Hamia kwenye habari

MEI 18, 2015
KOREA KUSINI

Hakimu wa Korea Kusini Afuta Mashtaka ya Wanaokataa Utumishi wa Kijeshi kwa Sababu ya Dhamiri

Hakimu wa Korea Kusini Afuta Mashtaka ya Wanaokataa Utumishi wa Kijeshi kwa Sababu ya Dhamiri

Mei 12, 2015, Mahakama ya Wilaya ya Gwangju iliamua kwamba Mashahidi watatu wa Yehova hawakuwa na hatia ya kukataa amri ya kujiandikisha jeshini. Hakimu Mkuu Choi, Chang-seok alisema hivi: “Ni muhimu kupatanisha uhuru wa dhamiri unaoruhusiwa na Katiba na wajibu wa kulinda taifa kwa njia inayofaa.” Aliongezea hivi: “Haki za msingi zinapopingana na mambo mengine katika katiba kama vile wajibu wa raia, ni muhimu kushughulikia tofauti hizo kwa njia ambayo mambo yote mawili yanaweza kutimizwa kwa nzuri iwezekanayo.” Mashahidi wanatazamia kuwa mwendesha mashtaka atakata rufani kupinga uamuzi huo ndani ya siku saba.