Hamia kwenye habari

JUNI 7, 2018
KUBA

Washiriki wa Familia ya Mashahidi Wamekufa Baada ya Ndege kuanguka Nchini Kuba

Washiriki wa Familia ya Mashahidi Wamekufa Baada ya Ndege kuanguka Nchini Kuba

Ijumaa, Mei 18, 2018, ndege aina ya Boeing 737 ilianguka muda mfupi baada ya kuondoka Havana, Kuba. Kati ya watu 113 waliokuwemo, mmoja tu ndiye aliyeokoka, na hivyo kuifanya kuwa aksidenti mbaya zaidi kutokea kwa miaka mingi.

Inasikitisha kwamba kati ya waliokufa kulikuwa na familia ya Mashahidi wa Yehova (baba, mama, na mwana mwenye umri wa miaka 22). Familia hiyo ilizikwa Jumamosi, Mei 26, 2018.

Wazee wanawategemeza kihisia na kiroho marafiki na familia ya waliokufa, na pia wenye mamlaka wameandaa msaada unaofaa. Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea “kuwafariji wote wanaoomboleza” katika kipindi hiki kigumu.—Isaya 61:1, 2.