Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 8, 2021
MAREKANI

Kimbunga Ida Chaikumba Marekani Kuanzia Kusini Hadi Kaskazini

Kimbunga Ida Chaikumba Marekani Kuanzia Kusini Hadi Kaskazini

Agosti 29, 2021, Kimbunga Ida kilipiga nchi kavu karibu na eneo la Port Fourchon, Louisiana. Dhoruba kali, mvua kubwa, na upepo mkali ulisababisha mafuriko, uharibifu wa mali, na ukosefu wa umeme katika eneo lote la Marekani linaloitwa Gulf Coast. Septemba 1 masalio ya Kimbunga Ida yalisababisha marufiko ya ghafla na vimbunga katika eneo la kaskazini-mashariki mwa Marekani. Katika maeneo fulani, inakadiriwa kwamba umeme utarudishwa baada ya majuma kadhaa.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Kufikia sasa hatujapata ripoti kwamba yeyote amekufa

  • Ndugu 2 walipata majeraha madogo

  • Dada 1 alilazwa hospitalini kwa sababu ya jeraha ambalo alipata alipokuwa akiondoka nyumbani kwake

  • Nyumba 1,429 zimeharibiwa kidogo

  • Nyumba 183 zimepata uharibifu mkubwa

  • Nyumba 19 zimeharibiwa kabisa

  • Majumba 43 ya Ufalme yameharibwa kidogo

  • Majumba 10 ya Ufalme yamepata uharibifu mkubwa

  • Majumba 4 ya Kusanyiko yamepata uharibifu mkubwa

Nyumba ya dada mmoja huko New Orleans, Louisiana, iliyoharibiwa na kimbunga hicho

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Waangalizi wa mzunguko na wazee wa maeneo hayo pamoja Halmashauri za Kutoa Msaada wanafanya ziara za uchungaji kwa ndugu na dada walioathiriwa

  • Msaada wa kibinadamu unatolewa kwa wale walio na mahitaji ya dharura

  • Jitihada za kutoa msaada zinatolewa kupatana na miongozo ya usalama ya COVID-19

Kwa kuwa ndugu zetu walikuwa wamejitayarisha kwa ajili ya misiba na pia kushirikiana kwao na miongozo ya serikali ya kuhama maeneo yaliyokuwa hatari kumesaidia kuokoa uhai.—Methali 22:3.