Hamia kwenye habari

DESEMBA 24, 2021
KANADA

Kielelezo cha Imani Katika Kambi za Kazi Ngumu Kanada

Kielelezo cha Imani Katika Kambi za Kazi Ngumu Kanada

Katika majira ya kiangazi ya 1946, wenye mamlaka nchini Kanada waliwaachilia huru Mashahidi wa Yehova waliokuwa katika kambi mbalimbali. Kambi hizo zilikuwa katika maeneo ya mbali ya msituni ya Kanada. Zaidi ya ndugu zetu 300 waliokuwa vijana wakati huo walilazimishwa kufanya kazi ngumu katika kambi hizo kwa kuwa walikataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri zao. Ndugu zetu walivumilia hali hizo ngumu na hata waliondoka kambini wakiwa imara zaidi kiroho. Miaka 75 imepita tangu ndugu zetu wapendwa walipoachiliwa na kutoka kwenye kambi hizo. Don MacLean, ni kati ya ndugu wachache waliokuwa katika kambi hizo, ambao wako hai hadi sasa. Anasema hivi: “Ninaweza kusema, mambo mengi yaliyonipata wakati wa vita yaliniimarisha sana. Kila mara ninapoyakumbuka ninamshukuru Yehova.”