FEBRUARI 17, 2022
MADAGASKA
Kimbunga Batsirai Chapiga Madagaska
Februari 6, 2022, Kimbunga Batsirai kilipiga pwani ya kusini-mashariki ya Madagaska na kiliambatana na upepo mkali uliovuma kwa kilometa 235 kwa saa. Maelfu ya watu walipoteza makao yao kwa sababu ya kimbunga hicho. Kilisababisha mafuriko makubwa na uharibifu mwingi.
Athari kwa Ndugu na Dada Zetu
Hakuna ndugu au dada aliyeuawa
Wahubiri 407 wamelazimika kuhama makao yao
Nyumba 35 zilipata uharibifu mdogo
Nyumba 19 zilipata uharibifu mkubwa
Nyumba 35 ziliharibiwa kabisa
Majumba 4 ya Ufalme yalipata uharibifu mdogo
Jitihada za Kutoa Msaada
Halmashauri ya Tawi imeanzisha Halmashauri 20 za Kutoa Msaada ili kupanga kazi ya kutoa msaada
Waangalizi wa mzunguko na wazee wa eneo hilo wanawasaidia ndugu zetu kiroho. Akina ndugu wamefanya mipango ya kuandaa makao ya muda, chakula, na mahitaji mengine
Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kulingana na miongozo ya usalama ya kujilinda dhidi ya COVID-19
Tuna uhakika kwamba Yehova atakuwa ‘kimbilio salama’ kwa ajili ya ndugu zetu katika kipindi hiki kigumu.—Zaburi 18:2.