Hamia kwenye habari

DESEMBA 6, 2018
MAREKANI

Tetemeko Kubwa Nchini Alaska

Tetemeko Kubwa Nchini Alaska

Novemba 30, 2018, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 lilipiga eneo karibu na Anchorage, Alaska. Ingawa hakuna ripoti ya mtu yeyote aliyekufa kutokana na tetemeko hilo, kulingana na vyombo vya habari, barabara zimeharibiwa sana.

Ofisi ya tawi ya Marekani inaripoti kwamba wahubiri saba walipata majeraha madogo kwa sababu ya tetemeko hilo. Nyumba kumi na sita za ndugu zetu na majumba mawili ya Ufalme yaliharibiwa. Chini ya mwongozo wa waangalizi wa mzunguko, makutaniko yanaandaa chakula, mavazi, maji, na makao kwa wale wenye uhitaji. Pia, wazee wa eneo hilo wanawapa wote walioathiriwa faraja ya kiroho.

Tunaendelea kusali kwa ajili ya ndugu zetu walioathiriwa na tetemeko hilo. Tuna uhakika kwamba Yehova atakuwa nguvu na ngome kwa watu wake wanapoendelea kumtegemea.—Zaburi 28:8, 9.