NOVEMBA 30, 2018
KOREA KUSINI
Ndugu Nchini Korea Waachiliwa Kutoka Gerezani
Ofisi ya tawi ya Korea inaripoti kwamba Novemba 30, 2018, ndugu 57 waliachiliwa kutoka gerezani na kuungana tena na familia zao. Ndugu ulimwenguni pote wanafurahia sana tukio hilo walilosubiri kwa hamu na wanamsifu Yehova kwa kuwapa kibali na baraka zake.—Hesabu 6:24-26.
Tunasali kwa ajili ya ndugu nane waliosalia gerezani ambao wanatarajia kuachiliwa baada ya kutumikia miezi 6 ya kifungo chao cha miezi 18.