Hamia kwenye habari

Kuanzia kushoto hadi kulia: Ndugu Choi Young-won, Baek Jong-hyun, na Kang Ra-yoon wakiaga familia zao kabla ya kwenda kuanza utumishi wa badala wa kiraia

NOVEMBA 23, 2020
KOREA KUSINI

Tukio la Kihistoria: Korea Kusini Yaanzisha Utumishi wa Badala wa Kiraia

Tukio la Kihistoria: Korea Kusini Yaanzisha Utumishi wa Badala wa Kiraia

Kwa mara ya kwanza katika historia, serikali ya Korea Kusini imeanzisha utumishi wa badala wa kiraia kwa watu wanaokataa kujiunga na utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri. Oktoba 26, 2020, ndugu zetu 63 walikubali aina hii ya utumishi na kuanza kazi ya miaka mitatu katika gereza walilopangiwa. Kazi wanazofanya zinatia ndani kutoa huduma za chakula, ununuzi, elimu, usafi na afya, na udumishaji. Kulingana na sheria zilizopo sasa, baada ya kutumikia kifungo kwa miezi miwili, nusu ya ndugu waliofungwa kufikia kipindi hicho wataruhusiwa kutoka gerezani baada ya saa za kazi ili kushiriki katika shughuli za kitheokrasi. Hata hivyo, wanapaswa kuwa wamerudi gerezani kufikia saa tatu usiku.

Ndugu Kim Hyun-soo, mmoja kati ya ndugu hao 63, anasema hivi: “Ijapokuwa utaratibu huo haujafikia viwango vya kimataifa, ninakubali utumishi huo kwa sababu ni wa kiraia na hauko chini ya usimamizi wa jeshi.”

Tuna uhakika kwamba ndugu zetu vijana waaminifu nchini Korea Kusini, wataendelea kumletea Yehova utukufu na sifa kupitia ‘matendo yao mema.’—Mathayo 5:16.

 

Ndugu Park Jae-hyuk akiaga familia yake anapoenda kuanza utumishi wa badala wa kiraia

Ndugu Lee Sang-joon akijitayarisha kuacha familia yake (kushoto). Wazazi wa ndugu Kim Yeong-hoon wakimkumbatia (kulia)

Ndugu Jeong Yeo-gyeom akienda kuanza utumishi wa badala wa kiraia