Hamia kwenye habari

JULAI 25, 2017
KANADA

Moto wa Msituni Waathiri British Columbia, Mashahidi Wakwama Kwenye Eneo la Kusanyiko

Moto wa Msituni Waathiri British Columbia, Mashahidi Wakwama Kwenye Eneo la Kusanyiko

Familia za Mashahidi wa Yehova zaidi ya 130 zilishindwa kurudi nyumbani kwao baada ya kuhudhuria kusanyiko lao la kila mwaka lililofanyika Julai 7-9, 2017, kwa sababu ya moto wa msituni uliokuwa ukisambaa katika eneo la kusini la Prince George, British Columbia, ambako wenye mamlaka walitoa agizo la kuwahamisha.

Ofisi ya tawi ya Kanada ya Mashahidi wa Yehova iliyoko kwenye mkoa wa Ontario, ilianzisha halmashauri ya kutoa msaada ili kuandaa nyumba na chakula kwa ajili ya Mashahidi walioathiriwa. Wasimamizi wa Kituo cha CN, mahali ambapo Mashahidi 2,500 hivi walikusanyika kwa ajili ya kusanyiko, waliwaruhusu kuegesha tela za magari yao kwenye uwanja huo ili ziwe makao ya muda.

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova linasimamia kazi ya kutoa msaada kutoka makao makuu ya ulimwenguni pote likitumia michango inayotolewa kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ya Mashahidi ya ulimwenguni pote.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1-845-524-3000

Kanada: Matthieu Rozon, +1-905-873-4100