Hamia kwenye habari

Ufa uliotokezwa na tetemeko la ardhi

JULAI 15, 2019
MAREKANI

Matetemeko ya Ardhi Yapiga Kusini mwa California

Matetemeko ya Ardhi Yapiga Kusini mwa California

Tangu Julai 4, 2019, matetemeko makubwa yaliyoambatana na matetemeko mengine madogo-madogo yalikumba eneo la jangwa la Mojave lililo kusini mwa California. Matetemeko hayo yanatia ndani tetemeko la kipimo cha 7.1 ambalo linasemekana kuwa lenye nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa katika eneo hilo katika miaka 200 iliyopita.

Matetemeko hayo yalitokea karibu na jiji la Ridgecrest, ambako kuna wahubiri 215. Tunashukuru kwamba hakuna ndugu yetu aliyejeruhiwa vibaya. Hata hivyo, wahubiri watatu walipatwa na majeraha madogo, na ripoti zilizotufikia zinasema kwamba wahubiri saba hawana makao. Pia, nyumba 7 za ndugu zetu ziliharibiwa kabisa, na nyingine 35 zinahitaji kufanyiwa marekebisho madogo. Zaidi ya hilo, Majumba mawili ya Ufalme yaliharibiwa kidogo.

Waangalizi wawili wa mzunguko wanasimamia kazi ya kutoa misaada katika eneo hilo. Waangalizi hao wanashirikiana na wazee wa makutaniko ya eneo hilo kuwafariji ndugu na dada walioathiriwa na tetemeko hilo.

Tunasali kwamba Yehova aendelee kuwapa waabudu wenzetu hekima wanayohitaji ili kukabiliana na majanga ya asili kama haya. —Methali 2:6-8.