Hamia kwenye habari

Ndugu Joseph F. Rutherford akizungumza katika kusanyiko la kihistoria lililofanyika Cedar Point, Ohio, U.S.A., Septemba 10, 1922. Picha ya kulia: Kamera ya kuchukua video ya sehemu za programu hiyo

APRILI 11, 2022
MAREKANI

Kutoka Kwenye Jumba la Makumbusho

Tunatafuta Sinema Iliyorekodiwa ya Kusanyiko la Cedar Point

Tunatafuta Sinema Iliyorekodiwa ya Kusanyiko la Cedar Point

Tangazo kwenye gazeti kuhusu sinema ya kusanyiko lililofanyika Cedar Point

Kusanyiko la 1922 lililofanyika Cedar Point, Ohio, U.S.A., linajulikana sana miongoni mwa Mashahidi wa Yehova kwa sababu ni katika kusanyiko hilo, Ndugu Joseph F. Rutherford aliwachochea wote watangaze Ufalme.

Pia, kuna sababu nyingine ya pekee: Kusanyiko hilo lilirekodiwa. Kufikia sasa, kumbukumbu zilizobaki za video hiyo hazijapatikana.

Picha moja ya kusanyiko hilo la kimataifa la Septemba 1922 linaonyesha kwamba kulikuwa na jukwaa dogo na kamera ya kuchukua video ya sehemu za programu hiyo muhimu. Enzi hizo, teknolojia ya kamera za kuchukua video ilikuwa haijazoeleka.

Inaelekea watu wengi walipata fursa ya kutazama sinema iliyorekodiwa ya kusanyiko hilo. Kwa mfano, Gazeti moja lilikuwa na tangazo kuhusu sinema hiyo. Tangazo hilo liliwatia moyo wasomaji “kutazama kusanyiko hilo nyumbani. Mwaone Rafiki zenu, mtazame hotuba ya Ubatizo.” Na pia gazeti hilo lilitoa dokezo la kushiriki huduma: “Wakaribishe jirani zako na uwatolee ushahidi kwa kutazama Sinema ya Kusanyiko pamoja nao. Agiza sasa.”

Ikiwa umewahi kuona kumbukumbu ya video ya sinema hii, tafadhali wasiliana na Idara ya Makumbusho kupitia MuseumDonations@jw.org au unaweza kuandikia Makao Makuu ya Mashahidi wa Yehova kupitia anuani hii 1 Kings Drive, Tuxedo Park, NY 10987. Tunatumaini tutafanikiwa kupata video ya sinema hiyo ya pekee ambayo ni sehemu muhimu ya historia ya Mashahidi wa Yehova.