Hamia kwenye habari

JANUARI 1, 2019
KYRGYZSTAN

Hatua Nzuri ya Kisheria Jijini Osh, Kyrgyzstan

Hatua Nzuri ya Kisheria Jijini Osh, Kyrgyzstan

Novemba 30, 2018, Wizara ya Haki ya Kyrgyzstan iliandikisha kisheria ofisi ya Mashahidi wa Yehova katika jiji la Osh, jiji la pili kwa ukubwa nchini Kyrgyzstan.

Ingawa ndugu zetu waliandikishwa kisheria nchini Kyrgyzstan tangu mwaka wa 1998, baada ya sheria mpya kuhusu dini kutekelezwa mwaka wa 2008, wenye mamlaka wamekataa kuwaandikisha kisheria katika majiji yaliyo kusini mwa nchi hiyo. Jiji la Osh liko upande huo wa kusini. Kwa sababu hiyo, mara nyingi wenye mamlaka wameona mikutano yetu ya Kikristo na huduma ya shambani kuwa kinyume cha sheria. Mara kwa mara, polisi wamevamia nyumba za akina ndugu au maeneo yaliyokodiwa ambako ndugu zetu walikusanyika kwa ajili ya ibada.

Tunafurahia hatua hiyo ya kuandikishwa kisheria na itasaidia kuthibitisha haki ya Mashahidi nchini Kyrgyzstan ya kukutana kwa uhuru na kushiriki kwa amani ujumbe wa Biblia na wengine.—1 Timotheo 2:1-4.