Hamia kwenye habari

MAENEO YA PALESTINA

Maelezo Mafupi Kuhusu Eneo la Palestina

Maelezo Mafupi Kuhusu Eneo la Palestina

Mashahidi wa Yehova wamekuwapo katika Eneo la Palestina tangu mwaka 1919. Walianzisha kutaniko jijini Ramallah mwaka 1920 na kuanzisha kutaniko la pili, karibu na Bethlehemu, mwaka 1942. Kutokana na vita vya Palestina vilivyotokea mwaka wa 1948, eneo liligawanywa katika sehemu mbili: Upande mmoja ukawa eneo la taifa jipya la Israeli, na upande mwingine ukawa chini ya Yordani. Kwa zaidi ya miaka 20 hivi, Mashahidi nchini Israeli na katika eneo la Palestina walikuwa hawawezi kuwasiliana. Baada ya Vita vya Siku Sita katika mwaka wa 1967, mawasiliano yalianza tena, na Mashahidi wakaanza tena kufurahia uhuru wa kukusanyika na kufanya utendaji wao katika Eneo la Ukingo wa Magharibi.

Ingawa Mashahidi wa Yehova katika Eneo la Palestina wameomba kusajiliwa kisheria, wenye mamlaka wameyakataa maombi yao. Mashahidi wanaweza kukusanyika pamoja kwa ajili ya ibada na kuwaambia wengine imani yao, lakini kukosa usajili wa kisheria kumewafanya wanyimwe haki za kibinafsi. Jitihada zinaendelea kufanywa ili kupata haki za msingi na kuweza kuandikishwa kisheria.