hewa, na Dada Mudaheranwa anatumikia kama muuguzi katika kituo maalum cha wagonjwa wenye maambukizi ya virusi vya corona. Katika kipindi hiki chenye mkazo mkubwa wa kihisia, wanapata nguvu kutoka kwa Yehova na kunufaika kwa kuwa na “hali nzuri ya moyo,” aliyoahidi—Isaya 65:14.

Ndugu Mudaheranwa anasema: “Wengi kati ya wafanyakazi wenzangu wana hofu sana, sijawahi kuwaona katika hali kama hiyo.” Dada Mudaheranwa anasema hivi: “Funzo la kibinafsi linasaidia sana. Tunafikiria kuhusu ishara za siku za mwisho, kisha tunajikumbusha kwamba Yehova yuko pamoja nasi, na hatatuacha kamwe. Pia, sala ni muhimu sana. Kabla ya kwenda kazini kila siku, ninasali kisha ninapata amani.”

Ndugu na Dada Mudaheranwa, wakishiriki katika mikutano ya kutaniko

Ndugu Mudaheranwa, anaeleza hivi: “Ninatoka Rwanda, na nilishuhudia mauaji ya kimbari. Jambo kama hilo halijawahi kutokea nchini Kanada, hivyo wakati mwingine, tunaweza kusahau kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Ni lazima nikiri kwamba, sikuwa nafikiri sikuzote kwamba siku ya Yehova iko karibu sana. Ugonjwa huu ulioenea duniani pote, umeimarisha imani yangu kwamba tunaishi katika siku za mwisho, na hilo pia limeimarisha imani yangu katika Biblia na unabii unaopatikana katika Biblia.”

Imani kama ya Ndugu na Dada Mudaheranwa, inaonyeshwa duniani pote kadiri watu wa Yehova wanavyoendelea kuwa na amani wakati wa janga hili.—Isaya 48:18.