Hamia kwenye habari

Kimbunga Batsirai chenye upepo mkali kilipiga pwani ya kusini-mashariki ya Madagaska. Kimbunga hicho kilisababisha mafuriko makubwa na uharibifu mwingi

FEBRUARI 17, 2022
MADAGASKA

Kimbunga Batsirai Chapiga Madagaska

Kimbunga Batsirai Chapiga Madagaska

Februari 6, 2022, Kimbunga Batsirai kilipiga pwani ya kusini-mashariki ya Madagaska na kiliambatana na upepo mkali uliovuma kwa kilometa 235 kwa saa. Maelfu ya watu walipoteza makao yao kwa sababu ya kimbunga hicho. Kilisababisha mafuriko makubwa na uharibifu mwingi.

Athari kwa Ndugu na Dada Zetu

  • Hakuna ndugu au dada aliyeuawa

  • Wahubiri 407 wamelazimika kuhama makao yao

  • Nyumba 35 zilipata uharibifu mdogo

  • Nyumba 19 zilipata uharibifu mkubwa

  • Nyumba 35 ziliharibiwa kabisa

  • Majumba 4 ya Ufalme yalipata uharibifu mdogo

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Halmashauri ya Tawi imeanzisha Halmashauri 20 za Kutoa Msaada ili kupanga kazi ya kutoa msaada

  • Waangalizi wa mzunguko na wazee wa eneo hilo wanawasaidia ndugu zetu kiroho. Akina ndugu wamefanya mipango ya kuandaa makao ya muda, chakula, na mahitaji mengine

  • Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kulingana na miongozo ya usalama ya kujilinda dhidi ya COVID-19

Tuna uhakika kwamba Yehova atakuwa ‘kimbilio salama’ kwa ajili ya ndugu zetu katika kipindi hiki kigumu.​—Zaburi 18:2.