DESEMBA 14, 2021
MAREKANI
Vimbunga Vyasababisha Uharibifu Mkubwa Katika Maeneo ya Kusini na Sehemu za Kati za Marekani
Kuanzia Desemba 10, 2021, vimbunga kadhaa vilipita kusini na katikati ya Marekani. Vilisababisha uharibifu mkubwa katika eneo lenye urefu wa kilometa 402. Watu kadhaa walikufa, wengine wengi wakapoteza makao yao, na majengo mengi yaliharibiwa. Jimbo la Kentucky ndilo lililoathiriwa zaidi.
Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata
Hakuna ndugu aliyejeruhiwa au kuuawa
Wahubiri 31 wamelazimika kuhama makao yao
Nyumba 10 ziliharibiwa kidogo
Nyumba 3 zilipata uharibifu mkubwa
Nyumba 9 ziliharibiwa kabisa
Jitihada za Kutoa Msaada
Waangalizi wa mzunguko na wazee wa makutaniko wanazifariji familia zilizoathiriwa
Jitihada zote za kutoa msaada zinatolewa kupatana na miongozo ya kujilinda dhidi ya COVID-19
Tuna uhakika Yehova anawahurumia sana ndugu na dada ambao wanateseka kutokana na misiba hiyo ya asili.—Isaya 63:9.